Tanzania inayonifanya niwaombe msamaha wana JF

Tanzania inayonifanya niwaombe msamaha wana JF

Mwaka 2006 nilitembelea BONGO wakati mambo ikiwa mbaya sana kwa wananchi kwa ajili ya UKAME NA UMEME ULIOSHINIKIZWA NA UJAMBAZI WA RICHOMD.
Nilipokuwa kwenye mizunguko yangu kwenye jiji la Dar kuonana na watu wangu nilimpa ride tu maeneo flani na pembeni kulikuwa na saloon a kina dada ambao walikuw wamekaa nje kwasababu hakuna biashara na hata air condition haifanyi kazi na kafeni kenyewe kaliko ndani kanapuliza joto badala ya hewa nzuri.
Ghafla akatokezea CHINGA MMOJA ambaye alikuwa amepigika kinoma huku malapa aliyovaa yakiwa hovyo hovyo huku kisigina kikiwa kinakanyaga chini!
Hutu chinga likuwa akiuza vyupi na sidiria akiwa amekamata mkononi huku akimlilia dada mwenye saloon anunue walau sidiria moja ili aweze kwenda kula!
Mjadala uliendelea huku chinga akiongea hadi mapovu meupe yakimtoka pembezoni mwa mdomo na huku akionekana kuwa maisha ni magumu na hata hali yake kiafya ni mbovu kutokana na mlo wa kubabiababia!

Mimi kuwa kwamngu pembeni kulinipa shida kwani nilkuwa sijui nimtetee yupi!
Chinga anasema hajala na anategemea kina dada wananunue sidiria ili walau akale...
Mwanadada wa saluni naye akawa nadai hata yeye anafunga muda si mrefu ili akajaribu kuangalia kama nyumbani kuna chakula kwani hajafanya biashata kwa karibu wiki kwasababu ya umeme.
Mabishano yalikuwa makali...Lakini wote waalikuwa hawana makosa...UCHUMI WETU ULIKUWA UMELALA EXCEPT KWA MAFISADI MAFIOSO ambao wao mambo ni mswano tu na migenerator huku wakiendelea kulipwa pesa za wananchi kwasababu tu RICHMOND ilishindwa ku provide umeme wa dharura kwa wananchi na hivyo mabilioni yao ya kodi kupewa kina ROSTAM,MKAPA,KIKWETE,LOWASSA,MRAMBA,MGONJA NA MAFIOSO WENGINE WA CCM!
Dada wa Saluni naye alikuwa akihitaji sidiria lakini hana pesa...Chinga akaomba walau mia saba ili akale...Dada akawa still hana...Na chinga kaanza kuchukia akidhani kuwa Dasa ni tajiri mwenye roho mbaya!
Nikatoa elfu nikampa nikamwambia ampe Dada hiyo sidiria...
Nikachoma gari moto huku machozi akinitoka!
EMPATHY TUME LACK...Afadhali sasa wengine nao wamegundua na kulia baada ya Kelly.

.....short & powerfull story how society inavyosuffer kutokana na ulafi wa mafisadi,mzee umegusa point zote jinsi rushwa ilivyoua biashara ya huyo dada na kuondoa purchasing power yake na kusababisha machinga alale njaa indirect kutokana na rushwa za kina lowassa na wenzake...na huo ni mfano mmoja tuu,millions wako affected na hizi tabia za mafisadi,nina uhakika kuna waliouwawa kwa kufanya ukibaka ili wale kutokana na njaa.
 
Hey guys, this is interesting stuff! Can someone assist me. I wanna down load the videos and save them in my computer. Its good for show casing. Mama Mwaituka who is mentioned in this video is she the same Madam who has been living with HIV/AIDS for almost twenty years? She is doing great job in helping other young girls to get out of this plight

PM


Kuna websites kadhaa zinafanana hivi kwenye google, zitumie hizo ku-download clips from youtube.
You simply need to enter the youtube link.


.
 
