Tanzania na Uganda zatajwa kushiriki majaribio ya chanjo ya HIV

Tanzania na Uganda zatajwa kushiriki majaribio ya chanjo ya HIV

Sawa ! Lakini utafiti wa kwetu tumefanyia kazi kwa kiwango kipi ?
MFANO NI JINSI NIMR WALIVYOTENGENEZA DAWA LISHE YAKUPAMBANA NA MATATIZO YA CORONA NA "KUPATA SHUHUDA NYINGI"


Tukatae na hili, tutumie tiba za asili.

Tujali vya kwetu.
 
kwaio katika mwaka unameza vidonge 365? biashara tu hio
 
Ile chanjo waliyochanjwa polisi iliishia

Kwa ufupi jitihada hizi utafiti wa kinga zilianza mwishoni mwa miaka ya 1980 kwenye nchi zilizoendelea kama vile Marekani ambako chanjo mpya ya majaribio ilianza 1987. Chanjo iliyofanyiwa utafiti na kujaribiwa ilikuwa HIV-1 ambayo ni mkakati wa gharama nafuu zaidi kwa kinga na udhibiti wa maambukizo ya HIV-1 duniani na Tanzania kwa jumla. Tangu wakati huo zaidi ya aina 30 tofauti za chanjo zimejaribiwa zaidi ya mara 100 katika awamu I/II kwa kushirikisha watu wengi wa kujitolea wasio na maambukizo ya VVU. Utengenezaji wa chanjo hufanyika kwa awamu. Kuna awamu moja hadi tatu na nchi zimo kwenye awamu tofauti.

Nchini Tanzania kuna maeneo matatu ya mradi wa kutayarisha majaribio ya kitabibu ya chanjo ambayo ni Muhimbili, Mbeya na Hospitali ya KCMC Moshi. Kazi ya utayarishaji wa chanjo nchini Tanzania ilijumuisha kufanya kazi na makundi rika ya polisi Dar es Salaam na makundi rika ya jamii Mbeya pamoja na kujenga uwezo tangu mwaka 1994. Mpango wa HIV wa Jumuiya ya Ulaya ulisaidia utafiti wa Vaccine Immunogenicity (Awamu I/II) nchini Tanzania tangu mwaka 2004. Kwa maelezo zaidi tembelea tovuti ya TACAIDS: www.tacaids.go.tz
 
Tanzania na Uganda zimetajwa kuwa kati ya nchi nne za Afrika kushiriki kwenye majaribio ya chanjo ya virusi ya UKIMWI, ikiwa ni sehemu ya jaribio la kwanza barani Afrika kujaribu chanjo mbili mpya dhidi ya VVU. Imearifiwa kuwa tayari majaribio yameanza wiki hii nchini Uganda na Afrika Kusini. Kwenye majaribio hayo chanjo mbili za mchanganyiko zitatolewa ili kuona kama zinaweza kuweka kinga kwa watu walio katika hatari ya kuambukizwa. Moja ya chanjo hiyo itakuwa ni kidonge cha kila siku.

Chanjo hizo mbili zimejaribiwa kwa usalama katika majaribio ya kimatitabu yaliyopita barani Afrika, Ulaya na Amerika. Kwenye majaribio ya sasa zaidi ya watu 1,600 wenye umri kati ya umri wa miaka 18 na 40 wanatarajiwa kushiriki katika majaribio yatakayofanyika kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo nchini Uganda, Tanzania, Msumbiji na Afrika Kusini. Utafiti huo unafadhiliwa na Ushirikiano wa Majaribio ya kimatibabu ya Nchi za Ulaya na kuungwa mkono na Umoja wa Ulaya.

Chanzo cha taarifa: Idhaa ya Kiswahili ya Radio China Kimataifa

Mwisho nimeongeza PDF ya Utafiti wa PrEPVacc kwenye bandiko hili; ambayo ni muhimu kufungua na kusoma.
View attachment 1655789

===============

Utafiti huu wa PrEPVacc ni nini?

PrEPVacc ni vitu viwili:

Ni kupima kama aina mbili za mchanganyiko wa chanjo ya majaribio zinaweza kukinga dhidi ya VVU. Aina zote hizi mbli za mchanganyiko tayari zilishajaribiwa kwenye tafiti za kitabibu na zimeonyesha usalama wake na kwa wakati huo huo, inapima aina mpya ya dawa kinga ya VVU (PrEP) dhidi ya dawa kinga ya VVU (PrEP) inayotumika sasa.

Utafiti uko wapi?

Utafiti huu unapangwa kufanyika kwenye vituo vitano katika nchi 4: Masaka, Uganda; Mbeya, Tanzania; Dar-es-Salaam, Tanzania; Maputo, Msumbiji na Durban, Afrika Kusini.

Chanjo ya VVU ni nini?

