SoC02 Tanzania na changamoto za afya ya akili

SoC02 Tanzania na changamoto za afya ya akili

Stories of Change - 2022 Competition
Joined
Aug 27, 2022
Posts
16
Reaction score
14
TANZANIA NA CHANGAMOTO ZA AFYA YA AKILI


Utangulizi


Afya ya akili kwa lugha rahisi tunaweza kusema kuwa ni ustawi wa mtu kisaikolojia na kihisia. Mara nyingi miili yetu huwa na afya njema, lakini kuna wakati miili yetu hupata magonjwa mbalimbali na hivyo kuhitaji tiba ili kurudi kwenye hali au utimamu wake.

Mtu anapokuwa na homa, mvurugiko wa tumbo au aina nyingine za magonjwa nirahisi sana kutambua na hivyo kwenda kwa watoa huduma (hospitali) kwaajili ya kupatiwa matibabu na kufanyiwa vipimo kubaini ugonjwa unaomsumbua mhusika lakini je vipi kuhusu afya ya akili?

Ubongo wa mwanadamu pamoja na kazi zingine unajihusisha zaidi na udhibiti wa mawazo na hisia za mwanadamu. Kama ilivyo kwa miili yetu kupata na kushambuliwa na magonjwa mbalimbali ubongo pia unaweza kuwa na ugonjwa na hivyo kupelekea kubadili hisia zetu, jinsi tunavyofikiri, jinsi tunavyoingiliana na kushirikkiana na watu wengine katika jamii na pia kubadili mienendo na maisha yetu kwa ujumla.

Mabadiliko haya ndiyo tunaweza kusema kuwa ni changamoto za afya ya akili (ugonjwa wa akili), kama ilivyo kwa magonjwa ya mwili mtu mwenye magonjwa ya akili anahitaji msaada kutoka kwa wataalamu wa afya ya akili (washauri na wanasaikolojia) ili aweze kurejea katika hali au utimamu wake wa akili kama mwanzo.

Katika nyakati tofauti tofauti kumekuwa na matukio mengi yanayohusishwa na changamoto za afya ya akili hapa nchini. Vyombo mbalimbali vya habari mitandao ya kijamii katika kipindi hiki vimekuwa vikiripoti matukio ya mauaji ya kinyama, uzalilishaji na ukatili mkubwa wa kijinsia kutokana na kinachodaiwa kuwa ni wivu wa kimapenzi.

  • Visa mbalimbali vilivyoripotiwa kutokana na changamoto za afya ya akili nipamoja na;
  • Mauaji yatokanayo na wivu wa mapenzi
  • Watoto kuua wazazi wao kutokana na mali
  • Wazazi kuua watoto wao kutokana na ugumu wa maisha, udokozi na tabia mbaya
  • Ubakaji na ulawiti kwa watoto
  • Watu kujinyonga na kujirusha kwenye majengo marefu (gorofa) n.k

Changamoto hizi za afya ya akili zinaligarimu taifa kwani waathirika wakubwa ni vijana ambao ni wazalishaji wakubwa na wadau wakubwa wa maendeleo kwa taifa (nguvu kazi ya taifa). Hivyo basi kuwa na waathirika wa magonjwa ya akili wengi katika kundi hili la vijana kunalirudisha nyuma taifa kimaendeleo.


Takwimu za magonjwa ya akili nchini

Katika kuadhimisha siku ya afya ya akili duniani Oktoba 2021 iliripotiwa kuwa Watanzania milioni saba wana matatizo yanayohusiana na afya ya akili(chanzo Mwananchi.co.tz) na miongoni mwa sababu zilizotajwa kuchochea tatizo hilo ni msongo wa mawazo, ugumu wa maisha na matamanio yakuwa na maisha bora.

Takwimu za wizara ya afya nchini Tanzania zinaonesha kuwa mtu mmoja kati ya watu wanne ana magonjwa ya akili (chanzo news.un.org/sw/story/2016) kutokana na hili mkurugenzi mtendaji wa UNICEF, Henrietta Fore alinukuliwa akisema “watoto wengi na vijana, matajiri kwa masikini wote katika kona zote za dunia wanakabiliwa na magonjwa ya afya ya akili, janga hilo halina mipaka huku matatizo ya akili yakianza kabla ya umri wa miaka 14, tunahitaji mikakati ya haraka na bunifu katika kuzuia, kuchunguza na iwapo inahitajika kutibu katika umri mdogo”(chanzo news.un.org/sw/story/2016).

