Tanzania isiwe na vazi moja tu la Taifa, tuwe na mavazi rasmi matano kutoka katika makabila yetu

Tanzania isiwe na vazi moja tu la Taifa, tuwe na mavazi rasmi matano kutoka katika makabila yetu

Kwanini tusitengeneze vitambaa vya hilo vazi wenyewe, China ni Neo New Economical Colonial Master
Mimi nakumbuka mama alikuwa anapika vitenge mwenyewe
Wakati huo kila mwananchi alikuwa na ile ari ya kujitegemea
Na SIDO ilijaribu lakini wezi wakaja kula kila kitu
Hata Shillingi ilikuwa inajibeba kwenye currency market

Mkuu achana hizi stori za mafuta ya mpako
Hamasisha micro development tusiwe nchi ya wachuuzi
Una mawazo hasi sana kijana wangu
 
Swali la kitoto sana hili
Wewe chiku mbona unakua mnaa? Wewe unadhani miaka yooote hii tangia tumepata uhuru hatukuliona hilo swala la vazi la taifa??

Kuungunisha makabila 130+ kuwa taifa moja sio jambo dogo, kunahitaji upeo wa kipekee na kutoa sadaka baadhi ya vitu vya kipuuzi vinavyochochea ukabila kama vile mavazi ya kikabila kuwa 'vazi la taifa'.

Hakuna vazi la taifa, hautaki unaacha.
 
Pwani jee?mbeya jee?mara na bukoba na mwanza jee vipi kwa upande wa nchi ya Zanzibar?
Mambo vp jamiiforums.

Ninashauri sana nchi yetu ya Tanzania isiwe na vazi moja tu la taifa. Tuwe na mavazi rasmi matano (5) kutoka katika makabila yetu yatakayorasimishwa na kupewa hadhi ya utaifa. Yaaani kama inawezekana mpangilio uwe hivi au hata kama kura ya maoni inaweza kupigwa itakuwa sawa tu.

Picha hapo chini ni Rais Mstaafu wa awamu ya nne mzee Kikwete na mkewe Mama Salma wakiwa wamependeza vizuri kabisa katika mavazi ya kabila ya Waha (baba) pamoja na Maasai (Mama)
=====
View attachment 1718602

(1) Kaskazini - Vazi la kimaasai (Mkoa Arusha)

(2) Kusini - Vazi la Kimakonde (Mkoa Mtwara)

(3) Mashariki - Vazi la Kisambaa (Mkoa Tanga)

(4) Magharibi - Vazi la Waha (Mkoa Kigoma)

(5) Kanda ya kati - Vazi la wagogo (Mkoa Dodoma)

Nchini Afrika ya kusini wamefanya hili kwa upande wa lugha rasmi za taifa, ila sisi tunaweza kufanya hivi hivi kwa upande wa vazi rasmi la taifa.

Kwa uhalisia tu ni kwamba, huko nchini Afrika ya Kusini kuna makabila mengi sana yaliyopo katika majimbo tofauti tofauti na matokeo yake lugha zinatawala katika majimbo yao husika ambayo inafanya kuwa lugha mahususi haswa kwa eneo/mkoa husika.

Takribani lugha thelathini na tano (35) zenye asili ya Afrika Kusini huzungumzwa katika nchi hiyo, kumi kati ya hizo ni lugha rasmi za taifa la Afrika Kusini: Ndebele, Pedi, Sotho, Swati, Tsonga, Tswana, Venda, Xhosa, Zulu na Afrikaans.

Lugha rasmi ya kumi na moja ni Kiingereza, ambayo ndiyo lugha ya msingi inayotumiwa katika mazungumzo ya kibunge na kiserikali, ingawa lugha zote rasmi zina uzito sawa katika hadhi ya kisheria na katika ya nchi hiyo.

Kama katika lugha 35 kutoka nchi nzima waliweza kuchagua lugha 11 tu kutambulika kama "official languages" na Tanzania yenye makabila takribani 120 pia inaweza kuchagua mavazi kutoka makabila 5 tu kuwa ndio mavazi rasmi ya taifa ili tumalizane na hili suala kwa maana tangia lianze kujadiliwa ni zaidi ya miaka 15 sasa na bado sijaona solution ya maana mpaka sasa.

Soma pia>>> Kwanini mitaa ambamo kuna Balozi za nchi tano zenye nguvu duniani isiitwe majina ya vivutio vya utalii vya Tanzania?

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
 
Wewe chiku mbona unakua mnaa? Wewe unadhani miaka yooote hii tangia tumepata uhuru hatukuliona hilo swala la vazi la taifa??

Kuungunisha makabila 130+ kuwa taifa moja sio jambo dogo, kunahitaji upeo wa kipekee na kutoa sadaka baadhi ya vitu vya kipuuzi vinavyochochea ukabila kama vile mavazi ya kikabila kuwa 'vazi la taifa'.

Hakuna vazi la taifa, hautaki unaacha.
Mnaa maana yake nini?
 
Mambo vp jamiiforums.

