Tanzania kuna baadhi ya Mawaziri wana uwezo mdogo, Wenzetu Kenya Rais kavunja Baraza zima la Mawaziri

Tanzania kuna baadhi ya Mawaziri wana uwezo mdogo, Wenzetu Kenya Rais kavunja Baraza zima la Mawaziri

Na Mh mwenyewe anaogopa kuwafukuza kwa sabanu za kisiasa tu ila sio za kiutendaji.

11 July 2024
Nairobi, Kenya,

RUTO AJITOKEZA LEO BILA MPAMBE KUVUNJA BARAZA LA MAWAZIRI
  • Mawaziri 21 watupiwa virago
  • Mwanasheria mkuu naye atimuliwa kwenda nyumbani

View: https://m.youtube.com/watch?v=lfSgveSkXE8


KINYUME na ilivyo desturi yake wakati akihutubia taifa, Rais William Ruto Alhamisi, Julai 11, 2024 wakati akivunja Baraza la Mawaziri hakuwa ameandamana na mlinzi wake.

Kwenye hotuba yake iliyochukua dakika chache tu, Rais Ruto alisimama kidete mbele ya mikrofoni za vyombo vya habari akiwa peke yake na kuporomosha tangazo ambalo limeandaa jukwaa la mazungumzo mazitio kote nchini.

Mlinzi wake wa karibu, hakuwepo.


Kiongozi wa taifa pia hakuwa ameandamana na naibu wake, Bw Rigathi Gachagua, Mkuu wa Mawaziri, Bw Musalia Mudavadi na viongozi wengine wa hadhi ya juu serikalini.

Isitoshe, mazingira ya jukwaa alilohutubia katika Ikulu, Nairobi, hayakuwa na yeyote.

Wanahabari kutoka mashirika mbalimbali ya habari yaliyopeperusha hotuba ya Dkt Ruto mbashara ndiyo walikuwapo, japo hawakupewa fursa ya kurusha maswali.


Hata ingawa alitetea serikali yake ya Kenya Kwanza katika kile alihoji kama kusaidia kuboresha gharama ya maisha, hatua ya kuvunja Baraza la Mawaziri limechochewa kwa kiasi kikubwa na maandamano ya vijana barobaro, walioamua kuchukua hatima ya nchi yao katika mikono yao vijana wa leo kizazi kipya cha Gen Z.

Vijana hao wamekuwa wakishiriki maandamano ya kitaifa kushinikiza serikali kushusha gharama ya maisha, ikiwemo kuwaandalia jukwaa mahususi la kupata kazi na mazingira bora ya ajira na biashara......


MAONI YA WANANCHI :


KATIKA mazingira ya siasa kali ambapo watu wanatishiana, haidhuru nikijaribisha uungwana, nijitie udarai wa kumshauri kiongozi wa nchi jinsi ya kuwa rais bora na wa kupendeza tena.

Nimesalitika kujaribisha uungwana baada ya kumwona Rais William Ruto na wafuasi wake sugu waliomchagua wakisisitiza mitandaoni kwamba Uchaguzi Mkuu ujao utafanyika mnamo mwaka 2027.

Kwa hivyo? Eti yeyote anayeota kwamba anaweza kumshuritisha Dkt Ruto kung’atuka kabla ya wakati huo anatwanga maji kwa kinu akitarajia yampe unga.


Siamini umefika wakati wa kukumbushwa kwamba tuzitayarishe kura zetu, ila tusubiri hadi mwaka 2027.

Afua ni mbili: Ama mihemko na fujo za kizazi kipya, almaarufu Gen Z, imemwogofya mno Dkt Ruto na wafuasi wake, au wamezidi kwa jeuri kiasi kwamba hawajali kelele za vyura wanaojaribu kumzuia ng’ombe kunywa maji.

Niruhusu niamini kwamba Rais Ruto ameshtuliwa na matukio ya hivi majuzi ambapo Gen Z wametokea kutosikia la mwadhini wala la mteka maji msikitini. Hawasemezeki.


Walimshinikiza kuondoa Mswada wa Fedha wa 2024, sasa wanamwambia, tena kwa kufoka: “Anguka nao!” Kimsingi wanamshurutisha ang’atuke kutoka mamlakani, hawamtaki.

Sioni ajabu kwa watu wasiompenda kiongozi wao kumwambia ajiengue kabla ya muhula wake wa kutawala kufikia kikomo; tumemsikia kinara wa Upinzani, Bw Raila Odinga, na wenzake wakisema hivyo tangu mwaka 1992.

Hata hivyo, Raila na wenzake hawajawahi kuyatia moto majengo ya Bunge kama walivyofanya vijana wa Gen Z.

Tuliwazoea Raila na wenzake wakitishia kuongoza maandamano hadi Ikulu, kwenda kumng’oa mwenyeji wake, lakini tulijua ni porojo tu.

