Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 1,906
- 5,000
Wakuu kwema?
Kampuni ya Ndege ya Tanzania inatarajiwa kupokea ndege mpya aina ya Boeing B787-8 Dreamliner, yenye uwezo wa kubeba abiria 262.
Tukio la mapokezi ya ndege hiyo mpya linatarajiwa kufanyika leo Agosti 19, katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Abeid Amani Karume, Zanzibar.
Waziri wa Uchukuzi wa Tanzania, Makame Mbarawa amesema kuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt Hussein Ali Mwinyi atashiriki kuipokea ndege hiyo.
Kama mnakumbuka May 2024 ATCL ilitoa taarifa ikikanusha ndege hiyo kupelekwa Malaysia kwaajili ya matengenezo makubwa yaani Check-C sababu wataalamu wa kufanya matengenezo hayo wapo nchini, na kwamba ilikuwa imepelekwa huko kutokana na matatizo ya engine, na ilikuwa imekwama muda mrefu sababu ya ugumu wa upatikanaji wa spea ambazo zina uhitaji mkubwa.
Zaidi kuhusu hili soma hapa: Air Tanzania yadai uhaba wa Injini umesababisha Ndege kukaa muda mrefu Karakana Malaysia
Ikumbukwe pia ndege hizi za Boeing (aina ya Max) licha ya kuwa ni za kisasa zimepigwa marufuku katika nchi nyingi kutokana na kuwa na hitilafu katika mifumo yake ya utengenezaji.
Zaidi soma hapa: Ndege aina ya Boeing 737 Max, ni hatari, zimepigwa marufuku nchi nyingi
Kampuni ya Boeing inaonekana kuwa na makandokando mengi, upande mmoja ndege zinapigwa marufuku kutokana na kuwa na hitilafu, upande mwingine kwenye aina nyingine spea zake ni mtiti kupata kiasi kwamba inachukua zaidi ya mwaka kufanya matengenezo, kwanini bado tunazikimbilia? Ni njia nyingine ya kufanya upigaji kwa kisingizo cha matengenezo?
Kampuni ya Ndege ya Tanzania inatarajiwa kupokea ndege mpya aina ya Boeing B787-8 Dreamliner, yenye uwezo wa kubeba abiria 262.
Tukio la mapokezi ya ndege hiyo mpya linatarajiwa kufanyika leo Agosti 19, katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Abeid Amani Karume, Zanzibar.
Waziri wa Uchukuzi wa Tanzania, Makame Mbarawa amesema kuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt Hussein Ali Mwinyi atashiriki kuipokea ndege hiyo.
Kama mnakumbuka May 2024 ATCL ilitoa taarifa ikikanusha ndege hiyo kupelekwa Malaysia kwaajili ya matengenezo makubwa yaani Check-C sababu wataalamu wa kufanya matengenezo hayo wapo nchini, na kwamba ilikuwa imepelekwa huko kutokana na matatizo ya engine, na ilikuwa imekwama muda mrefu sababu ya ugumu wa upatikanaji wa spea ambazo zina uhitaji mkubwa.
Zaidi kuhusu hili soma hapa: Air Tanzania yadai uhaba wa Injini umesababisha Ndege kukaa muda mrefu Karakana Malaysia
Ikumbukwe pia ndege hizi za Boeing (aina ya Max) licha ya kuwa ni za kisasa zimepigwa marufuku katika nchi nyingi kutokana na kuwa na hitilafu katika mifumo yake ya utengenezaji.
Zaidi soma hapa: Ndege aina ya Boeing 737 Max, ni hatari, zimepigwa marufuku nchi nyingi
Kampuni ya Boeing inaonekana kuwa na makandokando mengi, upande mmoja ndege zinapigwa marufuku kutokana na kuwa na hitilafu, upande mwingine kwenye aina nyingine spea zake ni mtiti kupata kiasi kwamba inachukua zaidi ya mwaka kufanya matengenezo, kwanini bado tunazikimbilia? Ni njia nyingine ya kufanya upigaji kwa kisingizo cha matengenezo?
