Tanzania ivunje uhusiano na Israel?

Tanzania ivunje uhusiano na Israel?

"Mess with the bull and you get the horns"
Having said that, Hamas is learning it the hard way you cant fire rockets into another country and when they react preemptively you start whining.
As far as out diplomatic ties with Israel are concerned, do you really think they will actually be moved by our diplomatic withdrawal?
 
After the six months of Truce Agreement between the government of Israel and Palestine ended, Hamas sent message to the goverment of Israel by Rocket propelled grenades. Remember Israel always kept away its stance with Palestine. But Hamas through manipulative language to its citizens and some quotations from the Holy QURAN poisoned some of its youth and made them live with the same belief that there is no peace until Israel withdraw from their territoty something of which is impossible. So with all due respect sir. MMKJJ I know you know history better than me because you are older than me for that matter but this conflict of decades and decades is being propagated with religeous beliefs. In Tanzania Nyerere decided to break diplomatic reletions with Israel not only through its policy of Socialism and self reliance but also security reasons. The issue of Israel aggression to Palestine became a camourflage. The issue of security was the main essence that led to the breaking of diplomatic relations between the two countries.
 
Nashangaa waislamu wanavyoandamana Dar kwa vifo vya wapalestina wakati waislamu weusi wa Darfur wanauwawa kwa wingi huko Sudani ya kusini.Nawataka waache double stardard

Waarabu ni watu wa ajabu hawako pamoja na bara la Africa kwenye shida zao.Wakati Afrika ilikuwa ikiwashambulia makaburu wa Afrika ya kusini waarabu walikuwa wakiendelea kuwauzia mafuta bila kuungana na Africa lakini wakati huo huo walikuwa wakitaka Afrika iwaunge mkono waarabu wa Palestina dhidi ya Israeli.

Waislamu wa Somalia ambayo iko Afrika wanauawa kila siku lakini husikii cha maandamano wala nini nchi za kiarbu kupinga uharamia unaofanyiwa raia wa Somalia wasiokuwa na hatia wala huoni Televisioni ya Waarabu ya Aljazeera (ARJAZEERA TV) ukipenda waweza iita HAMAS TV ikitangaza habari za raia wanaouliwa Somalia na kuitisha jumuiya ya kimataifa au ya kiislamu iwasaidie wasomali wa Afrika wasio na hatia wanaouawa kila siku.Habari za mauaji zinazotangazwa na HAMAS TV (ALJAZEERA TV) ni zile za wapalestina wakati kuna waislamu wasomali wenye hali mbaya kuliko wapalestina kutokana na vita.

Pia Upande wa Sudan serikali ya mwarabu Omar al Bashir na maraisi waarabu waliomtangulia walikuwa wakiwaua wakristo weusi wasiokuwa waarabu wa Sudani ya kusini hakukuwa na maandamano yoyote ya nchi za kiarabu kulaani,kuandamana n.k kuwatetea wakristo hao weusi wa Sudan waliokuwa wakivurumishiwa makombora na serikali ya mwarabu wa Kartoum sudan.

Watu tukadhani kuwa Serikali ya mwarabu wa Sudan ilikuwa ikiwaonea waafrika weusi wa Sudan ya kusini sababu ni wakristo jumuiya ya kimataifa ikapiga kelele hadi tatizo likafikia mahali pa kupungua wakapata serikali yao.Ilipoona imeshindwa kuendelea kunyanyasa waafrika weusi wa Sudan Kusini Serikali ya Mwarabu wa Sudani ikawageukia waislamu weusi wa Darfur na kuanza kuwanyanyasa na kuwaponda kwa makombora na maroketi.Wakati hilo likiendelea hatukuona nchi yoyote ya Kiarabu wakiandamana kupinga uvamizi na mashambulizi ya makombora Mwarabu Omar al Bashir Raisi wa Sudan kwa wananchi waislamu weusi wa Darfur.Tunashukuru mahakama ya kimataifa kutoa hati ya kukamatwa kwa mwarabu Omar AL basher angalau nchi za magharibi zisizo za kiislamu zimeamua kutetea waafrika weusi waislamu wa Darfur wakati waislamu wa Uarabuni wamekaa kimya wakila tambuu na kashata kama vile wanaokufa Darfur ni ngedere wa porini.

Ninachokiona ni kuwa waarabu hawako pamoja na waafrika weusi katika taabu zao lakini wao wanataka waafrika weusi wawe nao katika taabu zao.Wepesi kuhamasisha misikitini watu walaani mashambulizi ya waarabu Palestina lakini si wepesi kuhamasisha watu misikitini waandamane walaani ya Somalia au Darfur.Hata TV yao ya HAMAS TV (aljazeera TV) inakesha usiku na mchana kwa siku nyingi mfulilizo inatangaza mauaji Palestina lakini haijawahi tumia hata siku moja mfululizo kutangaza vita na mauaji yanayoendelea Somalia,Sudan ,Kusini ,Wala Darfur.