Hebu tumbua macho vizuri uone maajabu yanayofanywa na Gen Z. Wakisema watafanya kitu, wanakifanya. Wakisema maandamano yao yanaaza saa sita adhuhuri, yanaanza wakati huo. Na wakiahidi kutia moto majengo ya watu, unashtukia moshi ukifuka kutoka humo!

Wasiloweza kufanya kufikia sasa ni kuitwaa na kuikalia Ikulu, lakini ni siri iliyo wazi kwamba wana nia ya kufanya hivyo, tena wanaitangaza nia hiyo mtandaoni.

Wakati ambapo Mswada wa Fedha wa 2024 uliondolewa na maandamano yakaendelea, nilijiuliza yana umuhimu gani, hasa kwa kuwa kilichowakera kilifutiliwa mbali, ila baadaye niliwaelewa.

Ukitaka kuwaelewa Gen Z, unahitaji tu kujua kwamba Mswada wa Fedha ni kero iliyowasababisha kulipuka, ila haiwi kero ya pekee nchini Kenya.

Gen Z wamekerwa na ufisadi nchini Kenya. Wamekerwa na mazoea ya serikali kuwatumikia Wakenya kwa kiburi kana kwamba inawafanyia hisani.

Wamekerwa na baadhi ya nyuso ambazo zinaonekana kwenye baraza la mawaziri. Hawataki kuwaona watu waliokabiliwa na sakata za kila aina kisha mashtaka yakaondolewa ili wawe mawaziri.

Wanajiuliza iwapo Kenya imepungukiwa na watu wenye maadili kiasi kwamba Rais Ruto analazimika kuwateua mawaziri Bw Mithika Linturi, Bi Aisha Jumwa na wengineo.

Je, hao ndio vielelezo bora nchini? Kabisa hatuna wengine wenye sifa nafuu?

Ningekuwa Rais Ruto, ningecheza kamari kama Rais Kagame wa Rwanda, niwe sehemu ya, na wala si kizingiti dhidi ya, mabadiliko yanayonukia nchini.

Ningewafuta kazi mawaziri wote usiku mmoja, kisha siku inayofuata niwateue wengine wasiowapa Wakenya kinyaa!

Baraza langu jipya lingekuwa na mawaziri 12 pekee, wasio na wasaidizi, na wote wangekuwa na umri wa chini ya miaka 35.

Wote wangekuwa wataalamu wasiojulikana kitaifa, sikwambii kimataifa, na jukumu lao lingekuwa kuwahudumia Wakenya kwa uadilifu wa hali ya juu, lau sivyo wafungwe jela kisheria!

Wazee waliozoea kushikilia nyadhifa za uwaziri na nyinginezo kubwa serikalini ningewatafutia makosa ili ama niwanyamazishe au niwafungulie mashtaka kikweli, walioibia umma warejeshe walichoiba, lau sivyo waozee jela!

Huku moto wa mabadiliko ukiendelea kuwaka, ningeishawishi Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) iwasajili upya wapigakura, shughuli yenyewe iongozwe na Gen Z ili wahamasishane kujiandikisha, nimthubutishe yeyote kunipinga mwaka 2027...

Soma zaidi : Source : TAIFA LEO
 
Mnaamini kurogana sana na ndio maana mnaogopana kwa upumbavu huu
Hakuna cha siasa wala nini

Walikuwa wanaenda mpaka Nigeria kwa yule jamaa
Sasa na yeye kafa ila bado wanaamini ujinga huo
Unaogopa kufukuza kisa ana hirizi linadunda kwenye V8
 
Hapa waziri wa fedha anatukana kabisa lakini Chura hasikii kitu, naibu waziri tena wa kike anatumbukiza chupa ya Coca kwa kijana lakini DPP hampeleki mahakamani na akipelekwa kwa mfumo mwingine binafsi nayo hataki na bado yuko ofisini Chura hasikii!
RC analawiti, RC mwingine anatumia madaraka ya mwenyekiti Ulinzi na Usalama kutaka haki isitendeke na yupo ofisini Chura hasikii maana ni kiziwi. Yapo mengi na yaaibu kubwa lakini serikali ya CCM iko kimya.
Ndipo nikakumbuka Prof Kabudi (kabla ya kuwa wa Jalalani) aliwahi kusema ukimya wa Watanganyika kuna siku utawatoa wakubwa kwenye makazi yao mbio wakiwa uchi kama Nicolai Ceausescu wa Romania
 

Attachments

  • VID-20240710-WA0012.mp4
    3.8 MB
Wee BLACK MOVEMENT, Tafadhali sana! Hebu mtazame Tlaatlaah! Amesema unataka kulinganisha "usiku na giza"? Kabla haujafikia hatua ya kumlaumu mh.Rais Samia, hebu tujitazame sisi wananchi wake, kuanzia sisi wa enzi ya TANGANYIKA na wale wa TANZANIA, je, kichwani zimo? Uzalendo umo, je, linapokuja suala la nchi, ubinafsi huwa tunauacha na kuwa wamoja?

