Tanzania ina mambo ya ajabu sana; Uhamiaji inanyima watu wanaotusaidia uchumi work permits, wanapofunga ofisi na kuaga Serikali inawaomba wasiondoke!

Tanzania ina mambo ya ajabu sana; Uhamiaji inanyima watu wanaotusaidia uchumi work permits, wanapofunga ofisi na kuaga Serikali inawaomba wasiondoke!

Niliwahi kusema humu JF kwamba Tanzania ina mambo ya ajabu sana kuhusiana na utoaji wa work na residence permits hata kwa watu ambao ni wawekezaji, japo kila siku tunapiga kelele eti kuvutia wawekezaji.

Wawekezaji wanapokuja wanapata shida sana kupewa work au residence permits. Kuna wawekezaji Tanzania wamekaa zaidi ya miaka kumi nchini na wengine hata kuoa au kuolewa na Watanzania lakini bado wananyimwa permanent residence permits. Kuna wageni toka nje wenye utaalamu wengi sana Tanzania ambao wameoa au kuoelwa na Watanzania na kuwa na familia, lakini hata hawa hawaruhusiwi kufanya kazi nchini kwa ajili ya kutunza familia zao, wananyimwa work permits japo ni wake au waume wa Watanzania na serikali inasema haiwatambui kama wakazi wa kudumu nchini!

Hivi kweli kweli kuna watu na akili zao serikalini na huko Uhamiaji na hawaoni kuna tatizo hapa?

Kichekesho cha mwaka ni hili la hii NGO ya WUSC kutoka Canada. Wao walikuwa na ofisi nchini kusaidia na kutoa mafunzo kwa watu na taasisi mbalimbali nchini na hata za serikali. Wamekuwa na mchango mkubwa sana taasisi kama Chamber of Commerce (Women), Umoja wa Wakulima wadogodogo nchini (MVIWATA), Umoja wa Wajasiliamali wa Wahitimu wa Chuo Cha Sokoine (SUGECO) nk,

Lakini cha ajabu ni kwamba kila WUSC walipokuwa wanaomba vibali vya kazi kwa ajili ya wataalamu wao, Uhamiaji walikuwa wakiwakatalia na kuwakwamisha kwa sababu za kijinga kabisa. Ilifikia mahali uamuzi ukatolewa kwamba kwa sababu ya kukataliwa kupewa vibali basi ofisi ya WUSC nchini ifungwe.

Sasa siku ya kufunga rasmi ofisi ya WUSC, mgeni rasmi akawa Ofisa kutoka Wizara ya KIlimo. Hapo ndipo akawa anamwaga sifa kwa kazi iliyofanywa nchhini na WUSC na kuwaomba eti wasifunge ofisi na kuondoka!

Hivi Tanzania tuna watendaji wa namna gani lakinini? Kwa nini tunafanya mambo haya ya kijinga na kipumbavu kabisa - kama anavyosema Magufuli!

Hebu angalia ujumbe toka serikalini wakati WUSC wanafunga ofisi kwa kunyimwa work permits

View attachment 1390930View attachment 1390934

Ujumbe huu nataka uwafikie Raisi Magufuli na Waziri wa Mambo ya Ndani Simbachawene, kwamba kama kweli tunataka kuipeleka mbele Tanzania, tuache kabisa utendaji kama huu ambao ni mambo ya kijinga na kipumbavu ambayo hayawezi kufanywa na watu wenye akili timamu.

Source: IPPMedia
Govt simplifies issuance of work permits to attract more investments
Kuna mmoja alikuwa anafanya kazi shirika la afya Ireland! Aliomba managament ya shirika hili lisaidie kujenga hospitali kijijini kwetu na iwe full equips mpaka CT SCAN akakubaliwa! lakini alipoanza kutafuta kibali alijibiwa serikali imejitosheleza! Siku hizi hata kuja kutalii haji tena anaenda zake South tu!
 
