Tanzania ilipangwa na timu ngumu sana

Tanzania ilipangwa na timu ngumu sana

Tunaipongeza serekali ya awamu ya tano kuziwezesha timu za kundi la taifa stars kutinga hatua ya fainali...vivaa jiwe
 
Wakuu, kama tulivyoona timu mbili tulizo pangwa nazo kwenye makundi zote zimefika fainali

Algeria wameifunga nigeria 2-1,Senagal wameicharaza Tunisia 1-0 (hatua ya nusu fainali)

Kwa nilichokiona, Tanzania ilipangwa na timu ngumu sana na wala haziwiani katika viwango vya mpira

Huwenda labda tungepangwa na timu nyingine, tungejipatia pointi kazaa au tungefuzu 16 bora..

Bingwa na mshindi wa pili anatoka kwenye kundi letu, hii inaonesha ni kwa jinsi gani ilikuwa ngumu kwa taifa stars kufuzu hatua inayofata
Kwa hiyo unashauri mashindano yaanze upya? CCM Stars nayo ni timu ngumu sana
 
Hapana hao tunge wapiga kama tusingewaacha akina mkude, Banda na ajib pia kocha asingekuwa amunike tungerudi na kombe

Dah! andika Amunike sio amunike! Ukweli ni kwamba hamna kikosi cha kuchukua ubingwa hata kama kocha angekua wewe.
 
Hizo timu ulizotaja zote ni bora kuliko kenya! .. Huyo kenya kibonde sasa alipokutana na Tanzania dah .. ngoja tulale tu
yaani mkuu .usipotaja kenya ni kama hujacoment eti,sasa kenya na mazumgumzo yenu juu ya taifa stars yanaunganikia wpi majameni. Kenya itabaki juu kileleni chiiii .
 
yaani mkuu .usipotaja kenya ni kama hujacoment eti,sasa kenya na mazumgumzo yenu juu ya taifa stars yanaunganikia wpi majameni. Kenya itabaki juu kileleni chiiii .

We mkamba unasemaje?
 
Bila shaka una usingizi kalale kwanza huwenda umeandika ukiwa umefumba macho.
Utakapoamka naomba unijibu.
Unafikiri ni timu gani ingeweza kufungwa na Tanzania katika Afcon ya mwaka huu?
Na kwanini unafikiri hivyo?
Kwa ufupi hatukuwa na team ya kwenda AFCON hatukustahili tulilazimisha ila bado uwezo achana nae huyo anaejipa moyo eti tulipangwa na kundi gumu kila team ilikwenda kupambana na yeyote
 
Back
Top Bottom