mkuu ni kutoweza tuu kupata picture ya kisemacho,sipendi sema unaanza thibitisha pia kuwa kifikra upo nyuma sana ya vyeti ulivyo navyo.
Hizo nchi na miji ni nortorius kwa chao za "barabarani" kule india Ng`ombe ana nafasi barabarani, bajaj, watembea kwa miguu, magari, tembo n.k. na wote wanafuata upenyo uliopo.Mifano yangu ipo sahihi sana tofauti na unavyoweza ikataa kirahisi tuu.Nimekuambia suala la magari barabarani,ni mamlaka na wala si la elimu ya darasani kwa raia.Hizo mamlaka ndio zinahitaji kuwa na watu wenye utaalamu wa mambo ya traffic flow.Raia wa kawaida ana mashinikizo ya maisha, ana majukumu na malengo ya kufikia kila siku,watu wa dar ni wa kutoka maeneo tofauti ya nchi na nchi jirani.Kwao lazima wafike na chakula nyumbani, wafikishe kiwango cha mwenye basi etc.Nimekupa mfano wa somalia,huweze enda wagawia chakula halafu useme kuwa wagawane kwa mpangilio.Kitakacho waongoza si elimu wala akili,il njaa na hamu ya kuchukua kingi kama akiba.
[/FONT]Majenngo? sidhani kama nimelinganisha majengo tuu..nimesema wametupita vitu vingi,nikitegemea utashi na elimu yako itakupelekea ku recaal couples ya uvijuavyo.Kma miundombinu, elimu(usitoe tuu mfano wa vyuo vya chini ila pia na vya juu ,kwani vya juu ubora wake hatuna Tanzania nzima).
Sijui unamaanisha nini kuhusu vyeti feki au pengine huelewi.Mi nafahamu feki ni kitu kisichotoka kwa mtengenezaji au mtoaji,ila kinaigiza kitu cha mtoaji halali.Kama unaaamisha feki kama cheti basi TCU inabdi waweke mashine ya kucheki vyeti.Vyeti feki ina maana huyo mtu ama hakusoma kabisa hiyo fani au hakufikia pata vyeti.Kama unataka leta nortion ya Feki kama elimu duni basi utakuwa umepota zaidi.
Elimu duni si vyeti feki, labda useme marks feki, au hata maksi zisizostahili.kama vile mtu kupewa maksi kza juu katika vyeti na katik kumbukumbu za computer kwa kutumia watu wa ndani.Haya yanaweza ambatana na feki.Hapo tutakaribiana kifikra kwani hapo ndipo ninaposema TCU hawajapashika.Hawan vipimo kuwa mwanafunzi alivujishiwa mitihani na walimu, au alipewa alama na mwalimu za bure katik assignments na hivyo kumjengea mazingira ya kupata madaraja ya juu pasipo kuwa na huo weledi.
Ukweli ni kwamba kuna shida sana katika mifumo inayotegemea marks za mwisho.Na hivyo kufanya thamani ya vyeti vitolewavyo na vyuo vingi kuwa hovyo. Na hii ipo kuanzia huko ulipo asia hadi Africa.Unachoongelea hapa ni kama kunishawishi niamini kuwa hela huweza nunua mapenzi kila mahali.
India ina spectrum ya ajabu sana, India in Polution kubwa sana inayokwenda kwenye billion, na ukubwa wa nchi unaifanya iwe kama bara(ni sub continent), kwa hiyo kuna kufanikiwa kwa ndani,yaani kampuni inaweza kuwa tajiri sana kwa kufanya biashara ndani ya india pekee.ratio ya matajiri na masikini kwa India ni ndogo sana, ila ktik hiyo fraction ukilinganisha idadi ya watanzania utaona ni watu wengi sana.Ila sehemu ya jamii iliyo na elimu kubwa si kubwa hivyo, na miji kama Mumbai inavuta wasomi wengi zaidi na hivyo kuifanya india ionekane kuwa ni ya wasomi ,ila kwa ujumla india kama taifa bado halijaelimika.Pakistani ndio taabu kabisa.
Hakuna anayekataa elimu ni ya msingi kwa afya na uhai wa any civilization.Ila hapa issue si hiyo hapa issue ni mlinganisho wako wa Zanzibar na Bara katika ratio ya vyuo .Ila katik ubora hujataka kubali ukweli kuwa Zanzibar wana mwendo mrefu hadi waweze ingiza elimu bora katik hayo majengo na taasisi za elimu.Ili watoe watu walio bora kama unavyotaka aminisha watu hapa.
Km wewe ni mmojawapo ya watu wanaoamini kuwa West waliiba elimu toka kwa waarabu,there is no doubt huwezi kuwa na fikra mbadal linapokuja suala za Zanzibar na Bara.Nilishawahai jiuliza kama taaluma zilitoka huko ulipo kwanini sasa wasiwe kwa kwanza kujua matumizi ya mafuta?kwanini basi wasiwe wa kwanza rusha rocket kwenda space?Ndugu yangu upo mbali sana na ukweli, naona umejisahau sana hadi kduharau watu kirahisi.
Usiwe naive ndugu yangu, katika hiyo mihadhara huwa unapewa platiform ambayo inakuwa one way traffic, huku watu wakiwa na shauku ya kukuona ,pia unaweza kuwa ulikuwa ukilindwa na timetable,kama kuna speakers wengine basi watu hawawezi ondoka kwani kwani kuna watu wengine wanafuatia.Pia ujue unaweza kuwa ulikuwa katik minajili ya dini na hivyo kuwafanya watu wasiangalie sana area nyingine.Hizo titles zako zilisaidia tuu watu wakusilikile ila si kwamba ulikuwa that credible.NAOMBA NEXT TIME INGIA KATIKA DIALOGUE NA WASOMI WENGINE halafu uone jinsi haukubaliki kihivyo.
Teh teh, niache uvivu gani tena wa computer halafu nitembelee website ya TCU?websiete yenyewe kwanza ni ya ubora wa chini sana.
Labda nikupe ukweli tuu ili taabu iishe, huko ungangani ulipo elimu yao ni mushkeli sana ndio maana sioni ajabu kuwa unaiona zanzibar ina elimu kubwa sana.Ni watu wangu wa karibu sana watoto wao wapo Tanzania wanasoma.Na wameweka wazi kabisa kuwa elimu yetu ipo juu sana kuliko ya huko ulipo.Na hii inatokana na watu misguided kama wewe.Mnajipigia debe na vyeti vyenu ,ahalfu mnakuja ongoza uongozi wa hizi taasisi.
Investment ya shule katik bara hasa kwa taasisi binafsi huwezi fananisha na zanzibar katik miaka ya karibuni.Labda wafungue milango wadau wengine wenye mitazamo tofauti waingie.Shida ni kwamba washauri kama ni aina yenu zanzibar aitabaki katik ndoto,na hawatajua wapi wamekosea.Watabaki kudhani wanafanyiwa hila.Nimeelezea shida nyingi za zanzibar naona umepiga kimya kwa vile hazina maslahi nawe katik hizi propaganda.Hizo shida ni baadhi tuu ya zinazoweza waletea wazenj uhuru wa kweli.