Tanzania ina tatizo gani mpaka viongozi washindwe kuwajibika ipasavyo?

Tanzania ina tatizo gani mpaka viongozi washindwe kuwajibika ipasavyo?

leoleo-tu

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2018
Posts
2,224
Reaction score
6,784
Wakati mwingine ukifikiria maamuzi ya watendaji wa nchi hii yatakushangaza.

Kwa mfano: Bunju mwisho stand ya mabasi, walikuja wakasema mabasi yatoke yawe yanapaki barabarani watengeneze barabara na stand. Imepita zaidi ya miezi mitatu hakuna matengenezo ya stand wala nini na magari yanaendelea kupaki barabra ya Bagamoyo na kusababisha foleni.

Sasa kama walijua hawakuwa tayari, kwanini waliondoa mabasi hayo.

Na wafanyabiashara waliokuwa wamechukua mabanda pale stand kwa sababu hakuna biashara abiria hawaingii stand nao wamehamia barabarani.

Hii inanikumbusha walipobomoa stand ya Ubungo wakati ya Magufuli ilikuwa haijawa tayari na kusababisha abiria kupata shida sana.

Mfano 2: Siku moja Rais alikuwa anaenda Wazo kwa Makamba Sr. Siku 3 kabla wakapitisha gereda kurekebisha barabara ya mtaa maana ilikuwa ni mbovu sana. Wakaondoa vibanda vilivyo karibu na barabara. Bodaboda wakaambiwa kituo wakiondoe wakae mbali kabisa na barabara.

Rais akaja hata nusu saa hakukaa akaondoka maisha yakarudi kama kawaida. Sasa mimi kilichonishangaza haya ya kuondoa mabanda na boda wakae mbali walitaka Rais asione maisha halisi ya raia wake? Ina maana rais hajui uhalisia wa maisha ya raia wake na anapaswa asijue?

Kuna vitu vinafikirisha kweli
 
Hii nchi ni Maalum. Raisi wake ni Maalum. Raia wake ni Maalum. Wafanya kazi wake ni Maalum.Rangi zao ni Maalum. Lugha yao ni Maalum.Mavazi yao ni Maalum. Barabara zao ni Maalum. Gari zao ni Maalum. Wanaume wao ni Maalum. Wanawake wao ni Maalum.Watoto wao ni Maalum.Kila kitu chao ni Maalum.
 
Wakati mwingine ukifikiria maamuzi ya watendaji wa nchi hii yatakushangaza.
Kwa mfano: Bunju mwisho stand ya mabasi, walikuja wakasema mabasi yatoke yawe yanapaki barabarani watengeneze barabara na stand. Imepita zaidi ya miezi mitatu hakuna matengenezo ya stand wala nini na magari yanaendelea kupaki barabra ya bagamoyo na kusababisha foleni.
Sasa kama walijua hawakuwa tayari, kwanini waliondoa mabasi hayo.
Na wafanyabiashara waliokuwa wamechukua mabanda pale stand kwa sababu hakuna biashara abiria hawaingii stand nao wamehamia barabarani.
Hii inanikumbusha walipobomoa stand ya ubungo wakati ya Magufuli ilikuwa haijawa tayari na kusababisha abiria kupata shida sana.
Mfano 2: siku moja rais alikuwa anaenda wazo kwa Makamba Sr. Siku 3 kabla wakapitisha gereda kurekebisha barabara ya mtaa maana ilikuwa ni mbovu sana. Wakaondoa vibanda vilivyo karibu na barabara. Bodaboda wakaambiwa kituo wakiondoa wakae mbali kabisa na barabara.
Rais akaja hata nusu saa hakukaa akaondoka maisha yakarudi kama kawaida. Sasa mimi kilichonishangaza haya ya kuondoa mabanda na boda wakae mbali walitaka rais asione maisha halisi ya raia wake? Ina maana rais hajui uhalisia wa maisha ya raia wake na anapaswa asijue?
Kuna vitu vinafikirisha kweli
Wanataka kusema Raisi anajua watu wake wote wanaishi vzr, mbna uongo mwingine wa kijinga kabisa.
 
Back
Top Bottom