Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hapo ni maamuzi gani mabaya yamefanywa au ndio hasira za kushindwa UchaguziDuh!
Kiukweli ipo siku hawa wanasiasa wetu atatokea kiongozi mwingine kama JPM atawanyonga wote-tuanze upya! Huwezi ukawa na akili au nia njema na watu wako ukafanya maamuzi kama haya! No way.
Gharama za kuuvunja mkataba utatoa wewe mkuu?Bado nawaza hii nchi inaendeshwa na Sheria zipi hizo ?
Kauli imekaa kitetezi na kiulazimishi hata Kama iwe ni kweli Kuna harufu ya utapeli.
Harufu kabla ya kuufikia mkataba hamziskiagi ?Gharama za kuuvunja mkataba utatoa wewe mkuu?
Hofu yangu. Wanakimbilia mahakama za kimataifa tukivunja mikataba. Na wanashinda na kuendelea kulipwa billions hata kama tutasitisisha huduma. Kama IPTL downs, buzwagi nk
Serikali ya Tanzania imesema itaendelea kuheshimu mikataba yake na kampuni tanzu ya Adani Group licha ya mashtaka mapya dhidi ya Gautam Adani, mwenyekiti bilionea wa kundi hilo, anayekabiliwa na tuhuma za utoaji hongo na udanganyifu, afisa mwandamizi wa Mamlaka ya Bandari amethibitisha.
Wiki iliyopita, Adani na mpwa wake walikabiliwa na mashtaka ya udanganyifu na hati za kukamatwa zilitolewa dhidi yao, wakituhumiwa kupanga njama ya dola milioni 265 kuwahonga maafisa wa India ili kupata mikataba ya usambazaji wa umeme. Hata hivyo, Adani Group imekana tuhuma hizo.
Mwezi Mei, Tanzania ilisaini mkataba wa miaka 30 na Adani Ports, kampuni tanzu ya Adani Group, kuendesha Gati ya Makontena 2 katika Bandari ya Dar es Salaam. Mkataba huo pia ulijumuisha ununuzi wa asilimia 95 ya hisa za Kampuni ya Huduma za Gati za Makontena za Kimataifa ya Tanzania (TICTS) kwa dola milioni 95.
"Hatujakuwa na matatizo na mtu yeyote. Shughuli zetu zote zinafanywa kwa mujibu wa sheria na makubaliano yetu," alisema Plasduce Mbossa, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania, alipoongea na Reuters Jumanne. Alisisitiza kuwa Tanzania haikabiliwi na madai yoyote ya udanganyifu kuhusu mikataba yake. "Kama kuna watu wengine wanachukua hatua, basi wanachukua kwa sababu zao."
Wakati huohuo, nchini Kenya jirani, Rais William Ruto hivi karibuni alifuta mkataba wa Adani wa ujenzi wa njia za kusafirisha umeme. Pia alikataa mapendekezo ya kuongeza barabara ya pili ya ndege na kuboresha kituo cha abiria katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta, mpango ambao ungehusisha mkataba wa upangaji wa miaka 30.
PIA SOMA
- Bilionea Gautam Adani ambaye Kafulila anataka kumpa shirika la TANESCO ashitakiwa kwa utapeli huko Marekani
Sasa unataka tuendelee kuvunja mikataba?Ingekuwa inaendeshwa kwa Sheria na Taratibu basi hizi pesa ambazo tunalipa kila siku kwa kushindwa Kesi sababu ya kuvunja mikataba kama hii ya Mangungo wa Msovero waliotuingiza kwenye hio Mikataba wangekuwa Lupango na sio Kuendelea kula Matunda ya Upuuzi wao...
Tusiingie kwenye Mikataba ya kipuuzi in the first place..., na Hizi Mahakama za Kimataifa ambazo zinaleta loopholes za corporations kuendelea kunyonya developing countries na kuharibu mazingira vifungu vibadilishwe au kwenye mikataba tusiende huko..., sababu kinachoendelea ni watu kuingia kwenye upuuzi wakijua wao na vikaragosi wao wasio wazalendo tutapelekana mahakamani ili wajilipe...Sasa unataka tuendelee kuvunja mikataba?
Bora tuvunje tuwalipe kuliko waendelee kutuibia kila sku.Gharama za kuuvunja mkataba utatoa wewe mkuu?
Wametuibia wapi?Bora tuvunje tuwalipe kuliko waendelee kutuibia kila sku.
We ni msukule wa kijan?!! Au msukule wa kaskazn?!!Wametuibia wapi
Ungesema ni wapi wanatuibia?We ni msukule wa kijan?!! Au msukule wa kaskazn?!!
Kumbe huyo ndio tuliambiwa ni DP World? Tumekwishaa. wavunje haraka kabla hawajapatwa na kashfa zaidi.View attachment 3164291
=
Mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya Bandari nchini Tanzania Bw. Plasduce Mbossa ameliambia The Citizens kuwa TANZANIA inaendelea na mkataba wake wa uendeshaji wa bandari na Kampuni ya Adani Group kupitia Gati No2.
Mtakumbuka Tanzania na Adani Groups wamesaini mkataba wa zaidi ya $95milioni karibu sawa na zaidi ya TZS 247bn wa kuendesha Gate namba 2 utakaodumu kwa miaka 30.
Wakati haya yanaendelea kwa upande wake Bw. Davidi Kafulila Mkurugenzi Mtendaji wa PPP yeye ameendelea kuwa kimya juu ya ama ataendelea na mpango wake wa awali wa kumpata mbia katika Ujenzi wa msongo wa Umeme pamoja na Uendeshaji wa Viwanja vya ndege kwa sharti la PPP kwa kupitia watia nia waliopo au laa.
Wakati huu ambapo Adani Green Energy Ltd pamoja na kampuni ya Uingereza ya Gridworks Development Partners LLP zimeonesha nia hiyo ambazo ndizo kampuni pekee za kigeni zilizoonesha nia ya kuwekeza katika miradi hiyo na kwa kuzingatia tuhuma za sasa za rushwa na Ulaghai dhidi ya billionaire Adani Gautam.
![]()
Tanzania to keep Adani container terminal deal, official says
In May, Tanzania entered into a 30-year concession agreement with Adani Ports.www.thecitizen.co.tz
Hapana huyu ni Gate Namba 2Kumbe huyo ndio tuliambiwa ni DP World? Tumekwishaa. wavunje haraka kabla hawajapatwa na kashfa zaidi.
Mtu pekee wa kusafisha UCHAFU huu ni Kassimu Majaliwa!!!Duh!
Kiukweli ipo siku hawa wanasiasa wetu atatokea kiongozi mwingine kama JPM atawanyonga wote-tuanze upya! Huwezi ukawa na akili au nia njema na watu wako ukafanya maamuzi kama haya! No way.
Kumbe? Sasa kwa kashfa yake Marekani hadi Jirani zetu wamekatisha Mkataba nasi tunaendea je na mwenye kashfa zote hizo.Hapana huyu ni Gate Namba 2