Jumanne Jioni sina uhakika sana but nipe mawasiliano yako ili niwe nayo kwanza ntakushtua ila kikao kingine ni Jumamosi hii tarehe 10 kuanzia saa 11 pale Kilimanjaro Park , Mbele ya Mwika Hall
Harusi siyo ati kama bethdei pati..Kiafrika harusi ni shughuli ya familia,ndugu jamaa na marafiki kama msiba.Usijaribu kuonyesha hiyo jeuri hata kama una pesa... utajikuta unasusiwa mazishi ndugu.Utalia sana likikufika... si una pesa?
tausi
ulishawahi kuchangia lipi kati ya haya yafuatayo:-
- matibabu ya rafiki yako mgonjwa?
- elimu ya mtoto wa rafiki yako
- ujenzi wa zahanati
mimi siwezi kuchangia "shuguli" inayoisha baada ya "shughuli": Hii mnayoita "utamaduni wa kiafrika" kwangu mimi ni "utamaduni wa kijinga"!
Huwezi kumchangia mtu "kuoa" say tshs 200,000: Wakati mtu huyo huyo anaye mdogo wake ambaye anakosa tshs 100,000 za ada ya shule au mama yake mzazi kule kijijini hana tshs 50,000 ya matumizi madogo madogo: That is imbecility of highest order!
Mimi nimeoa bila kufanya "vikao vya harusi" na bila "kuchangiwa". Nilifunga ndoa 10years ago kanisa la mt joseph dar es salaam asubuhi na baada ya hapo sherehe ilifanyika nyumbani kwangu: Waliofika ndugu jamaa na marafiki wenye "mapenzi mema".
Kwa wale wanywaji: Kila mmoja alikuwa anaagiza kwa "pesa yake" kutoka baa ya jirani na chakula kiliandaliwa na majirani.
Nipo na mke wangu for 10 years now blessed with two kids - hutujawahi kwenda "kusuruhishwa" kwa padri au wazee wa kanisa - hata siku moja.
Tubadilike: Ndoa imara haijengwi kwa michango ya harusi - say no to michango:
Kama mwanajamii nimetimiza wajibu wangu kuwajulisha wanajamii wenzangu kuhusu malengo yangu hayo kwahiyo kuchanga au kuchangia au kuwa sehemu ya wanajamii wanaopenda kuwa kwenye kamati ya kufanikisha shuguli hii sio lazima -- lakini ni lazima mimi kutimiza wajibu wa kutaaribu jamii na nimeshafanya hivyo hivyo vingine ni juu ya mwanajamii mwenyewe kuamua
Ndugu Jamaa na Marafiki
Sijaingia kijiwe hichi siku nyingi kidogo muda mwingine tuko kwenye vijiwe vingine hongereni kwa mafanikio yaliyofikiwa na kijiwe hichi kwa miezi michache iliyopita mpaka sasa hivi - lakini kuna wale wakongwe siwaoni siku hizi kama Naima , AmazingFriend Na Haika Wale wa DHW naona nao wapo humu siku hizi lakini haijalishi .
Napenda kuwajulisha kwamba natarajia kufunga ndoa mwezi wa 9 Mwaka huu Maandalizi ndio yameshaanza na Tunaendelea Kawaida tu .
Nawakaribisha Kwa Maombi , Michango na Wale wanaopenda kuwa kwenye Kamati Ya Maandalizi Ningependa sana kuwa na watu wa jukwaa hili japo 20 Hivi itapendeza kujenga Undungu na mengine mengi .
Kuhusu hii kamati Nitawasiliana na Invisible Tuone Itakuwaje Au tunaweza kuanza na hapa hapa
Ahsante na Karibuni Tena