Binafsi sioni sababu ya kuvunja uhusiano wa Kibalozi na Israeli sababu waarabu nao hawakuvunja uhusiano na serikali oneaji ya Sudan inayoonea waafrika weusi ila napendekeza uhusiano wa kibalozi na waarabu wa Palestina ndio tuvunje maana wapalestina hatujawahi ona wakiandamana kupinga mauaji ya Somalia,Sudan kusini wala Darfur wala kuvunja uhusiano na adui huyo wa waafrika weusi.
Sioni sababu ya kuendelea na uhusiano na watu ambao hawako na wewe kwenye misiba yako lakini wanataka wewe ulie machozi hadi ujinyee kwenye misiba yao.Shenzi type. Wapalestina hawatusaidii kwenye migogoro ya Sudan Kusini wala ya waislamu wa Darfur na Somalia.Hao watoto na wanawake wanaoonyeshwa Palestina wanaathirika kwenye TV na hiyo vita na Israeli wana nafuu ukilinganisha na wanawake na watoto wa Somalia,Sudan kusini,na Darfur ambao hawana TV kama ya HAMAS TV (Aljazeera TV) ya ku-market taabu zao kwenye soko la wasaidaji wa kimataifa au waona huruma wa kimataifa.

Msimamo wa Tanzania ungekuwa kukaa kimya kama Wapalestina wanavyokaa kimya kwenye migogoro ya Somalia,Sudan Kusini na Darfur.Wa Tanzania tuanze kuwa na misimamo kwenye medani za kimataifa siasa za kujikomba komba hazina nafasi kwenye utandawazi.Utanawazi unahitaji watu wababe wanaojua haki zao na nchi zao na wawezao kuzisimamia bila woga wala kumeza maneno iwe kwenye vikao vya kimataifa,siasa,biashara au uchumi wa nchi.
 
Nashangaa waislamu wanavyoandamana Dar kwa vifo vya wapalestina wakati waislamu weusi wa Darfur wanauwawa kwa wingi huko Sudani ya kusini.Nawataka waache double stardard

Vyombo vya habari,Jumuia za kimataifa na sisi wenyewe tumewaangazia zaidi weupe kuliko bara letu wenyewe, kuliko sisi wenyewe. Zaidi ya yote kwa kuwaunga mkono weusi wa Darfur hujengi umaarufu kama ambavyo ingekuwa kwa Mashariki ya Kati.

Wapo watu hama wamesahau, au hawajui kabisa kuwa maelfu ya waafrika wanateswa na waafrika wenzao huko Darfur na DRC. Kwao si tatizo, tatizo ni wanapoguswa weupe (Wazungu kwa waarabu), Na waafrika wanashabikia kila mtu na upande wake!


Ndivyo Tulivyo.
 
Zakumi,
Hao wabaki huko huko. Tumeshindwa kuwapa Wanyarwanda na Warundi ardhi leo tuwakaribishe Wayahudi na Wapalestina? Wabaki huko huko!

Jasusi

Nijuavyo mimi Rukwa,Kigoma,Tabora, Kagera,SHY na Mwanza kuna Idadi kubwa ya Warundi na Wanyarwanda, Wanyarwanda ni wengi zaidi. Wapewe ardhi na kukaribishwa vipi zaidi ya walivyo sasa? Labda kama kuna tatizo jingine.
 
Huko nyuma tuliwahi kusema kuwa "kila mtu anastahili haki ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake". Pia tulisema kwamba kila watu wana haki ya kuwa na mahali ambapo watakuwa salama kutoka vitisho vyovyote vya utu wao na nafasi yao kama jamaa.

Kwa sababu hiyo tuliunga mkono POLISARIO na PLO, kama vile tulivyounga mkono Biafra, kuunga mkono ANC, FRELIMO n.k Tuliamini ya kwamba hakuna mwanadamu mwingine ambaye ana haki ya kumtawala kwa nguvu mwanadamu mwingine kwa kisingizio chochote kile. Hii ilikuwa ni falsafa yetu dhidi ya ukoloni.

Leo hii tunashuhudia yanayoendelea Palestina ambapo karibu maelfu ya watu wameshauawa. Je, Bunge linapokutana siku chache zijazo zilaani mauaji hayo? Je serikali ilaani pande zote mbili kwa kusababisha mazingira ambayo yanamnyima mwanadamu nafasi ya kuwa huru kufanya lolote? Je tuungane na nchi kama Venezuela na Bolivia ambazo zimevunja uhusiano na Israel kutokana na suala la Gaza?