Masaka(Uganda) mara ya kwanza ulipokuwa ukitetea ufisadi nilidhani wewe si Mtanzania hata baada ya kuangalia jina lako "masaka".....kuna mambo ambayo ukiyajua yatakusumbua kichwa
CCM kama chama sio kibaya na hakina sera mbaya ila utekelezaji wa sera zake ndio hao mafisadi wanazipindisha........sasa kaa kwanza kundini(CCM) waelimishe wenzako nao wajue hili alafu uje utuambie wanaichukulia vipi hali hii
 
Mkuu Masaka,

Mimi tangu mwanzo nilifahamu kwamba "you had lost the plot".

Ni kitendo cha kuonesha kukomaa kimawazo ambacho kimekufanya urudi nyuma na kampeni zako za "spining".

Haya onesha kweli kwamba umebadili mtazamo wako wa kifikra na usiwe tena "spinner".
 
Pamoja na masikitiko mengi yanayowakuta watanzania hila leo nimefurahi kuona hata MASAKA, HOLLO, nawengineo wameweza kuona matatizo yanayowakumba watanzania.

Mimi binafsi Ninawakaribisha kundini bila kujali vyama vyao vya siasa hila tukikumbuka wito uliotolewa na wapinzania wakati wakiwakilisha bajeti yao bungeni ni kwamba yote yanayoonekana mazuri na mabaya ni matunda ya chama cha mapinduzi.
 
.....short & powerfull story how society inavyosuffer kutokana na ulafi wa mafisadi,mzee umegusa point zote jinsi rushwa ilivyoua biashara ya huyo dada na kuondoa purchasing power yake na kusababisha machinga alale njaa indirect kutokana na rushwa za kina lowassa na wenzake...na huo ni mfano mmoja tuu,millions wako affected na hizi tabia za mafisadi,nina uhakika kuna waliouwawa kwa kufanya ukibaka ili wale kutokana na njaa.

Tatizo ni kwamba pale kama nisingetoa elfu...Then CHINGA angedhani mwanadada wa watu ana roho mbaya na ameshindwa kumuonea huruma kwa kununua sidiria yake kwa nusu ya bei aliyokuwa akihitaji mwanzo ili akajipendelee mchana mwema kwa mama ntilie!

Na Dada naye kama inavyojulikana ni victim together na CHINGA...
Sasa tatizo nihapo...Je hao wananchi wanajua haki zao?

Je yule CHINGA alijua kuwa kosa si la DADA? Bali mafioso Mafisadi?
Je dada naye anajua kuwa ameshaliwa na bado anaendelea kuliwa huku akielekea kaburini kwa ukosefu wa damu?
 
Nangoja mabadiliko katika avator ya Masaka na kauli mbiu ya CCM aiche then aje kwenye Vodacom anipe support ikiwa ni pamoja na yeye kutupa kadi yake ya Vodacom kwa kuanzia tu .
 
Waungwana,

Mwacheni kumkejeli huyu Masaka, labda analosema ni kweli kwamba alikuwa hajui hayo aliyoyaona pamoja na kuwa anaishi Dar. Huyu alikuwa ni mtetezi mkubwa wa CCM hapa JF, sasa nguvu za hija zetu na aliyoyaona kwa macho yake yamemwingiza kwenye kambi yetu na pia ameonyesha uungwana kwa kuomba msamaha. hivyo sidhani kama kuna haja ya kuendelea kumkejeli.
 
mmoja kati yao aliwafundisha kufanya usafi na kuwaonyesha namna ya kupata mwanga na baadaye wakaambukiza dunia nzima kuanzia kwa mafarao wa misri hadi kwa mayahudi wa silicon valley...

Sasa kwa nini sisi hadi twende ulaya ama Marekani kujifunza usafi?
 
Sasa kwa nini sisi hadi twende ulaya ama Marekani kujifunza usafi?

..sema wewe peke yako ndio juma mchafu sio kila mtu anajifunzia usafi ulaya,sijui lini utaacha ujuha? tumechoka tumechoka na upupu wako wa kila siku...jirekebishe sasa!
 
karibu Masaka .Dini yetu haifungamani na yeyote .Dini yetu inaitwa Tanzania kwanza .
 