Lakini pia mkurugenzi mkuu wa WHO Dkt Tedros Adhanom Ghebreyesus alinukuliwa akisema “ni watoto wachache tu wana uwezo wa kufikia programu zinazowafundisha mbinu za kukabiliana na hisia zao” (chanzo news.un.org/sw/story/2016). Hii inaonesha ni kwajinsi gani taifa na ulimwengu kwa ujumla unavyokabiliwa na changamoto za afya ya akili kwa watu wa rika lote na hivyo basi hatua makusudi zinapaswa kuchukuliwa kudhibiti hali ya ongezeko la watu wenye matatizo ya afya ya akili.


Mapendekezo
Kuwatumia wataalamu wa saikolojia waliopo nchini ili kutoa elimu juu ya afya ya kili, changamoto zake, sababu zake, dalili zake na wapi mwathirika anaweza kupata msaada wa kisaikolojia.

Kuajiri na kufungua vituo vingi nchini vinavyoweza kutoa msaada wa kisaikolojia kwa jamii. Mfano serikali imeanzisha kwenye vituo vya polisi kitengo cha dawati la jinsia wanawake, wazee na watoto, kamati za mtakuwa, wasaidizi wa sheria vijijini (paralegal) maafisa ustawi na maafisa maendeleo kila ngazi lengo likiwa kukomesha vitendo vya ukatili wa kijinsia bila kujua kuwa wanaofanya vitendo vya ukatili ni waathirika wa magonjwa ya akili na hvyo huhitaji zaidi msaada kutoka kwa wataalamu wa masuala ya saikolojia.

Kutekeleza sera ya elimu ya mwaka 2014 (education and training policy of Tanzania 2014) iliyokuwa inataka kila shule kuajiri mshauri (counselor) ambaye atasaidia wanafunzi juu ya changamoto za afya ya akili wanazokumbana nazo shuleni. Utekelezaji wa sera hii ungesaidia kupunguza waathirika wa matatizo ya akili kwenye jamii zetu lakini pia kuongeza uelewa kwa jamii juu ya changamoto za afya ya akili.

Kuandaa mtaala mpya wenye somo linalohusu afya ya akili toka ngazi za chini za elimu hii itasaidia kupambana na matatizo ya afya ya akili katika umri mdogo.


Hitimisho

Nichukue fursa hii kuishauri serikali yangu kupitia wizara ya afya kuona umuhimu wa kuwa na wataalamu wa saikolojia watakaokuwa na uwezo wa kushughulikia changaomo za afya ya akili wataalamu hawa waajiriwe kama wanavyoajiriwa wataalamu wa afya ya mwili kwa wingi hili litasaidia kujenga jamii imara isiyo kuwa na changamoto za ukatili wa kijinsia, mauaji ya kikatili yasiyokuwa na sababu za msingi ambayo yanaligarimu taifa. Ikumbukwe kuwa hakuna afya ya mwili bila afya na utimamu wa akili.

Ahsanteni sana naomba kuwasilisha.
 

Attachments

Upvote 10
Niwashukuru wale mnaoendelea kusoma makala yangu natumaini kuna jambo tunaweza kulipata linaloweza kubadilisha mitazamo yote juu ya afya ya akili
 
Nimekupa kura, hakuna awareness/uelewa wa afya ya akili katika jamii...wachache sana wakipatwa na changamoto ya afya ya akili wanajua waende wapi au wamfate nani au wafanyeje.....na hii inachangiwa na serikali kutolipa hili swala uzito, kuna kampeni kibao za ukimwi, saratani, etc lakini hardly utasikia uzinduzi wa kampeni za mambo ya afya ya akili, surely kama mtu mmoja kati ya wanne wana matatizo ya afya ya akili its time serikali na hili WAKALITAZAME!
 
