Tanzania close to securing funding for second phase of SGR project

Uwe unafahamu kusoma Phase 1 inagharimiwa na Serikali ya Tanzania 100%. Ikiisha na hakuna wa kumkopa tutaendelea wenyewe, lakini kwa sababu wapo ambao wapo tayari kutukopa kwenye phase II basi tutakopa kwa sababu uwezo tunao.

Tungekuwa na uwezo basi deni lingekuwa linapungua siyo kuongezeka.
 
Nakupa mfano mmoja tu. Huko ngara ambapo SGR itapita hadi Kigali mkungu wa ndizi ni shs 200 kwa sasa. Dar mkungu wa ndizi huo huo ni 20,000. Tatizo usafiri kutoka ngara hadi Dar inachukua siku 3 kwa lorry hivyo ndizi zitaiva. SGR itatumia masaa 10 kutoka Ngara hadi Dar. Hivyo bei ya ndizi itapanda huko Ngara na Dar itashuka maana zitakuwa ni nyingi. Niendelee au nisiendelee
 
sijui nijieleze vipi,

Kwanza hii miradi yote itakuwa na mandatory zipi ili pesa zilizotumika zirudi ili kulipa madeni kama hakuna nadiriki kunena hivi watanzania akili zetu zipo makalioni
 
Asante mkuu,sasa wadanganyika wanadhani uchumi utakuzwa na SGR,hawajui kuwa ile ni reli tu na ili izalishe pesa lazima kuwe na mizigo ya kupita juu yake,sasa kama watanzania si productivity sijui hiyo mizigo itatoka wapi?anyway hao hao ndo wanaaminishwa na Magufuli kwamba Serikali ina pesa nyingi while wao wamechoka sasa sijui huwa wanafikiri serikali inapata wapi pesa nyingi wakati wananchi wake wengi wamechoka
 
Na kuna mikungu mingapi hapo ngara?hata huko ngerengere kuna magunia kadhaa ya mahindi na bei ni ndogo kuliko dar,the questions kuna production ya kutosha kuwatoa watu kwenye umaskini au wewe mtu akishapata hiyo 20,000 hata kama anauza mikungu 100 kwa mwaka ndo atauaga umasikini?
 
Uwe unafahamu kusoma Phase 1 inagharimiwa na Serikali ya Tanzania 100%. Ikiisha na hakuna wa kumkopa tutaendelea wenyewe, lakini kwa sababu wapo ambao wapo tayari kutukopa kwenye phase II basi tutakopa kwa sababu uwezo tunao.
Wapo tayari kutukopesha. Watakapo anza kutukopa basi tutakuwa DONA KANTRI inshallah.
 
uchumi wa nchi unaanzia hapa 👇 👇 vinginevyo nchi inakwenda zigzag style
Gross Domestic Product—GDP
 
Tulisema tunajenga na pesa za ndani
Vipi mishikaki ya nundu imeisha? Basi nitaleta viatu kusafisha.
Lakini pia unatakiwa kuelewa unapokopa na kulipa deni, nani anakuwa ametekeleza huo mradi? ?
 
Jina baya liliharibu mtoto! Mtoto akijiita sijijui kubali kuwa hajitambui. Wewe ni mbishi tu. Angalia mfano mwingine, kabla ya kupita barabara ya lami, kwa kawaida huwa vijumba ni hohehae lakini ikiwa ni lami huwa ni mabadiliko ya maana. Sembuse train ambayo inaenda kwa kasi?. Pili hii train itakuwa inabeba mizigo mingi. Fikiria mtu wa Kahama, ataweza kusafirisha sementi toka Dar kwa bei ndogo na simenti Kahama itapungua bei kwani monopoly ya sementi haitakuwepo, hayo si maendeleo? Achana na masuala ya ngerengere think outside the box. Hata watu wa ngerengere haitakuwa lazima apange nyumba hapa mjini, itakuwa ni rahisi kulala ngerengere na kwenda Dar kufanyakazi kila siku. Niendelee nisiendelee
 
Una fikra duni kweli kweli, hivi kwa mfano Precision air ipo kwa ajili ya vingunge au matajiri au wateja.
Elewa mambo ya kiuchumi sio tu kwamba jambo husika lina impact gani kiuchumi na sio tu limegusa watu wangapi directly kuna wengine wana guswa indirectly
 
sijui nijieleze vipi,

Kwanza hii miradi yote itakuwa na mandatory zipi ili pesa zilizotumika zirudi ili kulipa madeni kama hakuna nadiriki kunena hivi watanzania akili zetu zipo makalioni
Kama zako ambazo umewekeza ktk vitu ambavyo hatuna mandatory ya kuvinunua
 
Sijui na Makinikia, na wenye fikra kama zenu,
Naomba mfiche ujinga nchi haiwezi kuacha kufanya project kama hii , tukikusubiri wewe uongeze tija, ukitilia maanani mahindi ni zao la msimu moja wakati ujenzi was reli ni project ya muda mrefu hivyo huwezi kuyaweka ktk mpangilio sawa.
Na zaidi ya hapo kauli ya Raisi kwamba hato panga bei ya mahindi na una ruhusiwa kutafuta soko mwenyewe ni motivation ya kutosha au unataka serikali ije kukulimia
 

Hakuna bank yoyote duniani inayemkopesha mtu ambaye hawezi kulipa. Hata wewe huwezi kumkopa mtu ambaye unafahamu kabisa hawezi kukulipa.
 
Kama wewe ni hohe hahe kalaga baho.
 

Kumbe unafahamu vinavyotumika? Uwe unafahamu na kutambua fani za uanduishi wa habari basi, mimi nimeleta habari kama ilivoripotiwa. Kama ni ya uongo haina facts pinga kwa facts weka wewe picha ambayo ni halisia basi tutakupigia makofi then pinga hoja ya story yenyewe haya mengine huwa tunaita maloloso tu.
 
Ni juzi tu alisema tuachane na misaada na mikopo, hatuna sababu ya kukopa kwa sababu tu yupo mkopeshaji, huo ni ujinga.


Mikopo ambayo hata wewe binafsi hutakiwi kuichukua ni ile ya riba kubwa. Utakuwa kichaa kuuza nchi kwa mikopo kama hiyo. Mikopo ya bei nafuu ndio wengi tunakopa kama hutaki shauri yako sisi tunasonga mbele.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…