Wenzetu wa KENYA, kichwani zimo, uchawa hawana, na ktk suala la KITAIFA wao huwa wamoja. Kwetu huku, suala la KITAIFA huwa ni la KIBINAFSI, wengi tunasema kwani"KATIBA" inaniletea ugali/chakula mezani!

Je, umeona kiwango chetu cha"AKILI"

Hapa kuna haja na hoja kweli ya kumlaumu MTENDAJI wetu No 1?

Je, tujilaumu sisi wenyewe?

Je, tulaumu utaratibu wetu juu ya jinsi tulivyopata Uhuru wetu?

Hebu hapa wanaJf tulitazame hili kwa jicho la TATU, tulifungue Ili kizazi kijacho kisipate hii laana tuliyonayo sisi. Hapa TANGANYIKA, kila aina ya maliasli tunayo, shida iko wapi? Mfano halisi watazame WA Malaysia, Singapore jinsi walivyoanza.

Hatukutofautiana sana tarehe za kupata Uhuru. Watazame leo hii wapo wapi! Hapa, msilete lawama ya ooh! Wakoloni walitumyonya sana, mara eeh! Mabeberu, mara aah! hao ni ngozi nyeupe!

Sema neno/toa hoja/fikiria kwa
makini hapa
 
Mawaziri wengi wa Tazania wana uwezi mdogo sana wa kufanya kazi, Ila wanabebwa kwa sababu za kisiasa tu.

Na Mh mwenyewe anaogopa kuwafukuza kwa sabanu za kisiasa tu ila sio za kiutendaj...
Hamna hoja yoyote hapa zaidi ya WIVU tu!
 
Bila ya yale maandamano angevunja? Huo ni msukumo wa Gen Z sio maamuzi yake

Usishangae ata akachagua upya teuzi zote
 
Said Mtanda ametajwa Sana kwenye lile sakata la yule binti anaye dai alilawitiwa na Nawanda. Alikua msitari wa mbele kesi isifike mbali. Wangeanza na yeye kabla hawajafika kwa wale ambao tuhuma zao haziko wazi.
Mm naona issue ya Said Mtanda sio issue ya, maana sana kudeal nayo. Ni issue ya, binti mwenye sifa, ya umalaya.

Kuna issue bhana za maana ambazo zinauma sana sana. Mfano, issue ya Bashe kuiba mabilioni ni issue hot sana. Na huyu Msomali mwizi sana, anatakiwa atolewe pale wizarani.

Kuna issue ya Mwigulu Nchemba, kuiba mabilioni, huku anadai eti ananunua magari. Kumbe, anaendesha timu ya mpira, hiyo ni issue hot sana. Na inatakiwa huyu Wazir aondoke pale.

Kuna issue ya Makamba kufanya ufisadi mkubwa Nishati. Hao wote ni wezi na ni mafisadi kubwa. Tusipoteza muda kujadili vi issue ya umalaya, ambayo haviwezi kutusaidia

Issue ya binti ni ya kisiasa zaid na tayari RC katoka. Tujadili mapapa na wezi wanaturudisha nyuma. Wafanyabiashara wanalalamika Kodi. Huku wazir wa fedha akisema bajeti ya ununuzi wa magari imepanda. Lakin kumbe pesa ni za kuendesha timu.

Regard.
 
Mawaziri wengi wa Tanzania wana uwezi mdogo sana wa kufanya kazi, Ila wanabebwa kwa sababu za kisiasa tu.

Kule Kenya, Ruto kavunja Balaza la Mawaziri na anatarajia kutangaza Baraza jipya siku chache zijazo. Haya ni maamuzi Magumu sana ambayo kwa nchi ya kubembelezana kama Tanzania huwezi yakuta kabisa.

Tanzania shida tuna mfumo wa kubembelezana, mfumo wa uchawa na mfumo wa kulindana sana.

Angalia hata Wakuu wa wilaya asilimia 100 wana uwezo mdogo sana ukitoa mihemko yao, kuna yule sijui Mkuu wa wilaya Mlemavu kule Kisarawe yule anauwezo mdogo mno ila ulemevu ndio umempatia ukuu wa wilaya. The same na Wakuu wa mikoa wana uwezo mdoho sana, Makonda anacheza na akili za wajinga wa hili Taifa.

PIA SOMA
- Breaking News: - William Ruto avunja Baraza la Mawaziri Kenya
Balaza ndio kitu gani?
 
Back
Top Bottom