Kufunga ofisi kwasababu ya kukosa work permit inamaanisha ni idadi kubwa ya wafanyakazi wamekosa permit kiasi cha kuathiri utendaji. Ina maana hizi NGOs zimejaa wageni kiasi hicho? Mbona kuna kampuni nyingi tu zina wafanyakazi wananyimwa permit na kampuni hazifungwi?
Hapana Mkuu. Kumbuka hii ofisi inahusiana na University hivyo wanaonyimwa permit ni wale wataalamu wanaokuja kwa ajili ya kufanya mafunzo. KUmbuka kwamba kwa utaratibu wa Tanzania, chukulia kama shirika la ndege KLM kwa mfano, ndege yao ikiharibika Tanzania pale JKNIA, ili mainjinia wao waje kutoka Netherlands kuitengeneza say kwa siku 7, wanahitaji work permit.

Kwa hiyo hata kama hawa wataalamu say magwiji wa University hii kutoka Canada wangekuwa wanakuja nchini kuendesha mafunzo bado watahitaji work permit. Hata mwandishi wa habari akija toka nje kufanya covering ya wiki moja serikali yetu inataka awe na work permit.

Sasa kuzipata hizo work permit, acha za muda mrefu, hata za muda mfupi tu ni issue kali Tanzania

Mkurugenzi aliwekwa Mtanzania kwa hiyo na yeye anapoteza kazi
 
Hii nchi ni ya vituko mno,permits zote zilitakiwa zitolewe na uhamiaji this buck stop on their door,ila wizara ya kazi inatoa mapendekezo yake kwa uhamiaji kuhusu umuhimu wa mtu anayeombewa permit,kwa nchi zinazojielewa wana kitu kinaitwa critical skills,sasa watu wenye nazo hizi ili kupata permit inabidi wapate motivation letter kutoka kwao,ila ni uamuzi wa immigrations wa kumpa au kukataa.tuendelee kusubiri noah zetu pale KIA.
 
Niliwahi kusema humu JF kwamba Tanzania ina mambo ya ajabu sana kuhusiana na utoaji wa work na residence permits hata kwa watu ambao ni wawekezaji, japo kila siku tunapiga kelele eti kuvutia wawekezaji.

Wawekezaji wanapokuja wanapata shida sana kupewa work au residence permits. Kuna wawekezaji Tanzania wamekaa zaidi ya miaka kumi nchini na wengine hata kuoa au kuolewa na Watanzania lakini bado wananyimwa permanent residence permits.

Kuna wageni toka nje wenye utaalamu wengi sana Tanzania ambao wameoa au kuoelwa na Watanzania na kuwa na familia, lakini hata hawa hawaruhusiwi kufanya kazi nchini kwa ajili ya kutunza familia zao, wananyimwa work permits japo ni wake au waume wa Watanzania na serikali inasema haiwatambui kama wakazi wa kudumu nchini!

Hivi kweli kweli kuna watu na akili zao serikalini na huko Uhamiaji na hawaoni kuna tatizo hapa?

Kichekesho cha mwaka ni hili la hii NGO ya WUSC kutoka Canada. Wao walikuwa na ofisi nchini kusaidia na kutoa mafunzo kwa watu na taasisi mbalimbali nchini na hata za serikali. Wamekuwa na mchango mkubwa sana taasisi kama Chamber of Commerce (Women), Umoja wa Wakulima wadogodogo nchini (MVIWATA), Umoja wa Wajasiliamali wa Wahitimu wa Chuo Cha Sokoine (SUGECO) nk,

Lakini cha ajabu ni kwamba kila WUSC walipokuwa wanaomba vibali vya kazi kwa ajili ya wataalamu wao, Uhamiaji walikuwa wakiwakatalia na kuwakwamisha kwa sababu za kijinga kabisa. Ilifikia mahali uamuzi ukatolewa kwamba kwa sababu ya kukataliwa kupewa vibali basi ofisi ya WUSC nchini ifungwe.

Sasa siku ya kufunga rasmi ofisi ya WUSC, mgeni rasmi akawa Ofisa kutoka Wizara ya KIlimo. Hapo ndipo akawa anamwaga sifa kwa kazi iliyofanywa nchhini na WUSC na kuwaomba eti wasifunge ofisi na kuondoka!