Je tukifanya hivyo hatutaulizwa uhusiano wetu na nchi kama Sudan, Somalia, Iran, n.k ambapo rekodi zao kuhusu haki za binadamu na raia si za kupewa sifa?

Au tuendelee kukaa pembeni tu na kuwaacha "wafu wawazike wafu wao"?

Ndugu yangu MKKJ,

Naona Mzee unaanza kutonesha kidonda hapa. Kwa taarifa nchi hii ndiyo maana hamna linalofanikiwa kwa sababu ya Ujinga wa Nyerere wa kuvunja uhusiano na Israel. hebu nitajie taifa lolote duniani ambalo halina uhusiano na ISRAEL na mambo yao yanakwenda vizuri ( amani, uhuru wa kweli, utajiri na ustaarabu) hakuna! tujifunze kitu.

kanuni za Mungu iko pale pale. Hii nchi kama nchi haina direct ralation na Mungu kwa sababu ya kuvunja principle yake tupo hapa leo hivi ni kwa sababu tu ya sisi tunaopiga magoti kumsihi Mungu kila leo (wakina Rutu) na huu uhusiano wa watu binasfi na ndiyo unaotulinda kidogo. Angalia Jirani zetu kama Kenya very clever!!!
 
Nimesoma kwa makini matamshi haya:

...hao Hamas wangekuwa na uwezo dunia nzima tungelazimishwa kuvaa kanzu na kibaraghashia,acha wachapwe tuu maana nao nia yao ni kuwamaliza na kuwafuta Israelites ila hawana uwezo tuu,wako pale kwa agenda za extremist kama Osama na Irans hardliners,hata 2 state solution hawataki,wanachotaka kuona ni Israel amekuwa wiped out,Israel watakuwa wajinga sana kutowachapa hawa..

"Mess with the bull and you get the horns"
Having said that, Hamas is learning it the hard way you cant fire rockets into another country and when they react preemptively you start whining"

..After the six months of Truce Agreement between the government of Israel and Palestine ended, Hamas sent message to the goverment of Israel by Rocket propelled grenades. Remember Israel always kept away its stance with Palestine. But Hamas through manipulative language to its citizens..

Baada ya kupitia hoja hizo .... vita vya hawa jamaa ni vita vya itikadi kabla ya kuwa vita vya vifaru na majeshi mpakani na mitaani huko gaza.

Kutathmini kinachoendelea gaza kwa kuangalia vifo au ni nani kaanza na ninani hakuuanza ni vigumu kufikia muafaka.

Mfano ukisikia Mtanzania mmoja amekufa huko msumbiji tutauliza ..kifo ni kwa ajali? au ni nini?

Kama ni ajali ambayo ni pure natural ...itaeleweka. Lakini kama amewindwa na kuuwawa kwa makusudi kwa kuwa ni mtanzania tu..itabidi kuhoji na kufuatilia. Serekali ya msumbiji ikishindwa kujibu na ikileta porojo zisizoeleweka tunasisitiza na ikishindikana kabisa hata vita vitatokea kutoa funzo na uhalisia wetu kama watu TUNAHITAJI KUHESHIMIWA PIA. Tutapigana vita. Tutafanya hivyo tena vizuri iwezekanavyo. Idd Amin anajua. Kwenye vita wanaweza kufa watoto na kina Mama etc lakini ni haki yetu kulinda na kutunza utu na Mtanzanania au kujua kwa nini Mtanzania mmoja amenyimwa haki yake ya kuishi na kuwa huru kama mtu.

Mwanachi mmoja wa Israeli akipigwa na roketi toka Hamas, Israeli ikae kimya kwa sababu ni mmoja tu?

Yaani Mmoja tu ndege au Inzi?

Ni mtu.

Na mtu na Utu wake hata kama ni mmoja hapimiki statisticaly. Lazima Alindwe na Kuhakikishiwa usalama wake na Mzazi au Nchi yake.

Kwa hiyo vita kama vya gaza vinapokuwa vinaendelea mtu unaweza kupotoshwa na kuanza kuangalia Statistics...Na kuacha kuangali chimbuko la ulinzi wa Utu na mtu wa nchi husika aliyekosewa hakia yake ya Kuishi na kujisitiri.

Shulihisho la kwanza haliko kwenye Vita maana Tatizo lilianzia kwenye kurusha roketi kwa "sababu nyingine".

