Tanzania National Business Council (TNBC). Mbona maneno "Tanzania" na "National" yanafanana?

Tanzania National Business Council (TNBC). Mbona maneno "Tanzania" na "National" yanafanana?

Infantry Soldier

JF-Expert Member
Joined
Feb 18, 2012
Posts
15,892
Reaction score
16,476
Good evening jamiiforums

Mnamo mwaka 2018 mwezi wa August niliwahi kuhoji usahihi wa kisarufi katika matumizi ya maneno "Tanzania" na "National" katika kuunda jina la uwanja wa taifa kwa lugha ya kiingereza uliosomeka kama "Tanzania National Main Stadium" kwenye lango kuu.

gfghnbmklkio.jpg


Soma Hapa>>> Uwanja wa taifa kuandikwa "Tanzania National Main Stadium" ni sahihi katika sarufi(grammar) ya kiingereza?

Sijaenda uwanja wa taifa muda mrefu ila kulingana na maelezo ya rafiki zangu nasikia lile bango pale lango kuu limetolewa na sasa pameandikwa "Benjamin Mkapa Stadium".

Kama hii taarifa ni kweli basi wamefanya jambo la maana sana kwa maana hata Senegal wanao uwanja wa taifa unaoitwa "Léopold Sédar Senghor" jina la baba wa taifa lile.

Kulingana na maelezo ya wataalam wa lugha, maneno "Tanzania" na "National" hayapaswi kutumika pamoja kwa maana yana maana zinazoshabihiana.

Je ni sahihi kwa shirika la utangazaji la TBC kuitwa TNBC (Tanzania National Brodcasting Corporation) au lile la nyumba la NHC kuwa TNHC (Tanzania National Housing Corporation)?

Sasa wiki iliyopita nikiwa ninatazama taarifa ya habari ile ya saa moja ambayo wanaiita ARIDHIO ndio nikaja kukutana na hii ya "Tanzania National Business Council" (TNBC) ndio nikakumbuka kuwa haya ndio yale yale ya uwanja wa taifa ya kuchanganya maneno mawili yanayoshabihiana kwa maana.

images (2).jpg


Kwanini isingekuwa "Tanzania Business Council (TABC)" au "National Business Council (NABC)" kama ilivyo kwa TBC na NHC?

Mbona shirika la Utanganzaji sio TNBC na wala lile la nyumba haliitwi TNHC? Kuna nini kinaendelea hapa au mimi ndio mshamba wa lugha? Kama suala ni mfanano mbona TISS ya BOT inafanana na ile TISS ambayo ni idara ndani ya ofisi ya Rais na bank kuu hawawazi hata kubadili jina la huo mfumo ila maisha yanaendelea kama kawaida?

fgkilopo.jpg


USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
 
Tanzania National Stadium ni Uwanja wa Taifa wa Tanzania. Na

Tanzania National Business Council ni Baraza la Biashara la Taifa la Tanzania/ Baraza la Taifa la Biashara Tanzania. Wameongeza neno Tanzania kuwa Specific zaidi. Wakiacha tu la Taifa kuna Mataifa mengi.
 
Tanzania National Stadium ni Uwanja wa Taifa wa Tanzania. Na

Tanzania National Business Council ni Baraza la Biashara la Taifa la Tanzania. Wameongeza neno Tanzania kuwa Specific zaidi. Wakiacha tu la Taifa kuna Mataifa mengi.
Asante kwa hoja yako nzuri mkuu. Sasa vp kuhusu TBC na NHC?
 
Asante kwa hoja yako nzuri mkuu. Sasa vp kuhusu TBC na NHC?
Tbc tayari kuna Tanzania. NHC Shirika la nyumba la Taifa nadhani hawakuona haja ya kuweka Tanzania sababu nyumba dont Move ni za humu humu ndani. But tbc inasikika nje ya nchi pia. So T inatambulisha nchi husika. Kama BBC,KBC,UBC,ZBC n.k
 
Kumbe ndio mana kuna BBC - British Broadcasting Corporation na sio BNBC- British National Broadcasting Corporation

Dah...! Tungetumia tu kiswahili chetu kwenye haya makampuni kukikuza kiswahili.
 
NHC Shirika la nyumba la Taifa nadhani hawakuona haja ya kuweka Tanzania sababu nyumba dont Move ni za humu humu ndani.
Hahahahahaaaa daaah ila wee jamaa justifications zako huwa zinaniachaga hoi sana. Sasa mbona boss mkuu wa NHC huwa ana move na kwenda Ulaya kikazi? Au akifika huko ndio anasema kuwa yeye ni boss wa TNHC na sio NHC tena?
 
Hahahahahaaaa daaah ila wee jamaa justifications zako huwa zinaniachaga hoi sana. Sasa mbona boss mkuu wa NHC huwa ana move na kwenda Ulaya kikazi? Au akifika huko ndio anasema kuwa yeye ni boss wa TNHC na sio NHC tena?
Huko NHC si ya Kimataifa. Akienda anaenda kwa issues zake ni sawa na kuwa na dawasa/dawasco siyo kwamba wakurugenzi hawa hawasafiri nje ya mikoa yao.
 
Huko NHC si ya Kimataifa. Akienda anaenda kwa issues zake ni sawa na kuwa na dawasa/dawasco siyo kwamba wakurugenzi hawa hawasafiri nje ya mikoa yao.
Mkuu, nimekuuliza swali comment yangu #8 ila umelikwepa mzee baba.
 
Hapana, National na nation ni vitu viwili tofauti kwa mantiki kwamba nation ni taifa na national ni la taifa, kwa maana hiyo sasa ni kuwa kuweka national na pia Tanzania ni kuonesha kuwa hilo shirika lipo Tanzania na si kwingine. Baraza la biashara la taifa la Tanzania. Over
 
Hapana, National na nation ni vitu viwili tofauti kwa mantiki kwamba nation ni taifa na national ni la taifa, kwa maana hiyo sasa ni kuwa kuweka national na pia Tanzania ni kuonesha kuwa hilo shirika lipo Tanzania na si kwingine. Baraza la biashara la taifa la Tanzania. Over
Vp kuhusu TBC? Haikustahili kuwa shirika la utangazaji la taifa la Tanzania (TNBC)?
 
Back
Top Bottom