TANROADS mnapata hela za kurudisha wakati huku Kibamba tuna lami chini ya asilimia 5 jimbo zima?

TANROADS mnapata hela za kurudisha wakati huku Kibamba tuna lami chini ya asilimia 5 jimbo zima?

Kwaasenga

Member
Joined
Jan 28, 2023
Posts
74
Reaction score
104
Nimesoma moja ya post humu kwamba kwa mujibu wa CAG, Tanroads walikuwa na bakaa kwenye bajeti yao. Nimesikitika sana kwa kweli. Hali ilivyo mbaya sana tena sana kwenye jimbo la kibamba kwa barabara zilizopo chini ya Tanroads, alafu inapatikana hela ya kurudi serikalini? Hii si ni dharau kweli?

Kuna barabara mbovu sijawahi kuona, kutokea mpigi magoe to mbezi kupigia barabara ya msumi na ile ya mbezi high school hizi barabara hazitamaniki kabisa. Watu wanateseka sana kwa kukosa usafiri, dalala zimehamisha ruti zao.

Hivi kweli Tanroads hawapo humu JF? Kwamba hawatusikii wananchi tunavyopata shida? Au mpaka aishi huku mkubwa flani ndo mtajenga?

Ikifika muda wa kuweka hata kifusi hakiwekwi, kinachofanyika ni kuparua parua kwa juu, baada ya siku mbili mahandaki yanaanza upya.

Tanroads mnatutesa wananchi.
 
Poleni sana, nadhani Jimbo la KIBAMBA ndio majibo ambayo Yako nyima sana kimaendeleo, hata mradi wa DMDP haujawahi kuwanufaisha.

Mkuu wa Wilaya, mbunge na diwani wanapaswa wachangamke.
 
Poleni sana, nadhani Jimbo la KIBAMBA ndio majibo ambayo Yako nyima sana kimaendeleo, hata mradi wa DMDP haujawahi kuwanufaisha.

Mkuu wa Wilaya, mbunge na diwani wanapaswa wachangamke.

DMDP iliishia Ilala, Temeke na Kinondoni. Lkn kama Tanroads hawatajenga barabara zao, DMDP haitatunufaisha kwa maana inajengaje barabara za Tarura kuja kuunga kwenye barabara kubwa za tope za Tanroads??
 
DMDP iliishia Ilala, Temeke na Kinondoni. Lkn kama Tanroads hawatajenga barabara zao, DMDP haitatunufaisha kwa maana inajengaje barabara za Tarura kuja kuunga kwenye barabara kubwa za tope za Tanroads??
Nimewahi kufika Jimbo la KIBAMBA wakati wa utawala wa Makonda, tulifika maeneo ya kiluvya kituo kikubwa Cha Polisi na aliwaahidi kuwapa KM 21 za lami ktk maeneo hayo ya kiluvya hondogo. Lkn ndg. Makala hajawahi kutekeleza Tena.

Nadhani kama TARURA wanapiga basi wanapiga kupitia fedha za Jimbo Hilo kwasababu viongozi na wananchi wmelala fofofooooo
 
Barabara ya Kwenda Msumi na hizi mvua ni hatari. Ukifika Mbezi stand kama unaenda Msumi na haujawahi kufika Wala usimuulize Mtu Gari ziko wapi. Angalia magari yaliyochoka na makuu kuu ndio hayo ya Msumi sasa.

Air Msumi…Mvua ikiwa inanyesha na nyie kulowana NDANI ya Gari ni kawaida.

Wakati wa kiangazi Kupanda ukiwa msafi na ukashuka ukiwa kama ulikuwa na kibarua cha kujipaka vumbi ni kawaida na usishangae ukiona Mtu anakucheka baada ya kushuka.
 
Hili jimbo liko vibaya sana kwa kweli
Mbunge wenu Issa Mtemvu si ndio mwezi huu bungeni alipendekeza sura ya Mama Samia iwekwe kwenye pesa. Kumbe jimbo lake wana shida kibao ila hajui vipaumbele
 
Barabara ya Kwenda Msumi na hizi mvua ni hatari. Ukifika Mbezi stand kama unaenda Msumi na haujawahi kufika Wala usimuulize Mtu Gari ziko wapi. Angalia magari yaliyochoka na makuu kuu ndio hayo ya Msumi sasa.

Air Msumi…Mvua ikiwa inanyesha na nyie kulowana NDANI ya Gari ni kawaida.

Wakati wa kiangazi Kupanda ukiwa msafi na ukashuka ukiwa kama ulikuwa na kibarua cha kujipaka vumbi ni kawaida na usishangae ukiona Mtu anakucheka baada ya kushuka.
😂😂😂
 
Nchi nyingi za Afrika zina milolongo mirefu ktk kutekeleza masuala ya maendeleo mpaka watakwambia sijui upembuzi yakinifu unafanyika kabla ya kujenga barabara tena upembuzi huo huchukua mwaka au zaidi wakishamaliza hapo utasikia Serikali inatafuta pesa yaani we acha
 
Mimi naomba mtu mmoja anayehusika na hizi barabara au anayejua vizuri kuhusu barabara ya kutoka pugu, kifuru, mbezi mwisho, mpigi magoe mpaka bunju inapita wapi?? Je, ni hii ya kupita makabe, kupita mbezi high school au kupita kibamba shule??
 
Back
Top Bottom