Kama sababu hiyo isipo pata suluhu na roketi zinaendela kurushwa lazima kufanya upande wa pili KUTII NA KUHESHIMU na hapo ndipo vita vinatokea na kwenye vita vya kukomboa mtu mmoja ..bado ni vita tu...Upande gani watakufa wachache kwenye vita sio hoja...as long as vita vimefikia kuanza vitaendelea MPAKA HESHIMA IPATIKANE..yaani Upande mwingine UTII.

Kusema tuvunje uhusiano na Israeli kwa mantiki hii ...sioni ina maana yeyote kihivyo.
 
Wana JF,

Katika vita hii inayoendelea ni vigumu kuwalaumu Israel wakati wao wanalojukumu la kujilinda. Tatizo hapa Israel imeamua kutumia nguvu nyingi lakini ukweli unabaki pale pale kwamba hii ni vita na HAMAS inapeleka makombora yake Israel. Uzuri hatupati habari kamili juu ya madhara ya hayo makombora.

Kwa upande mwingine tunapashwa kuyalaumu mataifa ambayo yanaisaidia HAMAS kwa kuwapelekea silaha lakini sasa Wapalestine hata wale ambao labda hawai-support HAMAS wanaumia. Je nchi hizo zinaiunga mkono HAMAS zimefanya nini mpaka sasa ukiacha makombora machache yaliyorushwa Israel kutokea Lebanon? Sasa wanakimbilia suluhisho la kidiplomasia wakati wapalestine wanaendelea kuuwawa. Mbona nchi hizo hazisaidii kuishambulia Israel? Nchi hizo haziwezi kusaidia kuishambulia Israel wazi wazi kwa kuwa kufanya hivyo ni sawa na kuunga mkono kikundi cha kigaidi. HAMAS si jeshi halali la wapalestina. Hivyo wanaogopa kujitokeza hadharani lakini upande wa pili wanaisaidia HAMAS kwa silaha na pesa.

Mataifa hasa ya kiarabu yafike mahali yaache unafiki ambao kwa kweli unawaumiza zaidi wapalestine zaidi ya faida ambayo wanaipata kupitia HAMAS. Mataifa haya yanaiogopa Israel kama ukoma lakini yanaisakizia HAMAS ipigane na Israel.

Nafikiri ilikuwa sahihi sana kwa Tanzania kuwa na neutral stand kwani both HAMAS and Isreal none of them is doing the right thing.

Siku njema.
 
Sidhani kama kuna haja ya kuvunja uhusiano kwa kuwa hilo halitasaidia kumaliza matatizo ya mashariki ya kati.

Kuna haja ya kushinikiza mabadiliko kwenye jumuiya za kimataifa ili ziwe na nguvu zaidi ya kuzuia mauaji ya watu wasio na hatia. Kwa maoni yangu jumuiya za kimataifa kama Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika ni butu mno. Mauaji yaliyotokea Rwanda, Iraq, Dafur na sasa Gaza ni baadhi tu ya vielelezo vya ubutu wa jumuiya hizi.

Pengine, ni kweli si vyema Jumuiya za Kimataifa zikaingilia moja kwa moja uhuru wa nchi kujiendesha. Lakini kama uhuru huu wa kujiendesha unahatarisha maisha ya wananchi wasio na hatia, nadhani ni uhuru usio na maana na hivyo jumuiya za kimataifa zinapaswa kuingilia kati hata kama ni kwa kutumia nguvu.
 
Wana JF,

Katika vita hii inayoendelea ni vigumu kuwalaumu Israel wakati wao wanalojukumu la kujilinda. Tatizo hapa Israel imeamua kutumia nguvu nyingi lakini ukweli unabaki pale pale kwamba hii ni vita na HAMAS inapeleka makombora yake Israel. Uzuri hatupati habari kamili juu ya madhara ya hayo makombora.

Kwa upande mwingine tunapashwa kuyalaumu mataifa ambayo yanaisaidia HAMAS kwa kuwapelekea silaha lakini sasa Wapalestine hata wale ambao labda hawai-support HAMAS wanaumia. Je nchi hizo zinaiunga mkono HAMAS zimefanya nini mpaka sasa ukiacha makombora machache yaliyorushwa Israel kutokea Lebanon? Sasa wanakimbilia suluhisho la kidiplomasia wakati wapalestine wanaendelea kuuwawa. Mbona nchi hizo hazisaidii kuishambulia Israel? Nchi hizo haziwezi kusaidia kuishambulia Israel wazi wazi kwa kuwa kufanya hivyo ni sawa na kuunga mkono kikundi cha kigaidi. HAMAS si jeshi halali la wapalestina. Hivyo wanaogopa kujitokeza hadharani lakini upande wa pili wanaisaidia HAMAS kwa silaha na pesa.

