Tanzania iliwahi kuwa nchi ya tatu kwa upelelezi duniani

Tanzania iliwahi kuwa nchi ya tatu kwa upelelezi duniani

Mbona kuna nchi zinafahamaika kwa majeshi zinaongoza duniani. Iweje intelligence agency tu ndo zisirankiwe? Wanazuoni niwaulize kwani ni lazima kila kitu kirankiwe kwa kuangalia quantitative data tu? Ina maana hatuwezi kujua kitu fulani ni cha ngapi kwa kuangalia qualitative data. Kama hatukuwahi kushambuliwa, na kama siri za usalama hazikuwahi kugunduliwa, na kama mbinu za majasusi ziligunduliwa mapema kabla madhara hayajatokea kwa nini tusijilinganishe na mataifa mengine na kujipa nafasi stahili? Mimi naweza kukubali kuwa huenda miaka hiyo intelligencia yetu ilikuwa ya tatu.

Nikuulize swali ndugu Mabaghee kutokana na maswali hayo hayo uliyouliza anayegundua siri za usalama wako anakuambia kua tumegundua siri za usalama wenu? unaposema siri za majasusi kugunduliwa mapema kabla madhara hayajatokea mna uhakika gan kua jasusi hajatoa siri yoyote kuhusu usalama wenu ( refer to Cohen ) na hayupo au hawatakuwepo wengine? anayesema TISS ilikua ya tatu atupe details za nini kiliwafikisha hapo na miaka gan sio maneno matupu na atupe top three tujue nani wa kwanza na nani wa tatu.. Jeshi ni tofauti na idara za ujasusi JWTZ ikinunua ndege za kivita Urusi, haitatangaza itafanya siri yake lakini mrusi atajua kila kitu kwasababu ndo kakuuzia, majasusi tunawazalisha wenyewe na kuwatuma wenywe kisiri hatuuziwi na mtu! Nakubali idara yetu ilipata heshima lakini hili la kua wa tatu nani kasema? hiyo CIA, FSB,Mossad na M16 ndizo taasisi zinazosifika lakini kila mtu ataichagua yake kwa vigezo vyake na huwez toa ranking yako kidunia ikatambulika na kua recorded kama zilivyodata za uchumi wa dunia kwamba tunajua anaanza Mmarekan anafuata China then Japan hili dunia nzima wanajua na wamelirecord. Kwenye intellijensia ni tofauti tutabaki kuhisi tu na ikishakua kila mmoja ana yake as the best bas hizo takwimu sio FORMAL bali ni INFORMAL!
 
Hizi story tulikuwa tunadanganyana baada ya kusoma vitabu vya Willy Gamba?
 
Sikuizi hawa wanausalama ndo wanaongoza kujitaja bar na kwenye vijiwe kuwa wao ndo usalama wa taifa..wewe nenda mtaani kwenu ukaulize nani usalama wa taifa uone raia watavokutajia enzi za mwalimu these people where silent as if they didnt exist..hata hao pccb wa rushwa kazi yao kulopoka tuuu nakutishia watu kuwa unanijua mm ni nani..hii yote inatokana na jinsi ya wanavochukuliwa kwenda masoni wanachaguana sana kiujamaa.
 
Ukiniambia Tanzania iliwahi kuwa nchi ya tatu kwa uzalishaji wa katani, utaniambia ni kwa tani, na mwaka. Na rekodi za World Trade Organization ambazo zipo na zinakubalika.

Of course kina Kiranga wanaweza kuzibishia, lakini Kiranga anaweza kubisha kwamba yeye mwenyewe ana exist, so that's entirely a different level of scrutiny.

Ukiniambia Tanzania iliwahi kuwa nchi ya tatu kwa upelelezi duniani, utanipa kigezo gani?

Hapo kwenye ready huo sio ubishi sasa ni uhuni
 
Hapo kwenye ready huo sio ubishi sasa ni uhuni

Kiranga hajabisha, amesema anaweza kubisha. Jua tofauti iliyopo hapo.

Na uhuni, kwa kiasi chake, sio mbaya sana kama unavyosingiziwa. Bila uhuni hakuna maendeleo.

Tatizo letu sio kwamba hatuna heshima sana.

