Bolt, Raia wa Jamaica ashinda tena medali ya dhahabu, alipata ushindi huo wa kipekee alipokimbia akitumia muda wa sekunde 9.58, na kukaribia mno kuivunja rekodi ya dunia. Alifuatwa na Mmarekani Justin Gatlin aliyechukua medali ya fedha huku nambari ya tatu ikitwaliwa na Adress de Gresse wa kutoka Canada. Umati mkubwa uliokusnyika katika uwanja mmoja nchini Jamaica ulishangilia kwa shangwe na vigelegele punde tu Bolt alipomaliza mbio hizo. Pia Jemimah Jeptoo Sumgong aliipatia Kenya medali ya kwanza ya dhahabu baada ya kushinda mbio za marathon kwenye mashindano hayo. Hiyo pia ilikuwa medali ya kwanza ya Kenya katika marathon ya wanawake katika michezo ya Olimpiki. Vilevile Sumsong mwenye umri wa miaka 31, alimaliza mbio hizo kwa saa mbili, dakika 24 na sekunde nne, na kumshinda Eunice Kirwa wa Bahrain aliyechukua medali ya fedha. Nafasi ya tatu ilimwendea Muethiopia Mare Dibaba.