Nimekupa kura, hakuna awareness/uelewa wa afya ya akili katika jamii...wachache sana wakipatwa na changamoto ya afya ya akili wanajua waende wapi au wamfate nani au wafanyeje.....na hii inachangiwa na serikali kutolipa hili swala uzito, kuna kampeni kibao za ukimwi, saratani, etc lakini hardly utasikia uzinduzi wa kampeni za mambo ya afya ya akili, surely kama mtu mmoja kati ya wanne wana matatizo ya afya ya akili its time serikali na hili WAKALITAZAME!
Nimekupa kura, hakuna awareness/uelewa wa afya ya akili katika jamii...wachache sana wakipatwa na changamoto ya afya ya akili wanajua waende wapi au wamfate nani au wafanyeje.....na hii inachangiwa na serikali kutolipa hili swala uzito, kuna kampeni kibao za ukimwi, saratani, etc lakini hardly utasikia uzinduzi wa kampeni za mambo ya afya ya akili, surely kama mtu mmoja kati ya wanne wana matatizo ya afya ya akili its time serikali na hili WAKALITAZAME!
Na hiyo takwimu ni ya mwaka jana nafikiri mwaka huu takwimu itaongezeka zaidi kutokana na mambo kadhaa yanayosababisha mfadhaiko wa akili mfano mabadiliko ya tabia nchi yameathiri sana watu ukame watu hawana chakula garama zamaisha zimepanda hii imechangia sana watu kuwa na msongo wa mawazo unaowabadilisha mitizamo yao, hisia zao na saikolojia yao kwa ujumla watu wanachangamoto lakini hawajui pa kuzipeleka. Lakini wataalamu wapo na hawatumiki tukipaza sauti kupitia jukwaa hili nafikiri serikali itatoa kipaumbele katika kutatua hili
 
Nimekupa kura, hakuna awareness/uelewa wa afya ya akili katika jamii...wachache sana wakipatwa na changamoto ya afya ya akili wanajua waende wapi au wamfate nani au wafanyeje.....na hii inachangiwa na serikali kutolipa hili swala uzito, kuna kampeni kibao za ukimwi, saratani, etc lakini hardly utasikia uzinduzi wa kampeni za mambo ya afya ya akili, surely kama mtu mmoja kati ya wanne wana matatizo ya afya ya akili its time serikali na hili WAKALITAZAME!
Nimekupa kura, hakuna awareness/uelewa wa afya ya akili katika jamii...wachache sana wakipatwa na changamoto ya afya ya akili wanajua waende wapi au wamfate nani au wafanyeje.....na hii inachangiwa na serikali kutolipa hili swala uzito, kuna kampeni kibao za ukimwi, saratani, etc lakini hardly utasikia uzinduzi wa kampeni za mambo ya afya ya akili, surely kama mtu mmoja kati ya wanne wana matatizo ya afya ya akili its time serikali na hili WAKALITAZAME!
Na hiyo takwimu ni ya mwaka jana nafikiri mwaka huu takwimu itaongezeka zaidi kutokana na mambo kadhaa yanayosababisha mfadhaiko wa akili mfano mabadiliko ya tabia nchi yameathiri sana watu ukame watu hawana chakula garama zamaisha zimepanda hii imechangia sana watu kuwa na msongo wa mawazo unaowabadilisha mitizamo yao, hisia zao na saikolojia yao kwa ujumla watu wanachangamoto lakini hawajui pa kuzipeleka. Lakini wataalamu wapo na hawatumiki tukipaza sauti kupitia jukwaa hili nafikiri serikali itatoa kipaumbele katika kutatua hili
 
Na hiyo takwimu ni ya mwaka jana nafikiri mwaka huu takwimu itaongezeka zaidi kutokana na mambo kadhaa yanayosababisha mfadhaiko wa akili mfano mabadiliko ya tabia nchi yameathiri sana watu ukame watu hawana chakula garama zamaisha zimepanda hii imechangia sana watu kuwa na msongo wa mawazo unaowabadilisha mitizamo yao, hisia zao na saikolojia yao kwa ujumla watu wanachangamoto lakini hawajui pa kuzipeleka. Lakini wataalamu wapo na hawatumiki tukipaza sauti kupitia jukwaa hili nafikiri serikali itatoa kipaumbele katika kutatua hili
Asante kwa kusoma na kupigia kura makala yangu 🙏🙏🙏
 
