Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Mara, Eng. Vedastus Maribe, amemuomba Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira, kusaidia kushinikiza Serikali kuu ili kuhakikisha barabara muhimu za mkoa huo zinajengwa kwa kiwango cha lami.
Maribe ameyasema hayo wakati wa ziara ya Wasira mkoani Mara, ambapo alitaka kufahamu maendeleo ya ujenzi wa barabara mbalimbali, ikiwemo barabara ya Mika-Kirongwe, ambayo ujenzi wake umekuwa ukifanyika kwa hatua ndogo ndogo.
Akijibu maombi hayo, Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Stephen Wasira, amesema atalifikisha suala hilo kwa mamlaka husika, ikiwa ni pamoja na kuzungumza na Waziri wa Ujenzi ili kuhakikisha barabara hizo zinakamilika.
Amesema ujenzi wa barabara hizo ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya CCM, ambayo inalenga kuboresha miundombinu ya usafiri na kukuza uchumi wa mkoa wa Mara.
Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Mara, Eng. Vedastus Maribe, amemuomba Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira, kusaidia kushinikiza Serikali kuu ili kuhakikisha barabara muhimu za mkoa huo zinajengwa kwa kiwango cha lami.
Maribe ameyasema hayo wakati wa ziara ya Wasira mkoani Mara, ambapo alitaka kufahamu maendeleo ya ujenzi wa barabara mbalimbali, ikiwemo barabara ya Mika-Kirongwe, ambayo ujenzi wake umekuwa ukifanyika kwa hatua ndogo ndogo.
Akijibu maombi hayo, Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Stephen Wasira, amesema atalifikisha suala hilo kwa mamlaka husika, ikiwa ni pamoja na kuzungumza na Waziri wa Ujenzi ili kuhakikisha barabara hizo zinakamilika.
Amesema ujenzi wa barabara hizo ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya CCM, ambayo inalenga kuboresha miundombinu ya usafiri na kukuza uchumi wa mkoa wa Mara.
Raisi Samia alipoingia ikulu pesa za barabara zikakata mfuko wa barabara ukahamishiwa Hazina wazipige vizuri na akina Mwigulu Nchemba, baadhi pesa zinaenda Zanzibar kujenga barabara za huko. Sijui kama Wasira atafanya kitu chochote. Wakandarasi hawajalipwa ni miaka sasa. Bank wanafilisi mali zao.
Raisi Samia alipoingia ikulu pesa za barabara zikakata mfuko wa barabara ukahqmishiwa hazina wazipige vizuri na akina Mwigulu nchemba, baadhi pesa zinaenda Zanzibar kujenga barabara za uko. Sijui kama Wasira atafanya kitu chochote. Wakandarasi hawajalipwa ni miaka sasa. Bank wanafilisi mali zao.
Huwezi fanya chochote, kwani serikali ndo imeshika mpini, watanunua magari ya bei mbaya kupita kwenye hizo barabara, lakini mkandarasi utaonekana huna maana. Enzi hizo zimepita za akina JPM waliokuwa wanathamini ujenzi na miundombinu, lakini hawa wao ni kitchen party, kula bata kupanda ndege na kuiba. Hivyo unaweza kulipwa baada ya 2030 kama huyu Raisi atapita.
NB: usichukuwe mkopo wowote kwa ajili ya ukandarasi watakufilisi.
: mfuko wa barabara ndo unatumika kununua magari ya serikali na pikipiki za CCM ssh, mabasi ya CCM, na kulipa mishahara ya wafanyakazi.
Raisi Samia alipoingia ikulu pesa za barabara zikakata mfuko wa barabara ukahqmishiwa hazina wazipige vizuri na akina Mwigulu nchemba, baadhi pesa zinaenda Zanzibar kujenga barabara za uko. Sijui kama Wasira atafanya kitu chochote. Wakandarasi hawajalipwa ni miaka sasa. Bank wanafilisi mali zao.