Ninashauri sana nchi yetu ya Tanzania isiwe na vazi moja tu la taifa. Tuwe na mavazi rasmi matano (5) kutoka katika makabila yetu yatakayorasimishwa na kupewa hadhi ya utaifa. Yaaani kama inawezekana mpangilio uwe hivi au hata kama kura ya maoni inaweza kupigwa itakuwa sawa tu.

Picha hapo chini ni Rais Mstaafu wa awamu ya nne mzee Kikwete na mkewe Mama Salma wakiwa wamependeza vizuri kabisa katika mavazi ya kabila ya Waha (baba) pamoja na Maasai (Mama)
=====
View attachment 1718602

(1) Kaskazini - Vazi la kimaasai (Mkoa Arusha)

(2) Kusini - Vazi la Kimakonde (Mkoa Mtwara)

(3) Mashariki - Vazi la Kisambaa (Mkoa Tanga)

(4) Magharibi - Vazi la Waha (Mkoa Kigoma)

(5) Kanda ya kati - Vazi la wagogo (Mkoa Dodoma)

Nchini Afrika ya kusini wamefanya hili kwa upande wa lugha rasmi za taifa, ila sisi tunaweza kufanya hivi hivi kwa upande wa vazi rasmi la taifa.

Kwa uhalisia tu ni kwamba, huko nchini Afrika ya Kusini kuna makabila mengi sana yaliyopo katika majimbo tofauti tofauti na matokeo yake lugha zinatawala katika majimbo yao husika ambayo inafanya kuwa lugha mahususi haswa kwa eneo/mkoa husika.

Takribani lugha thelathini na tano (35) zenye asili ya Afrika Kusini huzungumzwa katika nchi hiyo, kumi kati ya hizo ni lugha rasmi za taifa la Afrika Kusini: Ndebele, Pedi, Sotho, Swati, Tsonga, Tswana, Venda, Xhosa, Zulu na Afrikaans.

Lugha rasmi ya kumi na moja ni Kiingereza, ambayo ndiyo lugha ya msingi inayotumiwa katika mazungumzo ya kibunge na kiserikali, ingawa lugha zote rasmi zina uzito sawa katika hadhi ya kisheria na katika ya nchi hiyo.

Kama katika lugha 35 kutoka nchi nzima waliweza kuchagua lugha 11 tu kutambulika kama "official languages" na Tanzania yenye makabila takribani 120 pia inaweza kuchagua mavazi kutoka makabila 5 tu kuwa ndio mavazi rasmi ya taifa ili tumalizane na hili suala kwa maana tangia lianze kujadiliwa ni zaidi ya miaka 15 sasa na bado sijaona solution ya maana mpaka sasa.

Soma pia>>> Kwanini mitaa ambamo kuna Balozi za nchi tano zenye nguvu duniani isiitwe majina ya vivutio vya utalii vya Tanzania?

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
DRC wamerahisisha san. Wao wanakitambaa ( Kitenge) chenye utambulisho wa DRC, kuna rangi za bendera blue ikiwa imekolea zsidi na viashiria vingine kihusu taifa hilo.

Hicho kitambaa sababu kimetengenezwa maalum hukiti kama hicho na viashiria vyake huko china au nchi nyingine.

Walichoruhusu wao ni kila mtu kushona dizain anayoona inampendeza iwe shati , suruali, kilemba,koti, n.k.

Ni rahisi wao kutambuana hata akivaa juu shati la kitambaa kile na chini jeans .
 
Kuungunisha makabila 130+ kuwa taifa moja sio jambo dogo, kunahitaji upeo wa kipekee na kutoa sadaka baadhi ya vitu vya kipuuzi vinavyochochea ukabila kama vile mavazi ya kikabila kuwa 'vazi la taifa'.
Mbona Dodoma ndio mmepafanya kuwa makao makuu ya taifa? Kwani hilo haliwezi kuchochea ukabila? Makao makuu ya Serikali ilikuwa Dar (Kwa Wazaramo) sasa mmeamua kuihamishia Dodoma (Kwa Wagogo), unafikiri wazaramo wanajisikiaje kama issue ni ukabila?
 
Vazi la kimasai tayari ni vasi lililopasishwa na jamii kuwa vazi la kitaifa sijui serikali inasubiri nini kulipitisha kuwa la kitaifa, likifuatiwa na kanga na kitenge, japo ni mavazi ya Afrika nzima.
Msuko wa nywele ya masai nao unapendwa Tanzania nzima na dunia.
Waafrika huwa hatuchukui maamuzi ya haraka sijui kwa nini?
 
Mbona na wewe ideas zako ni kama za hao wahenga tu
Usipende kuwaza katika hali hasi bali chanya.Mbona kiswahili wabantu wa qaote wamekipokea kuwa lugha yetu rasm! Kumbuka wabantu babu yetu ni mmoja makabila ni koo mbalimbali za mbantu.
Umezikubali suti,kanzu ila hutaki vazi la ndugu yako bali la mwarabu na mzungu.
 
Back
Top Bottom