Chanjo inafundisha mwili kujikinga dhidi ya maambukizi fulani au kupigana na ugonjwa kwaajili ya kukuweka na afya njema. Dunia bado haina chanjo inayo kinga VVU iliyosajiliwa. Ili kutengeneza chanjo, watafiti wanahitaji kuipima kwa watu, ili kugundua kama itaweza kusaidia kukinga au kupigana na VVU. Inatolewa kwa sindano.

Dawa Kinga ya VVU ya Kumeza (Oral PrEP) ni nini?

Dawa Kinga ya VVU (PrEP) ni matumizi ya dawa za kufubaza VVU kwa watu wasio na maambukizi ya VVU ili kupunguza hatari yao ya kupata maambukizi ya VVU. Dawa Kinga ya VVU imeonyesha kuzuia VVU na inapatikana duniani kama kidonge.

Utatoa mchango gani kwa kushiriki?

Kuna njia nyingi za kuzuia VVU, ila kila mwaka maambukizi mapya yanaendelea kuripotiwa. Ushiriki wako na jitihada zako zitasaidia kujibu maswali mawili kwa taarifa ambazo zinaweza kusaidia kuzuia maambukizi mapya kwenye jamii yako.

• Tutaweza kusema iwapo utengenezwaji wa aidha ya mchanganyiko miwili ya chanjo ya kuzuia VVU inafaa au la

• Tutaweza kusema kama aina mpya ya dawa kinga ya VVU (PrEP) inakubalika, ni salama na ina ufanisi kama aina ya dawa kinga ya VVU ya kumeza inayotumika kwa hivi sasa na wanawake pamoja na wanaume

Wanawake na wanaume wenye umri wa miaka 18–40 wenye hatari ya kupata maambukizi ya VVU wanaalikwa kushiriki kwenye utafiti wa PrEPVacc.

Unaweza kushiriki kama:

• Una afya njema

• Una umri wa miaka 18–40 siku ya mchujo

• Una utayari na una uwezo wa kutoa ridhaa kushiriki kwenye utafiti huu

• Una utayari na unaweza kuja katika mahudhurio yote na kufanyiwa kipimo cha VVU na kutoa damu, mkojo na sampuli nyingine kwa wakati zinapohitajika

Afya na haki za washiriki zitalindwa vipi?

Wakati wote tutawapa washiriki taarifa kamili kuhusu utafiti kabla mshiriki hajajiunga kwenye utafiti, ili uweze kutupa ridhaa ya kushiriki.

Washiriki wana haki ya kujitoa kwenye utafiti wakati wowote.

Kipindi cha utafiti, wafanyakazi wa kliniki watawafuatilia washiriki ili kuhakikisha kwamba chanjo na dawa kinga dhidi ya VVU hazisababishi matatizo yoyote ya kiafya.

Wafanyakazi wa utafiti pia, watawasaidia washiriki kuripoti matatizo yoyote ya kijamii ambayo wanapata kutokana na kuwepo kwenye utafiti.

Usalama wa washiriki upo chini ya uangalizi wa timu inayofuatilia usalama na bodi ya kujitegemea ya ufuatiliaji wa usalama ambayo mara kwa mara huangalia taarifa za kiafya za washiriki na kuamua kama ni salama kuendelea na chanjo na dawa kinga ya VVU.

Kamati ya maadili ya kitaasisi inapitia na kufuatilia mpango wa utafiti kwa kila kituo kinachofanya utafiti huu, pamoja na taarifa inayotolewa kwa watu kuhusu utafiti huu, maendeleo ya utafiti, na matatizo ya kiafya ya washiriki. Kamati hii ya maadili pia huangalia kama haki za washiriki zinaheshimiwa.

Kila kliniki ya utafiti ina bodi ya ushauri wa jamii. Wajumbe wake ni watu wa mahali hapo hapo ambao wanashauri watafiti na kuleta wasiwasi na masilahi ya jamii na washiriki wa utafiti kwa watafiti.
I assume this is another fake news since source imetoka radio China
 
Ile chanjo waliyochanjwa polisi iliishia wapi.


UTAFITI WA MUHAS WAONYESHA CHANJO DHIDI YA VVU NI SALAMA TUTAUPINGA NAO ?​

Akiwasilisha matokeo hayo, Profesa wa Mikrobiolojia na Immunolojia MUHAS, Eligius Lyamuya, amesema chanjo hiyo iliyofanyiwa majaribio imetengenezwa nchini Sweden na wataalam wenzao ambao wanashirikiana nao katika masuala ya tafiti; "Tumeifanyia utafiti chanjo hii tuliangalia iwapo ni salama na iwapo ina uwezo wa kuchangamsha ile kinga ya mwili kutengeneza viashiria vya kinga na iwapo ina uwezo wa kutengeneza chembe chembe hai za mwili. "Au uwezo wa kutengeneza molecular mbalimbali ambazo zinaashiria hii inaweza kuwa zinahusika katika kinga dhidi ya chanjo ambayo imetolewa." Hivyo, tumebaini chanjo hii ni salama na wote waliochanjwa hakuna ambaye amepata madhara yoyote hadi sasa wako vizuri," alisema.