Tatizo letu tuna heshima sana, na uhuni kidogo sana.
 
kwa hiyo.......wa zamani walikuwa hadi darasa la saba

Kuna kazi nyingine ni Mungu tu anakuwa kakupa kipaji uifanye vizuri. Kwa kadri ya simulizi, nasikia kitu kikubwa katika kazi hii ni ukweli, umakini, uaminifu na usiri. Unaweza kabisa kupata sifa hizi katika mtu aliyeishia la pili. Wakati wa vita ya wenyewe kwa wenyewe kule Marekani, wapiganaji wa majimbo ya kaskazini waliokuwa wakipinga utumwa waliwatumia wapelelezi weusi katika majimbo ya Kusini mwa america wasiokuwa na elimu lakini waliokidhi sifa hizi nilizozitaja, yaani ukweli, umakini, uaminifu na usiri na ni hawa hasa waliofanikisha ushindi. Fanya Google kutumia maneno "Black Dispatches" utapata simulizi hizi za kusisimua kuhusu mashushushu weusi wakati wa vita ile na kazi kubwa waliyoifanya kupeleka ushindi kaskazini. Elimu kubwa ni muhimu, lakini si lazima.
 
Kiranga hajabisha, amesema anaweza kubisha. Jua tofauti iliyopo hapo.

Na uhuni, kwa kiasi chake, sio mbaya sana kama unavyosingiziwa. Bila uhuni hakuna maendeleo.

Tatizo letu sio kwamba hatuna heshima sana.


Tatizo letu tuna heshima sana, na uhuni kidogo sana.

Mkuu hebu nieleweshe mazuri ya uhuni
 
Machakato mzima tunaambiwa uliratibiwa kwa muhusika (target) kuchunguzwa toka akiwa shule ya msingi....leo hii HUNA UNAYEMFAHAMU huwezi ingia USALAMA wa Taifa.Taasisi ambayo ni nyeti kwa mustaakabali wa taifa haipaswi kuwa ya Kindugu na kufahamiana (urafiki). Kama kuna ubovu tunauona leo basi inaweza kuhusishwa na haya angalau machache yanayotokea.
 
Mkuu hebu nieleweshe mazuri ya uhuni

Kwanza nieleweshe uhuni unauelewaje? Definition yako ya uhuni ni nini?

Tusije kuwa tunaelewa vitu viwili tofauti kwa neno moja hilihili kutokana na mitazamo yetu ya maisha.

Shilingi moja ile ile watu wawili wanaoiangalia kutoka pande tofauti watakwambia wanaona vitu tofauti.

Mwingine atakwambia anaona mwenge, mwingine atakwambia anaona kichwa.
 
Kwanza nieleweshe uhuni unauelewaje? Definition yako ya uhuni ni nini?

Tusije kuwa tunaelewa vitu viwili tofauti kwa neno moja hilihili kutokana na mitazamo yetu ya maisha.

Shilingi moja ile ile watu wawili wanaoiangalia kutoka pande tofauti watakwambia wanaona vitu tofauti.

Mwingine atakwambia anaona mwenge, mwingine atakwambia anaona kichwa.

Mkuu kwa uelewa wangu uhuni ni kufanya jambo ambalo lipo kinyume na maadili na taratibu za jamii husika kwa makusudi kwa mfano kwa kijana wa kiume kuwa na wanawake wengi huo ni uhuni. Hebu niambie na wewe una uelewaje uhuni
 
Kuna kazi nyingine ni Mungu tu anakuwa kakupa kipaji uifanye vizuri. Kwa kadri ya simulizi, nasikia kitu kikubwa katika kazi hii ni ukweli, umakini, uaminifu na usiri. Unaweza kabisa kupata sifa hizi katika mtu aliyeishia la pili. Wakati wa vita ya wenyewe kwa wenyewe kule Marekani, wapiganaji wa majimbo ya kaskazini waliokuwa wakipinga utumwa waliwatumia wapelelezi weusi katika majimbo ya Kusini mwa america wasiokuwa na elimu lakini waliokidhi sifa hizi nilizozitaja, yaani ukweli, umakini, uaminifu na usiri na ni hawa hasa waliofanikisha ushindi. Fanya Google kutumia maneno "Black Dispatches" utapata simulizi hizi za kusisimua kuhusu mashushushu weusi wakati wa vita ile na kazi kubwa waliyoifanya kupeleka ushindi kaskazini. Elimu kubwa ni muhimu, lakini si lazima.
tuko pamoja......sasa nashangaa mtu anasema hawa polisi wa siku hizi hamna kitu kabisa kwa sababu wanachukuliwa hadi wenye four za 32 utafikirielimu kubwa ni ni kigezo cha kuwa askari bora
 
