Tangu nimeanza kupiga mazoezi badala ya kupungua naongezeka uzito

Mkuu Kama ulikuwepo Vile, Binafsi Mwezi ulopita Nilipima Uzito nikawa na Kilo71 na niakaanza Mazoezi angalau kupungua sasa Zimeongezeka Kilo 4, Sasa Nashindwa Nifanyaje ila Nimepata ushauri kwa Wadau Nipunguze kula pia Niendeleee na Mazoezi kuruka kamba na Juice ya limau 2×Per day ...... Jahbless Workout
 
kwanza nikupongeze kwa dhati kuamua jambo jema!
lakini naomba nitumie ukurasa huu kutoa darasa,
YAPO MAZOEZI YA KUONGEZA UZITO NA PIA YAPO YA KUUNGUZA UZITO Mimi nafikiri tatizo lako hujafaham, yaani unaunguza na kuongeza pasipo kujua
mazoezi ya kupunguza UZITO ni kama kukimbia, kuruka kamba, kuogelea n.k
na mazoezi ya kuongeza ni kama ngumi,masumbwi,push up, kufanya mapenz n.k
kwa maelezo yako YAPO juu ni dhahili utakuwa unachanganya mazoezi,
pia inashauriliwa epuka kuvaa headphones wakati Wa mazoezi, inatamkwa mazoezi mazuri ni Yale ysnayofanyika ubongo ukiwa free kwa maana ya kufanya mazoezi tu
 
pia kuweni makini na mizani mingine mibovu itawavuruga; tumieni mizani iliyohskikiwa, hususani ile ya kwenye magodown ni mizuri zaidi
 
nimekuelewa mno yaani, asante sana!
 

Itabidi umwone mtaalam wa vyakula au aitwa nutritionist aili akupangie aina ya vyakula.

Ni lazima katika wiki ule vyakula tofauti vyenye virutubisho tofauti.
 
Acha kula nyama Nyekundu.....kula Samaki,Kuku na Mbogamboga kwa maana ya matunda matunda.
Nyama haina mchango mkubwa kwenye kuongeza uzito

Vitu vinavyoongeza uzito ni pamoja na vyakula vya wanga kama ugali,wali mikate, vyakula vya kusindikwa, juice za dukani, sukari, kutopata usingizi wa kutosha n.k

Pia ongeza zoezi la kukimbia angalau ziwe km 3 au zaidi kwa siku

Pia, tatizo wengine wakifanya mazoezi wanapata njaa sana hivyo wanakula sana mwisho wa siku zoezi linakuwa kichocheo cha kuongeza uzito

Kwenye menu yako hakikisha kunakuwa na mboga za majani nyingi na kaugali kadogo. Pia tumia matunda na ukiweza hususani usiku piga desh.
 
Mkuu unamaanisha huyu jamaa asifanye kazi ingine ni mazoezi tuu?Kumbuka mambo mengine yanatakiwa yaendelee pia. Afanye mazoezi kiasi na control aina ya chakula atapungua tuu.
 
Je nguo zako zinabana au zinapwaya.?Yaweza kua umepungua fat lakini umegain muscles hasa kwa vile unapiga sana push up ambacho ni kitu kizuri. Na jee hilo dona unalokula ni kiasi ganI isije kua una consume more calories than what you are burning. Kwa hiyo lazima ubalance your calories intake isije kua kwa vile unapiga mazoezi na ukaamua ndio dona ulipige kama kuli. Obviously usikae na njaa lakini ni muhimu kutizama diet yako.
 
Mkuu hizo push up unazipgaje?
 
Hivi juice ya limao ipoje na inapatikanaje??
 
Dawa ya kupungua uzito ni Stress tu.
Yaani ukivurugwa haswa lazima uperuruke kilo
Tafuta janga likupe kashikashi hadi uvurungwe, nakwambia wiki mbili tu utanyondea hatari.
 
Ndani ya miezi 2 niliweza kupunguza kilo 12… ni mazoezi na nidhamu ya kula…. Jioni ndio muda ambao unatakiwa uwe makini sana na unachokula na mwisho wa mlo wa jioni ni saa 1. Ule chakula chepes sana, mie nakula matunda 2 tu na nimezoea na usingizi nzr saaana.
 
Ugali wa dona unanenepesha sana. Fanya mazoezi then, asubuhi pata chai sukari kwa mbali na mayai + mkate vipande 2 ( mimi asubuhi sinywi chai au natafuna tango tu. Mchana kula kidogo sana kutuliza njaa( sio kushiba, mboga mboga zikiwa nyingi sio wanga). Usiku kula matunda tu ( mimi natafuna tango au nalala bila kula) kwa muda wa week 3 nimepungiza kilo 3 kutoka 78 to 75.
 
Kira zoezi lina faida ktk mwili. So!inawezekana mazoezi ufayo ya kuongeza uzito
 
Pendelea kunywa maji na acha vyakula vyenye high 'carbohydrates', 'fats & oils'
 
Kunywa maji ya vuguvugu especially morning, usitumie mda mwingi kulala, Epuka kulala ukiwa umeshiba, ruka Kamba sana, pia kuna zoezi kama la kuruka matairi hivi kama utakua unafanya lile within a week utapunguza kgs then pia kata tumbo sana
Push ups & squats piga kawaida tu sababu havipunguzi uzito
 
unafanya mazoezi bika kanuni, na kula bila kanuni pia.
Ili nisiandike vingi, ingia google tafuta vyakula vinavyofaa kwa mtu mwenye lengo kama lako.
Ingia youtube angalia tutorials za mazoezi ya kupunguza uzito. Kisha anza kufanya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…