Tanzania kuimarisha ufanisi wa mfumo wa kodi ili kukuza uwekezaji nchini

Tanzania kuimarisha ufanisi wa mfumo wa kodi ili kukuza uwekezaji nchini

Ojuolegbha

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2020
Posts
1,278
Reaction score
797
mini_magick20241116-35876-cfy7d8.jpg

Tanzania imechukua hatua stahiki za kuimarisha ufanisi wa mfumo wake wa kodi, ili kukuza uwekezaji na biashara na mataifa mbalimbali duniani.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Mahamoud Thabit Kombo, amesema hayo tarehe 13 Novemba, 2024 jijini Dar es Salaam alipozungumza na Jumuiya ya Wanadiplomasia wanaowakilisha nchi na Mashirika ya Kimataifa nchini.

Mhe. Kombo amesema Serikali inatambua malalamiko yanayohusiana na mfumo wa ulipaji kodi kwa wafanyabiashara wa ndani na wa kigeni na katika kukabiliana na changamoto hiyo imeunda Tume ya Rais kwa ajili ya kupitia na kutathimini mfumo uliopo, ambapo pia itapitia upya Sera ya kodi. Ameingeza kuwa Serikali itashirikisha wadau mbalimbali ili kutoa maoni yao yatakayochangia kuleta matokeo chanya kwa walipa kodi na tija kwa Taifa.

mini_magick20241116-35876-50sdxn.jpg

Mhe. Kombo ameongeza kuwa, katika kuimarisha Diplomasia ya kijamii na kiuchumi na kuendana na Siasa za kImataifa, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefanya mapitio ya Sera ya Mambo ya Nje ya mwaka 2001.

Amewaambia Mabalozi kuwa mchakato wa mapitio ulijumuisha mashauriano ya kina na wadau mbalimbali ndani ya nchi na nje ya nchi.

“Ni furaha yangu kuwaarifu kuwa Sera ya Mambo ya Nje ya mwaka 2001 sasa itajulikana kama Toleo la 2024 baada ya kuridhiwa na Baraza la Mawaziri tarehe 25 Oktoba, 2024, Kuanzia sasa, Sera ya Mambo ya Nje Toleo la mwaka 2024 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itapatikana kwenu nyote na kwa wadau wengine itakapochapishwa na kusambazwa rasmi”, alisisitiza Balozi Kombo.

mini_magick20241116-35876-xr49yh.jpg

Amesema kuwa Sera ya Mambo ya Nje itaendelea kuzingatia Diplomasia ya Uchumi, na misingi iliyopo ya kulinda maadili ya kijamii na ya kitamaduni ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama kitambulisho muhimu cha Taifa ikilenga kukuza amani, utulivu, usalama, Utawala Bora na Udugu; huku ikiheshimu misingi ya kutofungamana na upande wowote (Non-Alignment); a uhusiano wa Kidiplomasia ya uwili, Kikanda na Kimataifa.

Aliongeza kuwa Sera hiyo ya Mambo ya Nje pia itazingatia masuala mbalimbali ya kisasa ikiwemo matumizi ya Lugha ya Kiswahili yatakayoimarisha diplomasia na kuendeleza ajenda ya Uchumi wa Buluu.

mini_magick20241116-35876-s65jy7.jpg
 

Attachments

  • mini_magick20241116-35876-ehduby.jpg
    mini_magick20241116-35876-ehduby.jpg
    72.4 KB · Views: 3
  • mini_magick20241116-35876-v5kxhb.jpg
    mini_magick20241116-35876-v5kxhb.jpg
    72.2 KB · Views: 3
  • mini_magick20241116-35876-ggf9qn.jpg
    mini_magick20241116-35876-ggf9qn.jpg
    74.3 KB · Views: 4
  • mini_magick20241116-35876-vdp3a3.jpg
    mini_magick20241116-35876-vdp3a3.jpg
    91.9 KB · Views: 6
  • mini_magick20241116-35876-31m107.jpg
    mini_magick20241116-35876-31m107.jpg
    99.8 KB · Views: 4
  • mini_magick20241116-35876-9xdgkj.jpg
    mini_magick20241116-35876-9xdgkj.jpg
    102.5 KB · Views: 3
Back
Top Bottom