Chanjo dhidi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU) inayofanyiwa majaribio nchini Tanzania ni salama na ina uwezo wa kuufanya mwili kutengeneza viashiria vya kinga.Hata hivyo hiyo haimaanishi chanjo hiyo ni kinga dhidi ya Maambukizi ya Virusi (VVU) hivyo, matokeo ya utafiti uliofanywa na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), yamebainisha. UTAFITI WA MUHAS WAONYESHA CHANJO DHIDI YA VVU NI SALAMA


I assume this is another fake news since source imetoka radio China
Tunashindwa nini kutembelea vituo vya utafiti huu unaofanyika Tanzania ?
Utafiti huu unakufanyika kwenye vituo vitano katika nchi 4: Masaka, Uganda; Mbeya, Tanzania; Dar-es-Salaam, Tanzania; Maputo, Msumbiji na Durban, Afrika Kusini. Nimeweka pdf ili kupata maelezo ya kwenye chapisho la kwanza katika bandiko hili na rejeja kwa kubofya link Tanzania na Uganda zatajwa kushiriki majaribio ya chanjo ya HIV
 
Hapo lengo si kupata hiyo chanjo, lengo ni kumegewa fungu nono toka WHO ili waweze kuzitafuna, ni hilo tu; otherwise chanjo ikipatikana biashara si ndio inakuwa imefika mwisho? Sasa nani atakubali biashara yake ife
 
Habari za namna hii Zipo tangu miaka ya 70 na zitaendelea kuwepo kwasababu NI MIRADI YA WATU !

Na atakayegundua Tiba Atauwawa haraka sana kwasababu HIV project ni Business! (Biashara)
Unadhani wanasayansi miaka yote hiyo wakiamua wanashindwa?
Jibu ni kwamba hawawezi coz Biashara
Mbona corona wameipata?
 
Tanzania na Uganda zimetajwa kuwa kati ya nchi nne za Afrika kushiriki kwenye majaribio ya chanjo ya virusi ya UKIMWI, ikiwa ni sehemu ya jaribio la kwanza barani Afrika kujaribu chanjo mbili mpya dhidi ya VVU. Imearifiwa kuwa tayari majaribio yameanza wiki hii nchini Uganda na Afrika Kusini. Kwenye majaribio hayo chanjo mbili za mchanganyiko zitatolewa ili kuona kama zinaweza kuweka kinga kwa watu walio katika hatari ya kuambukizwa. Moja ya chanjo hiyo itakuwa ni kidonge cha kila siku.

Chanjo hizo mbili zimejaribiwa kwa usalama katika majaribio ya kimatitabu yaliyopita barani Afrika, Ulaya na Amerika. Kwenye majaribio ya sasa zaidi ya watu 1,600 wenye umri kati ya umri wa miaka 18 na 40 wanatarajiwa kushiriki katika majaribio yatakayofanyika kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo nchini Uganda, Tanzania, Msumbiji na Afrika Kusini. Utafiti huo unafadhiliwa na Ushirikiano wa Majaribio ya kimatibabu ya Nchi za Ulaya na kuungwa mkono na Umoja wa Ulaya.

Chanzo cha taarifa: Idhaa ya Kiswahili ya Radio China Kimataifa

Mwisho nimeongeza PDF ya Utafiti wa PrEPVacc kwenye bandiko hili; ambayo ni muhimu kufungua na kusoma.
View attachment 1655789

===============

Utafiti huu wa PrEPVacc ni nini?

PrEPVacc ni vitu viwili:

Ni kupima kama aina mbili za mchanganyiko wa chanjo ya majaribio zinaweza kukinga dhidi ya VVU. Aina zote hizi mbli za mchanganyiko tayari zilishajaribiwa kwenye tafiti za kitabibu na zimeonyesha usalama wake na kwa wakati huo huo, inapima aina mpya ya dawa kinga ya VVU (PrEP) dhidi ya dawa kinga ya VVU (PrEP) inayotumika sasa.

Utafiti uko wapi?

Utafiti huu unapangwa kufanyika kwenye vituo vitano katika nchi 4: Masaka, Uganda; Mbeya, Tanzania; Dar-es-Salaam, Tanzania; Maputo, Msumbiji na Durban, Afrika Kusini.

Chanjo ya VVU ni nini?