Hivi Tanzania tuna watendaji wa namna gani lakinini? Kwa nini tunafanya mambo haya ya kijinga na kipumbavu kabisa - kama anavyosema Magufuli!

Hebu angalia ujumbe toka serikalini wakati WUSC wanafunga ofisi kwa kunyimwa work permits

View attachment 1390930View attachment 1390934

Ujumbe huu nataka uwafikie Raisi Magufuli na Waziri wa Mambo ya Ndani Simbachawene, kwamba kama kweli tunataka kuipeleka mbele Tanzania, tuache kabisa utendaji kama huu ambao ni mambo ya kijinga na kipumbavu ambayo hayawezi kufanywa na watu wenye akili timamu.

Source: IPPMedia
Govt simplifies issuance of work permits to attract more investments
Nimekuelewa sana mkuu....
na inatia sana uchungu....
niliwahi lalamika pahala...
 
Work permit inatolewa na wizara ya kazi ukimaliza unaenda uhamiaji kupata resident permit ilitakiwa kuwe na dirisha moja la kushugulikia hayo Mambo vinginevyo usumbufu unabaki palepale
 
Hapana Mkuu. Kumbuka hii ofisi inahusiana na University hivyo wanaonyimwa permit ni wale wataalamu wanaokuja kwa ajili ya kufanya mafunzo. KUmbuka kwamba kwa utaratibu wa Tanzania, chukulia kama shirika la ndege KLM kwa mfano, ndege yao ikiharibika Tanzania pale JKNIA, ili mainjinia wao waje kutoka Netherlands kuitengeneza say kwa siku 7, wanahitaji work permit.

Kwa hiyo hata kama hawa wataalamu say magwiji wa University hii kutoka Canada wangekuwa wanakuja nchini kuendesha mafunzo bado watahitaji work permit. Hata mwandishi wa habari akija toka nje kufanya covering ya wiki moja serikali yetu inataka awe na work permit.

Sasa kuzipata hizo work permit, acha za muda mrefu, hata za muda mfupi tu ni issue kali Tanzania

Mkurugenzi aliwekwa Mtanzania kwa hiyo na yeye anapoteza kazi
 
Halafu pia na ikumbukwe kuwa Tanzania haitoi kitu kinaitwa permanent residence permit. Wanakataa katakata, si kwa wale waliooa au kuolewa Tanzania, hata wawekezaji walioajili Watanzania na ambao wamekuwa Tanzania kwa zaidi ya miaka mitano. Nchi nyingi duniani ukishakuwa na residence au work permit kwa zaidi ya miaka mitano ukiishi katika hiyo nchi, basi unakuwa ume-qualify kupata Permanent Residence Permit. Tanzania hakuna mtu anapewa permanent residence permit labda kwa maagizo ya Magufuli tu.
 
Work permit inatolewa na wizara ya kazi ukimaliza unaenda uhamiaji kupata resident permit ilitakiwa kuwe na dirisha moja la kushugulikia hayo Mambo vinginevyo usumbufu unabaki palepale
Okay sawa. Hata hivyo ujinga na upumbavu katika suala hili unabaki pale pale hata kama waliofanya hivyo ni Wizara ya Kazi
 
Kama unayemsaida hataki msaada wako si unaondoka tu. Tushakuwa matajiri, au hamsikii kila siku mkubwa akisema
 
Work permit inatolewa na wizara ya kazi ukimaliza unaenda uhamiaji kupata resident permit ilitakiwa kuwe na dirisha moja la kushugulikia hayo Mambo vinginevyo usumbufu unabaki palepale
Hebu ona hapa. Work permits za Tanzania zinaitwa Residence Permits Class A, B na C. Na zinatolewa na Uhamiaji. Hata ukinyimwa una appeal kwa Waziri Mambo ya Ndani, sio Wizara ya Kazi

1584446931708.png
 
Kama unayemsaida hataki msaada wako si unaondoka tu. Tushakuwa matajiri, au hamsikii kila siku mkubwa akisema
Mkuu huyo asiyetaka msaada ni Tanzania au watendaji wajinga na wapumbavu ndani ya Tanzania? Mie ni Mtanzania nahitaji huu msaada, sasa nani anasema sitaki msaada? Huyo aliyekaa ofisini ndio anahitaji huu msaada?
 