Mataifa hasa ya kiarabu yafike mahali yaache unafiki ambao kwa kweli unawaumiza zaidi wapalestine zaidi ya faida ambayo wanaipata kupitia HAMAS. Mataifa haya yanaiogopa Israel kama ukoma lakini yanaisakizia HAMAS ipigane na Israel.

Nafikiri ilikuwa sahihi sana kwa Tanzania kuwa na neutral stand kwani both HAMAS and Isreal none of them is doing the right thing.

Siku njema.

Ukinipiga kwenzi nikakurudishia kwa kukupiga mtama nitakuwa nimekuonea?

Alafu tusijidanganye, tukivunja uhusiano na Israel hakuna chochote watakachokosa au kupungukiwa, mwisho wa siku nchi wahisani wakikohoa wakasema turudishe uhusiano tutarudisha tu.

Iran imeshaanza kumake moves za ku-urge nchi kuvunja uhusiano na Israel?
 
- Wabongo bwana, kama kawaida yetu kujaribu kujiingiza ingiza kwenye yasiyotuhusu, yanayotuhusu hapa nyumbani ambayo ni mengi sana hata pa kuanzia hujui, lakini sasa tuko ya huko Middle East as if kuna anaye-care kuhusu msimamo wetu na hivyo vita!

Hebu tutafute mbinu za kulinda Albino hapa kwanza, ndio tukasaidie wengine huko Middle East!
 
Nakubaliana na Netanyahu kabisa..

Tanzania tuna priority nyingi sana za zinazotugusa maisha yetu ya kila siku kwa karibu kabisa zaidi ya kuingilia mgogoro ulioko maelfu ya kilometa mbali na nchi yetu. Sijui ni nani alietuloga watanzania tukawa na tukawa na kimbelembele kisichosaidia cha kuingilia mambo yasiyotuhusu na kuacha kushughulikia yale ya muhimu yanayotuhusu......kwenda kuandamana kuwatetea wapalestina si priority kwa nchi yetu hata kidogo....

Sijui ni kwanini Tanzania hatuwezi kujifunza kutokana na makosa sijui ni uvivu wa kufikiri au ni nini hasa kinachotusumbua. Tulipoteza resource nyingi sana kuwatetea nchi nyingine zipate uhuru hali sisi wenyewe tukiwa tumebakia masikini wa kutupwa na wale tuliokua tunawatetea wakiwa na maisha mazuri na zaidi sana wakiwa hawataki hata tukanyage katika nchi zao.

"Everybody is for himself" ….Nashangaa sana bado watanzania wanakua na wema wa mshumaa (kuwamulikia wenzio huku wao wakiteketea) na kupoteza muda wao kutetea kitu ambacho hakitawasaidia wao kwa namna yeyote. By the way hao wapalestina mnaojifanya kuwatetea hawana mpango na sisi hata kidogo ndio maana hata siku moja sijasikia maandamano ya waarabu kutetea mauaji wanayofanyiwa watu weusi au matatizo ya Somalia.

I can assure you, kama ingekua ni waafrika weusi wangekua wanabutuliwa hivi sasa wapalestina wasingepoteza hata lepe la usingizi wao kuandamana kuwatetea. Lets be mature, tuache kupoteza muda kwa kujiingiza katika mambo ambayo hayatuhusu.

Pande zote mbili zikae pamoja zikubaliane. wapalestina waache uchokozi wao kwa kudhani kua ipo siku wataiondoa Israeli katika ile nchi. Watafute suluhisho la kuishi kama raia wema wakifuat asheria na kuacha uchokozi wa kurusha maroketi kwa Israeli. Kama wanaona kuishi kwa Amani na Israeli ni vigumu na kuchagua kutumia ubabe basi matokeo ya kumchokoza mbabe ndio hayo wanayoyavuna sana.

Watu wenyewe hawana nguvu alafu wanampiga Mbabe makonzi, Mbabe anapojibu mapigo kwa kuwakata mitama wanaaanza kulalamika....Oooh anatuonea, anapiga ngumi za machoni...n.k.

Lastly. Ningefurahi sana kwama watanzania tungeamka na kuwa tunafanya vitu kwa faida sit u kwa ushabiki usioleta manufaa kwa taifa. Nasikitika sana ni kwanini hatuna ubalozi wa Israeli hapa Tanzania wakati tunajua ya kwamba kama taifa tungefaidika sana kwa kupata teknolojia na utaalamu wa hali ya juu waliokua nao waisraeli.
 