..sema wewe peke yako ndio juma mchafu sio kila mtu anajifunzia usafi ulaya,sijui lini utaacha ujuha? tumechoka tumechoka na upupu wako wa kila siku...jirekebishe sasa!

hahaaaa ! natoka zangu mie ! hahaaaaaaaaa..lol
 
Masaka usishangae mzee ndo wanja la fisi hilo, watu wanajimwaga pale kama hakuna kesho ! na kuna wengine NASIKIA wamewekeza pale usishangae tena wengine viongozi!
 
..sema wewe peke yako ndio juma mchafu sio kila mtu anajifunzia usafi ulaya,sijui lini utaacha ujuha? tumechoka tumechoka na upupu wako wa kila siku...jirekebishe sasa!

Wewe Koba ni mchafu na unanuka mdomo....watu wamechoka na harufu mbaya ya mdomo wako. Nenda kwa mganga wa meno unaweza ukasaidiwa.
 
Masaka usishangae mzee ndo wanja la fisi hilo, watu wanajimwaga pale kama hakuna kesho ! na kuna wengine NASIKIA wamewekeza pale usishangae tena wengine viongozi!

No no no no no no....

KadaMpinzani, tunataka usema kitu serious hapa, tujue kama unaona mwenzio kakosea au huwa mnaleta mawazo msiyomaanisha kutoka moyoni.

Una nini cha kusema kuhusu mwezio alivyo pata "maono ya Sauli" na kugeuka njia? Halafu baadae ndio tutaendelea na utani.
 
Wewe Koba ni mchafu na unanuka mdomo....watu wamechoka na harufu mbaya ya mdomo wako. Nenda kwa mganga wa meno unaweza ukasaidiwa.

...you belong uwanja wa fisi na sijui ulifikaje huko Alaska unakofanya kazi ya kuvua samaki.
 
No no no no no no....

KadaMpinzani, tunataka usema kitu serious hapa, tujue kama unaona mwenzio kakosea au huwa mnaleta mawazo msiyomaanisha kutoka moyoni.

Una nini cha kusema kuhusu mwezio alivyo pata "maono ya Sauli" na kugeuka njia? Halafu baadae ndio tutaendelea na utani.

On a serious note,
ni kwamba Masaka ni mwanaccm ! au kabadirika nini ? uanachama ? kwani nani aliyesema wanaccm hawana huruma ? yeye kaona huruma kama binadamu na sio kama mwanaccm au mwanampinzani !

Haya endeleeni na mjadala, mie navuta pumzi !
 
Wewe Koba ni mchafu na unanuka mdomo....watu wamechoka na harufu mbaya ya mdomo wako. Nenda kwa mganga wa meno unaweza ukasaidiwa.

...you belong uwanja wa fisi na sijui ulifikaje huko Alaska unakofanya kazi ya kuvua samaki.

heheee ! wazee hapa nafikiri itakuwa vizuri tukiongelea hii topic ya uwanja wa fisi maana kwa mtazamo wangu binafsi pia naona yanayotokea uwanja wa fisi hayana tofauti na yale yanayotokea club billicanas isipokuwa tu billicanas hamna matope kama wanja la fisi ! SIJUI NYINYI MNAONAJE !
 
heheee ! wazee hapa nafikiri itakuwa vizuri tukiongelea hii topic ya uwanja wa fisi maana kwa mtazamo wangu binafsi pia naona yanayotokea uwanja wa fisi hayana tofauti na yale yanayotokea club billicanas isipokuwa tu billicanas hamna matope kama wanja la fisi ! SIJUI NYINYI MNAONAJE !

Kuna wakati inabidi ubaradhuli wako uuweke pembeni. Watu wanataka kujadili mambo ya maana kuhusu hatima ya nchi yetu lakini wewe unaleta mambo yasiyo na kichwa wala miguu!! Mtu mzima hovyoooo! Kuna forum ya jokes nenda huko wala hakuana atakayekusumbua haya ukiandika upupu wa namna gani.
 
Back
Top Bottom