Chanjo inafundisha mwili kujikinga dhidi ya maambukizi fulani au kupigana na ugonjwa kwaajili ya kukuweka na afya njema. Dunia bado haina chanjo inayo kinga VVU iliyosajiliwa. Ili kutengeneza chanjo, watafiti wanahitaji kuipima kwa watu, ili kugundua kama itaweza kusaidia kukinga au kupigana na VVU. Inatolewa kwa sindano.

Dawa Kinga ya VVU ya Kumeza (Oral PrEP) ni nini?

Dawa Kinga ya VVU (PrEP) ni matumizi ya dawa za kufubaza VVU kwa watu wasio na maambukizi ya VVU ili kupunguza hatari yao ya kupata maambukizi ya VVU. Dawa Kinga ya VVU imeonyesha kuzuia VVU na inapatikana duniani kama kidonge.

Utatoa mchango gani kwa kushiriki?

Kuna njia nyingi za kuzuia VVU, ila kila mwaka maambukizi mapya yanaendelea kuripotiwa. Ushiriki wako na jitihada zako zitasaidia kujibu maswali mawili kwa taarifa ambazo zinaweza kusaidia kuzuia maambukizi mapya kwenye jamii yako.

• Tutaweza kusema iwapo utengenezwaji wa aidha ya mchanganyiko miwili ya chanjo ya kuzuia VVU inafaa au la

• Tutaweza kusema kama aina mpya ya dawa kinga ya VVU (PrEP) inakubalika, ni salama na ina ufanisi kama aina ya dawa kinga ya VVU ya kumeza inayotumika kwa hivi sasa na wanawake pamoja na wanaume

Wanawake na wanaume wenye umri wa miaka 18–40 wenye hatari ya kupata maambukizi ya VVU wanaalikwa kushiriki kwenye utafiti wa PrEPVacc.

Unaweza kushiriki kama:

• Una afya njema

• Una umri wa miaka 18–40 siku ya mchujo

• Una utayari na una uwezo wa kutoa ridhaa kushiriki kwenye utafiti huu

• Una utayari na unaweza kuja katika mahudhurio yote na kufanyiwa kipimo cha VVU na kutoa damu, mkojo na sampuli nyingine kwa wakati zinapohitajika

Afya na haki za washiriki zitalindwa vipi?

Wakati wote tutawapa washiriki taarifa kamili kuhusu utafiti kabla mshiriki hajajiunga kwenye utafiti, ili uweze kutupa ridhaa ya kushiriki.

Washiriki wana haki ya kujitoa kwenye utafiti wakati wowote.

Kipindi cha utafiti, wafanyakazi wa kliniki watawafuatilia washiriki ili kuhakikisha kwamba chanjo na dawa kinga dhidi ya VVU hazisababishi matatizo yoyote ya kiafya.

Wafanyakazi wa utafiti pia, watawasaidia washiriki kuripoti matatizo yoyote ya kijamii ambayo wanapata kutokana na kuwepo kwenye utafiti.

Usalama wa washiriki upo chini ya uangalizi wa timu inayofuatilia usalama na bodi ya kujitegemea ya ufuatiliaji wa usalama ambayo mara kwa mara huangalia taarifa za kiafya za washiriki na kuamua kama ni salama kuendelea na chanjo na dawa kinga ya VVU.

Kamati ya maadili ya kitaasisi inapitia na kufuatilia mpango wa utafiti kwa kila kituo kinachofanya utafiti huu, pamoja na taarifa inayotolewa kwa watu kuhusu utafiti huu, maendeleo ya utafiti, na matatizo ya kiafya ya washiriki. Kamati hii ya maadili pia huangalia kama haki za washiriki zinaheshimiwa.

Kila kliniki ya utafiti ina bodi ya ushauri wa jamii. Wajumbe wake ni watu wa mahali hapo hapo ambao wanashauri watafiti na kuleta wasiwasi na masilahi ya jamii na washiriki wa utafiti kwa watafiti.

Ni nani anapewa chanjo ... mtu asiye na virus au mwenye virus
Je lengo ni kujua kama virus vinakufa kwa hiyo dawa au virus havimpati aliyekunywa hiyo dawa
Je kama mtu akinywa dawa akaenda kupima nguvu ya virus na dawa isifanye kazi, atafidiwaje?
 
Ni nani anapewa chanjo ... mtu asiye na virus au mwenye virus
Je lengo ni kujua kama virus vinakufa kwa hiyo dawa au virus havimpati aliyekunywa hiyo dawa
Je kama mtu akinywa dawa akaenda kupima nguvu ya virus na dawa isifanye kazi, atafidiwaje?
Umesoma pdf hapo juu marxlups ? Maelezo yanajitosheleza !
 
Kabla ya kupinga utafiti huu wa PrEPVacc ni vema tujikumbushe historia za chanjo kama Polio, Ndui, Dondakoo, Pepopunda, Surua, Kifaduro, HPV kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa kubofya link chini
World Health Organization (WHO)​


1608749358129.png
 
Back
Top Bottom