Tanzania ilikuwaje Miaka 1,500 iliyopita

Masulupwete

JF-Expert Member
Joined
Feb 15, 2012
Posts
2,366
Reaction score
2,424
Wakuu stori inayotrend saivi ni tamko la mamlaka za Uturuki kubadili matumizi ya jengo la kale la Hagia Sophia lililojengwa mwaka 537 (yapata miaka 1,500 iliyopita) kutoka kuwa makumbusho na sasa kuwa eneo lakuabudia.

Miaka 1,500 ni mingi sana kwa historia ya mwanadamu.

Nimejiuliza sana hawa wenzetu walifanya haya yote miaka 1,500 iliyopita. Hivi wakati huo sisi tulikuwa tunafanya nini au nini kilikuwa kinaendelea huku kwetu?
 
Babu zetu walikuwa wanawinda tu huko,
 
Mimi naamini hizo early years hapa kwetu Tanzania palikuwa ni "No man's Land".

Sisi tulikuwa Kongo huko au Central Africa migrating from the Desert.

Sehemu kama Raptah,Azania,Zanzibar,Kilwa zilikuwa kama vijiwe vya mabaharia kukutana ili kufanya biashara,na kupumzika(kupata maji fresh na kadhalika.Baadae waliamua ku-explore ndani--na sisi tukitokea humo ndani tukakutania katikati.

Intermarriages zikatokea,wengine ndio wakabaki humohumo.

Ni mtazamo tu!
 
Picha za kariako za 1920's palikua ni kijiji full nyumba za udongo hapo.

Nadhani miaka 1500 iliyopita nilikua nashinda juu ya miti nikiwa nakula matunda na asali huku nikicheza cheza na wadogo zenu huko mitini.
[emoji23][emoji23][emoji23]mkuu nirejeshee mbavu zangu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…