Tanzania hoi kwa furaha duniani

Hii ni sawa na mwanafunzi aliyefeli lakini anafurahia kwa vile katika mpangilio wa majina, jina lake limetangulia kuorodheshwa.

Siku zote, balow 50%, wewe ni failure.
 
Asa mtu unapata wapi furaha ukigeuka huku Makonda ukigeuka huku sukari hamna mara polisi wameruhusiwa kuchukua ya kubrashi viatu mara unasikia kitita kipya nhif kimetoka
 
Nikashangaa eti mama juzi anaongea eti Tanzania ni ya 4 sijui 6,sijui 8 kwa furaha?.
Nikacheka. Nikajua tayari machawa wamefanikiwa kumuingiza mama chaka au kujifariji ingali ukijua kabisa 90% ya wananchi masikini wa kutupwa watapata wapi furaha il-hali mlo mmoja tu kwa siku unawasumbua?.

Achilia mbali watapata wapi furaha il-hali wale wenye kutumia nguvu kutafuta riziki kwa kutumia umeme unawakatikia siku nzima.
Wafanyabiashara kunyanyaswa na TRA watapata wapi furaha?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…