Ndugu zangu,ili nchi iwe nafasi za juu ki intelgesia kuna vitu vingi wanangalia aisee,mojawapo ni technologia na umahiri au uwezo wa taifa husika au watu wapelezi kimataifa,.Tanzania haipo hata top 100,kwanza Tanzania haina maslai nje ya nchi kama wengine au kitisho kikubwa na uchumi mbovu. Sikia niwaambie
nchi ya kwanza kwa ujasusi duniani ni1.Pakistan(ISM)
YA PILI 2.U.S.A (CIA)
YA TATU BRITAIN .M16
YA NNE NI FSB YA URUSI
YA TANO NI MSS YA CHINA
YA KUMI NI MOSAD YA ISRAEL.
 
Sidhani kama tuliwah hata kushika kumi bora.......Bongo hii hii...au nyingine???:mvutaji:
 
Niliwahi kusikia ila sikufanya utafiti zaidi kwahiyo sisi ni wakali upande wa upepelezi basi inabdi mataifa makubwa yatutambue na yatupe kipaumbele pindi muafaka
Ndugu wana bodi,wakati nikiwa mdogo enzi za mwalimu kuliwahi kuwa na uvumi kuwa Tanzania ilikuwa na idara nzuri sana ya TISS hata ikawa nchi ya Tatu kwa upelelezi duniani.

Kwa upande mmoja naweza kuona ukweli wa hili nikijaribu kulinganisha TISS ya enzi za Nyerere na TISS ya ezi hizi,nakumbuka wapelelezi wa enzi hizo wengine waliweza hata kuwa kama vichaa kwa kuvaa nguo chafu ili waweze kukamilisha upelelezi na wakafanikiwa hata kuwakamata makaburu waliokuwa wanakuja nchini kutoka Afrika kusini kwa njia za pori,lakini siku hizi wasomali wanaingia nchini na kutoka wachache ndo kuwa wanakamatwa tena na polisi kwa kupewa taarifa na raia wema na sio TISS.

Naomba michango yenu wana bodi kuhusu jambo hili ukilinganisha na haya matukio yanayotokea kwa sasa.
 
tuko pamoja......sasa nashangaa mtu anasema hawa polisi wa siku hizi hamna kitu kabisa kwa sababu wanachukuliwa hadi wenye four za 32 utafikirielimu kubwa ni ni kigezo cha kuwa askari bora

mgogoro uliopo katika jeshi la polisi la tanzania ni mchanganyiko wa kitu zaidi ya kimoja. elimu duni ikiwa moja ya matatizo hayo. Kwa hiyo ni sahihi kulaumu tatizo la elimu kwa kuwa ni moja katika matatizo ambayo yanaonekana kuwapo katika jeshi hili; lakini kuna exceptions! Kwa hivyo SI sahihi kufanya condemnation za kijumla-jumla. Kwa hiyo kama kuna kosa linafanywa na jamii ni kule kufanya stereotyping; kufanya blanket statement kuwa askari polisi woooote wana ufinyu wa elimu. Wakati kuna exceptions!

Yupo askari polisi mmoja pale IB ambaye namjua kwa jina na sura yake ana elimu ndogo sana ya darasani, lakini Mungu alimpa kipaji cha uchoraji. Leo ukimsimulia habari za sura ya mtu fulani kwa maneno, kesho ataichora hiyo sura almost exactly ulivyoelezea. Nataka kusema vipaji vina nafasi katika utendaji, lakini pia si kila askari polisi mwenye elimu ndogo ana kipaji. Kwa hiyo hatuwezi kudai kwamba askari polisi woooote wenye elimu ndogo wana kipaji. Hapo pia kutakuwa na exceptions.

Nadhani malalamiko yamekuwa yakiongezeka dhidi ya polisi kwa sababu exceptions za walio na elimu ndogo katika jeshi la polisi pasipo kipaji zinazidi exceptions za askari polisi wenye elimu ndogo lakini wakiwa na kipaji. Makoroma ni mengi zaidi kuliko nazi katika jeshi hili.
 
Niliwahi kusikia ila sikufanya utafiti zaidi kwahiyo sisi ni wakali upande wa upepelezi basi inabdi mataifa makubwa yatutambue na yatupe kipaumbele pindi muafaka

Weka past tense kwenye hiyo red yako. Sema kwa hiyo sisi tulikuwa wakali upande wa upepelezi kabla ya hawa wababaishaji waliopo kupewa kazi siku hizi kwa kigezo cha dini.
 
Back
Top Bottom