- Wabongo bwana, kama kawaida yetu kujaribu kujiingiza ingiza kwenye yasiyotuhusu, yanayotuhusu hapa nyumbani ambayo ni mengi sana hata pa kuanzia hujui, lakini sasa tuko ya huko Middle East as if kuna anaye-care kuhusu msimamo wetu na hivyo vita!

Hebu tutafute mbinu za kulinda Albino hapa kwanza, ndio tukasaidie wengine huko Middle East!

......mmmhh!!........Mzee Kheri ya mwaka mpya........
 
Nakubaliana na Netanyahu kabisa..

Tanzania tuna priority nyingi sana za zinazotugusa maisha yetu ya kila siku kwa karibu kabisa zaidi ya kuingilia mgogoro ulioko maelfu ya kilometa mbali na nchi yetu. Sijui ni nani alietuloga watanzania tukawa na tukawa na kimbelembele kisichosaidia cha kuingilia mambo yasiyotuhusu na kuacha kushughulikia yale ya muhimu yanayotuhusu......kwenda kuandamana kuwatetea wapalestina si priority kwa nchi yetu hata kidogo....

Sijui ni kwanini Tanzania hatuwezi kujifunza kutokana na makosa sijui ni uvivu wa kufikiri au ni nini hasa kinachotusumbua. Tulipoteza resource nyingi sana kuwatetea nchi nyingine zipate uhuru hali sisi wenyewe tukiwa tumebakia masikini wa kutupwa na wale tuliokua tunawatetea wakiwa na maisha mazuri na zaidi sana wakiwa hawataki hata tukanyage katika nchi zao.

"Everybody is for himself" ….Nashangaa sana bado watanzania wanakua na wema wa mshumaa (kuwamulikia wenzio huku wao wakiteketea) na kupoteza muda wao kutetea kitu ambacho hakitawasaidia wao kwa namna yeyote. By the way hao wapalestina mnaojifanya kuwatetea hawana mpango na sisi hata kidogo ndio maana hata siku moja sijasikia maandamano ya waarabu kutetea mauaji wanayofanyiwa watu weusi au matatizo ya Somalia.

I can assure you, kama ingekua ni waafrika weusi wangekua wanabutuliwa hivi sasa wapalestina wasingepoteza hata lepe la usingizi wao kuandamana kuwatetea. Lets be mature, tuache kupoteza muda kwa kujiingiza katika mambo ambayo hayatuhusu.

Pande zote mbili zikae pamoja zikubaliane. wapalestina waache uchokozi wao kwa kudhani kua ipo siku wataiondoa Israeli katika ile nchi. Watafute suluhisho la kuishi kama raia wema wakifuat asheria na kuacha uchokozi wa kurusha maroketi kwa Israeli. Kama wanaona kuishi kwa Amani na Israeli ni vigumu na kuchagua kutumia ubabe basi matokeo ya kumchokoza mbabe ndio hayo wanayoyavuna sana.

Watu wenyewe hawana nguvu alafu wanampiga Mbabe makonzi, Mbabe anapojibu mapigo kwa kuwakata mitama wanaaanza kulalamika....Oooh anatuonea, anapiga ngumi za machoni...n.k.


Lastly. Ningefurahi sana kwama watanzania tungeamka na kuwa tunafanya vitu kwa faida sit u kwa ushabiki usioleta manufaa kwa taifa. Nasikitika sana ni kwanini hatuna ubalozi wa Israeli hapa Tanzania wakati tunajua ya kwamba kama taifa tungefaidika sana kwa kupata teknolojia na utaalamu wa hali ya juu waliokua nao waisraeli.

Utaalamu waliokuwa nao haumwagwi kama pipi. Hizo ni ndoto za alinacha. Hoja ya kufunguliwa kwa ubalozi iwe kwa mahusiano ya kijamii kama vile nchi zingine zilivyo na ubalozi.

Kama mnataka wataalamu nimeshauri toeni Uraia kwa wayahudi na waPalestina kwa sababu wengine wanataka sehemu ya kukaa tu na Tanzania mnayo ardhi kubwa.
 
Nashangaa waislamu wanavyoandamana Dar kwa vifo vya wapalestina wakati waislamu weusi wa Darfur wanauwawa kwa wingi huko Sudani ya kusini.Nawataka waache double stardard



Embu angalia vizuri sources zako sudan ya kusini wanakaa wasudani wa upande gani.Sidhani wale janjaweed wanauwa watu wa imani yao.
Mungu pekee anajua yale aliyopanga kwa wanadamu na hizi imani zetu.
 
