Tanzania na Ireland kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na maendeleo

Tanzania na Ireland kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na maendeleo

Ojuolegbha

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2020
Posts
1,278
Reaction score
797
Tanzania na Ireland zimeazimia kuimarisha ushirikiano katika nyanja mbalimbali za maendeleo na uchumi ili kukuza uhusiano wa kidiplomasia, biashara, na uwekezaji kati ya Nchi hizo mbili.

Makubaliano hayo yamefikiwa wakati wa mazungumzo rasmi kati ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) na Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Ireland anayeshughulikia masuala ya ushirikiano wa kimataifa, maendeleo, na Diaspora, Mhe. Neale Richmond.

Mazungumzo hayo yamefanyika katika ofisi ndogo ya Wizara jijini Dar es Salaam, ambapo viongozi hao walijadili fursa na mikakati ya kuimarisha mahusiano ya pande mbili kwa manufaa ya kiuchumi na kijamii.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Kombo ameishukuru Serikali ya Ireland kwa ushirikiano wa muda mrefu na mchango wake katika sekta za elimu, biashara, uwekezaji, utalii, afya, jinsia, uwezeshaji wa wanawake, pamoja na mifugo.

Aidha, alimpongeza Mhe. Richmond kwa ziara yake rasmi nchini Tanzania tangu alipoteuliwa, akisisitiza kuwa ziara hiyo ni ishara ya juhudi za dhati za kuimarisha uhusiano kati ya mataifa haya mawili.

Mhe. Kombo amesisitiza umuhimu wa kuongeza kiwango cha biashara kati ya Tanzania na Ireland, akihimiza wawekezaji kutoka Ireland kuchangamkia fursa zilizopo nchini, hasa katika sekta za kilimo, utalii, nishati mbadala, teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA), viwanda, na miundombinu.

Pia, amebainisha kuwa kiwango cha biashara kati ya mataifa hayo bado ni kidogo, hivyo kuna haja ya kuweka mikakati madhubuti ya kuongeza biashara yenye uwiano sawa.

Katika sekta ya utalii, Waziri Kombo amependekeza kuimarishwa kwa juhudi za kutangaza vivutio vya Tanzania kwa soko la Ireland na kuboresha miundombinu ya usafiri ili kuvutia wageni zaidi.

Aidha, amependekeza kuanzishwa kwa mfumo wa mashauriano ya kisiasa kati ya Tanzania na Ireland ili kuimarisha zaidi uhusiano wa kidiplomasia na kuweka msingi wa ushirikiano wa karibu katika masuala ya kimataifa.

Kwa upande wake, Mhe. Richmond ameahidi kuimarisha mshikamano wa kiuchumi na kijamii kati ya mataifa haya mawili kwa manufaa ya pande zote.

publer-1741964760094.jpg
publer-1741964738911.jpg
publer-1741964761783.jpg
 

Attachments

  • publer-1741964763522.jpg
    publer-1741964763522.jpg
    52.9 KB · Views: 1
  • publer-1741964740856.jpg
    publer-1741964740856.jpg
    84.9 KB · Views: 1
  • publer-1741964742722.jpg
    publer-1741964742722.jpg
    85.2 KB · Views: 1
  • publer-1741964765256.jpg
    publer-1741964765256.jpg
    71.6 KB · Views: 1
  • publer-1741964767070.jpg
    publer-1741964767070.jpg
    70.3 KB · Views: 1
  • publer-1741964746251.jpg
    publer-1741964746251.jpg
    82.3 KB · Views: 1
  • publer-1741964751712.jpg
    publer-1741964751712.jpg
    82.1 KB · Views: 1
  • publer-1741964749915.jpg
    publer-1741964749915.jpg
    79 KB · Views: 1
  • publer-1741964756704.jpg
    publer-1741964756704.jpg
    89.9 KB · Views: 1
  • publer-1741964755350.jpg
    publer-1741964755350.jpg
    118.5 KB · Views: 1
  • publer-1741964753407.jpg
    publer-1741964753407.jpg
    77.2 KB · Views: 1
  • publer-1741964768975.jpg
    publer-1741964768975.jpg
    92.3 KB · Views: 1
  • publer-1741964770774.jpg
    publer-1741964770774.jpg
    110.6 KB · Views: 1
  • publer-1741964744534.jpg
    publer-1741964744534.jpg
    54.8 KB · Views: 1
  • publer-1741964758334.jpg
    publer-1741964758334.jpg
    85.5 KB · Views: 1
  • publer-1741964748079.jpg
    publer-1741964748079.jpg
    81.2 KB · Views: 1
Tanzania na Ireland zimeazimia kuimarisha ushirikiano katika nyanja mbalimbali za maendeleo na uchumi ili kukuza uhusiano wa kidiplomasia, biashara, na uwekezaji kati ya Nchi hizo mbili.

Makubaliano hayo yamefikiwa wakati wa mazungumzo rasmi kati ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) na Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Ireland anayeshughulikia masuala ya ushirikiano wa kimataifa, maendeleo, na Diaspora, Mhe. Neale Richmond.

Mazungumzo hayo yamefanyika katika ofisi ndogo ya Wizara jijini Dar es Salaam, ambapo viongozi hao walijadili fursa na mikakati ya kuimarisha mahusiano ya pande mbili kwa manufaa ya kiuchumi na kijamii.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Kombo ameishukuru Serikali ya Ireland kwa ushirikiano wa muda mrefu na mchango wake katika sekta za elimu, biashara, uwekezaji, utalii, afya, jinsia, uwezeshaji wa wanawake, pamoja na mifugo.

Aidha, alimpongeza Mhe. Richmond kwa ziara yake rasmi nchini Tanzania tangu alipoteuliwa, akisisitiza kuwa ziara hiyo ni ishara ya juhudi za dhati za kuimarisha uhusiano kati ya mataifa haya mawili.

Mhe. Kombo amesisitiza umuhimu wa kuongeza kiwango cha biashara kati ya Tanzania na Ireland, akihimiza wawekezaji kutoka Ireland kuchangamkia fursa zilizopo nchini, hasa katika sekta za kilimo, utalii, nishati mbadala, teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA), viwanda, na miundombinu.

Pia, amebainisha kuwa kiwango cha biashara kati ya mataifa hayo bado ni kidogo, hivyo kuna haja ya kuweka mikakati madhubuti ya kuongeza biashara yenye uwiano sawa.

Katika sekta ya utalii, Waziri Kombo amependekeza kuimarishwa kwa juhudi za kutangaza vivutio vya Tanzania kwa soko la Ireland na kuboresha miundombinu ya usafiri ili kuvutia wageni zaidi.

Aidha, amependekeza kuanzishwa kwa mfumo wa mashauriano ya kisiasa kati ya Tanzania na Ireland ili kuimarisha zaidi uhusiano wa kidiplomasia na kuweka msingi wa ushirikiano wa karibu katika masuala ya kimataifa.

Kwa upande wake, Mhe. Richmond ameahidi kuimarisha mshikamano wa kiuchumi na kijamii kati ya mataifa haya mawili kwa manufaa ya pande zote.
well done ndugu waziri 💪👊
 
Bila kuandaa watu na kuheshimu taaluma za watu hakuna maendeleo yatapatikana hata kama Tanzania itasaini ushirikiano na Marekani, nchi imejaa matumizi makubwa ya anasa tupu
 
Back
Top Bottom