Naombeni wadau ukipata mda pitia makala yangu na ikikupendeza uipe kura ili kupitia jukwaa hili la story of change serikali ione umuhimu wa kupambana na changamoto hizi za afya ya akili ni wazi kuwa kundi hili labmagonjwa ya akili lipo kwenye makindi ya magonjwa yasiyoambukiza lakini waathirika wake ni wengi na hawapati msaada wa tiba kutoka kwa wataalamu wa tiba ya afya ya akili
 
Tatizo ni kubwa kuliko tunavyodhani.
Tupaze sauti tuokoe kizazi hichi na kijacho watu wengi watafungwa kutokana na mauajia yanayosababishwa na wivu wa mapenzi lakini kuwafunga sio suluhisho zaidi ya kumuongezea matatizo mengine ya afya ya akili
 
Kuwaona wataalamu gharama kinoma .
Kikubwa ni uelewa kwani hata mtu akiwa na magonjwa mengine kama saratani, magonjwa ya moyo n.k garama kubwa hutumika kutibu .
Lakini pia kuna kituo kinatoa hudhma za ushauri na saikolojia kinaitwa Same Counseling Foundation kipo wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro lakini pia watu hawaendi kwa wingi kupata msaada wa kisaikolojia kwahiyo swala kubwa ni uelewa wa hizi changamoto kabla ya tiba. Lakini pia kukiwa na wataalamu na vituo vingi vinavyotoa tiba ya afya ya akili garama zitapungua🙏🙏🙏
Usisahau kupaza sauti yako kwa kunipigia kura
 
Tunapozingatia kwenda kwenye vituo vya afya na kwenye hospitali kubwa kufanya uchunguzi (checkup) tusisahau kwenda kwenye vituo vya ushauri na kwa wataalamu wa saikolojia na afya ya akili kuangalia utimamu wetu wa kisaikolojia na kihisia kwani utimamu wetu wa kihisia na kisaikolojia una mchango mkubwa kwenye utimamu wetu wa mwili kumbuka hata baadhi ya maradhi ya moyo na presha husababishwa na misongo ya mawazo na changamoto zingine za kisaikolojia. Tusichukulie poa afya ya akili ni muhimu kwa ustawi wako, familia yako, jamii yako na taifa kwa ujumla. Vunja ukimwa waone wataalamu wakushauri ✍️
 
Kuna msemo usemao "self care is not a selfish" ukiwa na maana kuwa kujijali sio ubinafsi.
Unapojali afya yako ya mwili kwa chakula kizuri, mavazi mazuri na hata matibabu mazuri kumbuka pia kujali afya yako ya akili.
Natambua kuwa tunatingwa na shughuli m alimbali za kutafuta tonge lakini tufanye mambo ya kasaida katika siku za weekend ili tuweze kutafuta utimamu wa mwili na akili kwa juma lingine la utafutaji
1️⃣ Pata muda wa kupumzika na kutafakari hali yako ya utendaji kwa week nzima ikiwa na maana kuwa ulifanikiwa wapi na ulikwama wapi ili uboreshe.
2️⃣ tafuta jambo linaloweza kukuburudisha mfano tembelea fukwe, milima, ndugu jamaa na marafiki na furahi nao.
3️⃣ Fanya mazoezi ili kuufanya mwili upumue hii ni sawa na kureboot au kurefresh kifaa kama pc au simu.
4️⃣ Kumbuka kunywa maji kwa kiwango kinachostahili

Mwisho kumbuka ibada and always be positive ✍️
 
Habari ndugu zangu wana JF nipende kuwaalika kusoma makala yangu ju ya afya ya akili na ikikupendeza nipigie kura ili ilete tija kwa jamii jinsi ya kupiga kura gusa kimshale "^" mwisho wa makala yangu na utakuwa umeshapigia kura makala yangu 🙏🙏
 
Back
Top Bottom