Tanzania ni nchi isiyofungamana na upande wowote, sawa bwana/bibie

Pia Tanzania sio nchi ya kidini, ndio maana sisi ni marafiki wa Irani, ni marafiki wa Marekani pia

Ni marafiki wa RUSSIA na ni marafiki wa USA

Hiyo ndio raha yake

kama wakigombana ni wao, sisi hatuhusiki, ili mradi tusiwe sehemu ya ugomvi
 
Huko nyuma tuliwahi kusema kuwa "kila mtu anastahili haki ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake". Pia tulisema kwamba kila watu wana haki ya kuwa na mahali ambapo watakuwa salama kutoka vitisho vyovyote vya utu wao na nafasi yao kama jamaa.

Kwa sababu hiyo tuliunga mkono POLISARIO na PLO, kama vile tulivyounga mkono Biafra, kuunga mkono ANC, FRELIMO n.k Tuliamini ya kwamba hakuna mwanadamu mwingine ambaye ana haki ya kumtawala kwa nguvu mwanadamu mwingine kwa kisingizio chochote kile. Hii ilikuwa ni falsafa yetu dhidi ya ukoloni.

Leo hii tunashuhudia yanayoendelea Palestina ambapo karibu maelfu ya watu wameshauawa. Je, Bunge linapokutana siku chache zijazo zilaani mauaji hayo? Je serikali ilaani pande zote mbili kwa kusababisha mazingira ambayo yanamnyima mwanadamu nafasi ya kuwa huru kufanya lolote? Je tuungane na nchi kama Venezuela na Bolivia ambazo zimevunja uhusiano na Israel kutokana na suala la Gaza?

Je tukifanya hivyo hatutaulizwa uhusiano wetu na nchi kama Sudan, Somalia, Iran, n.k ambapo rekodi zao kuhusu haki za binadamu na raia si za kupewa sifa?

Au tuendelee kukaa pembeni tu na kuwaacha "wafu wawazike wafu wao"?

Mzee wa kijiji
Siasa isiyofungamana na upande wowote. Imetufunga?
 
- Wabongo bwana, kama kawaida yetu kujaribu kujiingiza ingiza kwenye yasiyotuhusu, yanayotuhusu hapa nyumbani ambayo ni mengi sana hata pa kuanzia hujui, lakini sasa tuko ya huko Middle East as if kuna anaye-care kuhusu msimamo wetu na hivyo vita!

Hebu tutafute mbinu za kulinda Albino hapa kwanza, ndio tukasaidie wengine huko Middle East!
nimezichunguza hoja zako na kugundua kwamba zimejaa uzawa na uraia wa mipaka , jambo ambalo naliona linakupotezea mwelekeo katika mijadala yako. just kumbuka kwamba hii mipaka kakuwekea mkoloni na isikufanye mipaka hii kumsahau anaedhurika. eniwei , ukihisi kwamba jambo halikuhusu kwanini hukai kimya? badili ya ku interfere mada za watu kwahali ya kuwatoa watu nje ya mada? , aloanzisha hii mada limemgusa ndo maana akaanzisha sasa wewe kama halijakugusa just ignore the thread!. tukirudi kwenye subject , sioni sababu ya kuwa na uhusiano na israel mpaka pale watakapokomesha occupation na wakakubali at least kuishi kwa heshima katika hiyo ardhi walioiba.
 
nimezichunguza hoja zako na kugundua kwamba zimejaa uzawa na uraia wa mipaka , jambo ambalo naliona linakupotezea mwelekeo katika mijadala yako.

- Mkuu mimi sijachunguza hoja zako maana sina huo muda, ila ninajua one thing kwamba unapokuwa na tatizo na hoja zangu huwa unakimbilia hili jina badala ya kutumia jina lako la kawaida, kitu ambacho mtumizma kama mimi siwezi kuthubutu kukifanya, na ndio maana hapa Jf kunakuwa na malumbano ya kitoto ambayo huwa unayaanzisha mara kwa mara kwa kujificha ficha, kwa hiyo nafikiri unazo akili timamu za kusoma between the lines kwamba ni nani exactly asiyekwua na muelekeo kati yangu na wewe!

just kumbuka kwamba hii mipaka kakuwekea mkoloni na isikufanye mipaka hii kumsahau anaedhurika. eniwei , ukihisi kwamba jambo halikuhusu kwanini hukai kimya? badili ya ku interfere mada za watu kwahali ya kuwatoa watu nje ya mada? , aloanzisha hii mada limemgusa ndo maana akaanzisha sasa wewe kama halijakugusa just ignore the thread!.

- Kwa kawaida Jf mkuu huwa hatuogopani, ingawa kuna watu kama wewe na wenzako flani ambao mnaonekana kupenda kuogopwa sana kwamba mkitoa mada au hoja, wengine ni lazima tukubali tu na kama hatutaki kukubali basi tusitoe hoja zetu tofauti on it, really? Eti mkuu ndiyo hasa sababu ya kuwepo kwetu hapa JF?