Mleta mada lazima utofautishe kati ya work permit na resident permit.

uhamiaji wanatoa resident permit na Wizara ya kazi kwa kupitia kamishna wa kazi ndio wanatoa work permit

ili kupata work permit ni lazima upate resident permit kwanza

hivyo uhamiaji hawahusiki na work permit.

Sent using Jamii Forums mobile app


Whatever lakini wamenyimwa

Wewe utuambie unajaribu kutetea nini?
 
Nasikia Rwanda watu kama hawa wanapewa kila kitu hadi ulinzi
 
WOte ni wapumbavu hao walikuwa wanatengeneza mazingira ya rushwa.

Hawana lolote walimuacha isabela ameenda ubelgiji amerudi na korona wapo wapo tu na inabidi hii korona iwakamte wampelekee hata bosi wao ili wakoma na watie akili
Corona ianzie kwao na familia zao mtu kaondoka sijui tar 5/3 -15/3 karudi wakati huko mambo si mambo ,chakushangaza waliwazui wanafunzi wasirudi vyuoni wala walioko huko wasirudi huyo sijui aliwapa nini!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu ulivyoiweka ni as if work permit ndio sababu pekee ya hawa kuondoka.
Hats km kungekuwa na sababu 1000, lkn work permit ikawa moja wapo ya sababu, lzm serikali ione kwamba ina mchango wake na imawajibika kujenga mazingira rafiki
 
Inawezekana Mkuu. KUmbuka unaweza kuwa na residence permit lakini usiruhusiwe kufanya kazi. Ila ukiwa na work permit basi hiyo ni residence permit pia.

Ukienda South Africa kwa mfano, unakuwa na residence permit ya kukaa siku 90. Lakini huna work permit huwezi kufanya kazi katika huo muda.

Ukipewa work permit ya mwaka mmoja, basi hiyo pia ni residence permit ya mwaka mmoja.
We jamaa ni zuzu
 
.
Mleta mada lazima utofautishe kati ya work permit na resident permit.

uhamiaji wanatoa resident permit na Wizara ya kazi kwa kupitia kamishna wa kazi ndio wanatoa work permit

ili kupata work permit ni lazima upate resident permit kwanza

hivyo uhamiaji hawahusiki na work permit.

Sent using Jamii Forums mobile app


Huu ndio kati ya urasimu ambao unadidimiza ukuaji wa kiuchumi nchi hii. Kwanini mtu anayetaka kufanya kazi nchi hii alazimike kutafuta permits mbili? Hivi mtu akipewa work permit halafu anyimwe residence permit itakuwaje? Maana huwezi kufanya kazi nchini bila kuwa resident.

Mimi nadhani kwa wafanyakazi wageni permit ingekuwa moja, yaani uhamiaji na wizara ya kazi wangeungana wakatoa permit moja ambayo utaratibu wa kuipata ungekuwa mmoja. Ili mtu akishaipata anaanza kazi moja kwa moja.

Residence permit za uhamiaji zibaki kuwa za waliooa/kuolewa na watanzania. Na mtu ambaye ni mke/mume wa mtanzania na wanaishi nchini automatically angeruhusiwa kufanya kazi na angepewa ukaazi wa kudumu (permanent residence) na baada ya miaka kadhaa angeruhusiwa kuomba uraia. Huu ndio utaratibu unaotumiwa na nchi nyingi tu duniani sijui kwanini sisi tunajiona wapekee sana
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pamoja na mapungufu huku immigration, nadhani kuna suala zito zaidi nyuma ya pazia. Awamu hii haina mwamko na NGO kwa vile wanataka kudhibiti kila kitu. NGO wanakuwa huru na miradi na fedha zao ambazo hazipiti jungu kuu na hivyo kujikuta wanakuwa frustrated na system.
 
Back
Top Bottom