- Haya where do you draw the line na hii hoja yako uchwara? Kwa mfano viongozi wetu wanasema na kufanya madudu then kwa nini tunawapigia kelele hapa a ku-intefere hoja zao huku tunajua kua hazituhusu? Unasema kuwa-Ignore kwa sababu hoja zao hazijatugusa? Hivi kwenye hoja yangu hapa na hii thread ni wapi nimekutaja jina na kukugusa? Au ni wapi nimemgusa mtoa mada? Uonaona sasa mlikofikia katika kutaka kuimbisha wananchi hapa nyimbo zenu?

- Ebo ni haki yangu kuchangia hoja hapa katika mada yoyote ile kama ilivyohaki ya kila member hapa, mkuu nenda uanzishe forums ambayo utaweka sheria zako kwamba kama mada haikugusi basi ignore, lakini usijaribu kunifundisha mimi mtumizma how to write hapa au what to write, nimesema na ninarudia tena kwamba Tanzania tunamatatizo mengi sana hapa nchini kwetu na besides historia iko wazi kwamba no body cares na msimamo wetu, hasa baada ya kuisha kwa Cold War halafu pia ni haya mambo ya kujiweka kimbele mbele na ishus za mataifa mengine matokeo yake sasa Mozambique na Uganda wanatuacha kimaendeleo sisi bado tunalilia Palestine na Israel ambao hawajawahi kutulilia hata siku moja!

Eti mkuu ni kipi hapa kinakuwa kigumu kwako kuelewa nikusaidie zaidi?


tukirudi kwenye subject , sioni sababu ya kuwa na uhusiano na israel mpaka pale watakapokomesha occupation na wakakubali at least kuishi kwa heshima katika hiyo ardhi walioiba.

- Hivi ni lini Israel imewahi kutaka uhusiano na sisi kwamba sasa tunawawekea masharti ya kuwepo na uhusiano nao? Hebu jaribu kuangalia kwa marefu na mapana ni nani hasa anyemuhitaji mwingine kati yetu na Israel? Sisi tulipo-occupy Uganda ni nani aliyetutenga unayemkumbuka?

- Hivi ni heshima gani hasa unayoitaka kutoka kwa Israel hata baada ya kuwarudishia ardhi yao ya Gaza hawa ndugu zetu Wapalestina? au unasema kwamba Israel wakipigwa rockets wanyamaze ndio itakuwa kuishi kwa amani na ndilo liwe sharti letu kwa Israel ili tuwe na uhusiano nao?

- Unaona tena kumbe hapa ndio kwenye tauizo lako, kwamba Israel wameiba ardhi waliyopewa na UN, sasa unajua kwua siwezi kukubali hii hoja kwa hiyo unaanza na mikwala mingi na vitisho, halafu mwishoni ndio unaweka sasa agenda yako, sasa mkuu wangu kweli unafikiri mimi FMES ninaweza kuupanda huu mkenge wako wa kwamba Israel wameiba ardhi ya Wapalestina? Sasa kwa niniu usieme haya toka mwanzo badala yake ukazunguka mibuyu wee na milima?

Mkuu wangu Tanzania tumefika mahali tutafute mahusiano yenye faida kwetu,na ambayo yanaweza kutusaidia kitaifa huku tuki-maintain heshima yetu mbele ya jumuiya za kimataifa, vita kama hivi haviwezi kuwa dhana ya sisi kuvitumia kama sharti la kidiplomasia katika kuanzisha au kutoanzisha mahusiano na mataifa mengine duniani, tufike mahali sasa Tanzania tujifunze diplomasia za kisasa za "Smart Power" ama sivyo tutaendelea kuachwa nyuma wenzetu wanaondoka mkuu,

By the way naomba uniambie ni nini msimamo wa Uganda na Mozambique katika vita hivi? Bwa ! ha! ha! ha!

Ahsante Mkuu, hii ni kutoka kwa Wazee wa Sauti ya umeme FMES!
 
Sahihisho:Israel iliondoka Gaza Strip mwaka 2005, lakini tangu wameondoka mpaka leo Hamas wanarusha rockets kwa nini, mbona West Bank wanaishi vizuri?

Once again, Israel haitopungukiwa na chochote kwa kutokuwa na uhusiano na Tanzania, heck wameishi miaka mingi bila uhusiano na nchi zote zilizoizungula ispokuwa Jordan na Egypt ndio itakuwa sie? You must be kidding!!!
 
Back
Top Bottom