Tanzania National Identities (Vitambulisho vya Taifa)

Tanzania National Identities (Vitambulisho vya Taifa)

Simple test. Ningekuwepo pale kwenye maandamano leo ningejidai mimi ni mwandishi wa habari halafu niwaulize waandamanaji ni kitu gani cha muhimu walichosikia kwenye hotuba ya rais ambacho kimewasisimua kiasi ya kuandamana?
 
Hivi kuna habari kama polisi iliarifiwa na kuruhusu maandamano hayo ? Maana kumekuwa na mtindo ambao si wakawaida kwa Polisi kutangaza habari za maandamano ya vyuma vya upinzani ,utawasikia wanafikiria ,wameruhusu halafu utasikia wameandika barua kuzuia mpaka itakapotolewa taarifa nyengine.
Wapinzani mupo ? mambo kama haya ni lazima muyachungue na kupata uthibitisho kuwa CCM waliandika barua kuomba kibali au kuiarifu polisi ,maana hi nchi si ya CCM peke yao wafanye watakavyo bungeni na huku mitaani mambu ni hayo hayo.


Hili ni muhimu kuliangalia kwa udnani kwa sababu kuna uwezekano maandamano haya yamefanyika kienyeji mno. Yamekuwa ya ghafla sana. Hivi watu wakiomba kuandamana kupinga hotuba ya muunwgana wanaweza kuruhusiwa haraka haraka namna
hii?


Raisi Kikwete amezuia maandamano yaliyoitishwa na TUCTA. Asema mgomo wa wafanyakazi ni batili. Ninachokiona ni kwamba anaafiki na kukubali kwamba wafanyakazi wanayo madai ya msingi. Chenye dosari ni wao kuto-kutoa notisi siku 60 kabla ya mgomo.




Mimi sishangazwi wala nino maana ndio demokrasia lol....mkipinga wenzenu wanaunga mkono....!! Mwendo mdundo.



Huenda vyama mbadala na taasisi za kijamii zinaandaa maandamano kupongeza hotuba ya Spika Sitta.




.
 
Maandamano hayo nadhani yalikuwa ya kukubaliana kuwa endapo kama ni kweli pesa hizo zimerudishwa. Basi zipewe wananchi husasan kilimo.

Lakini sidhani kama ni kweli eti hotuba yote imepongezwa. Hapo ni upotoshaji wa wazi. Hizo pesa anazodai ziende kwenye kilimo na wakati ni wapinzani waliotoboa SIRI ya pesa hizo walizokwisha gawana. Halafu then wanawageuka wapinzani kiasi hicho ni jambo la kisikitisha sana kama ni kweli kuna demokrasia.

Hao waliyoyaweka madhambi hayo wazi na wao ni wa kupewa nafasi ya kutoa mchango wao kwenye issue nzima. Maana wananchi na wao waelewe kuwa kama haikuwa kwa wapinzani basi hata hizo pesa wasingeziona!
 
Kama wanaanchi wanaandama kumpongeza JK, hiyo ni dalili tosha kwamba somo letu hapa JF halitoshi kabisa. Wakati sisi tunaenda mwezini, CCM wanaenda kwa wananchi.

Pia ni makosa kuwalaumu CCM kuaandaa hayo maandamano, wa kulaumiwa hapo ni sisi wenyewe ambao tunashindwa kufikisha hoja zetu kwa wananchi. Na pia hao wananchi ambao pamoja na hali ngumu, ufisadi na dhuluma zingine bado wanapoteza muda wao kwenda kwenye maandamano ya kumuunga mkono msanii.
 
Ni maandamano ya Chama Chake yakiunga mkono mkubwa wao ,si ya Kiuwananchi wakiunga mkono Hatuba ya Raisi wao.

Natumai ipo tofauti ,cha muhimu ni taratibu zinazokubalika kwa Vyama vyote kufanya maandamano Je zilifuatwa na Chama cha CCM nafikiri kulichunguza suala hili linahitaji wanasheria wa vyama pinzani na mawakili wao.

Je vyama vya upinzani vinaweza kwa upande wao kupinga aliyoyazungumza Mh.Kikwete?
Je wananchi wa Tanzania wanaweza kuandaa maandamano kupinga hayo hayo mazungumzo bila ya kupitia vyama vya siasa ?
 
Kweli hii njaa itamaliza watu wetu pamoja na nchi yetu......yani ripoti pumba vile lakini bado watu wanaipongeza?? duh!! kweli mitanzania ndivyo tulivyo..!
 
Kama wanaanchi wanaandama kumpongeza JK, hiyo ni dalili tosha kwamba somo letu hapa JF halitoshi kabisa. Wakati sisi tunaenda mwezini, CCM wanaenda kwa wananchi.

Pia ni makosa kuwalaumu CCM kuaandaa hayo maandamano, wa kulaumiwa hapo ni sisi wenyewe ambao tunashindwa kufikisha hoja zetu kwa wananchi. Na pia hao wananchi ambao pamoja na hali ngumu, ufisadi na dhuluma zingine bado wanapoteza muda wao kwenda kwenye maandamano ya kumuunga mkono msanii.

Kwani hujawahi kusikia madai kwamba watu weusi wana akili pungufu kuliko wengine? Sijui ukweli wa madai hayo, ila inaonekana kuna matatizo fulani katika fikra za binadamu-nyani.
 
Kazi ni kubwa sana tuliyo nayo. Kadri siku hizi zinavyoenda ubaya wa hotuba ya JK unabadilika kutoka ya ovyo kuwa mbaya, ya kawaida na hatimaye itafaika mahala itaonekana kuwa ilikuwa nzuri, hasa watakapomaliza kuijadili wabunge.

Naambiwa wabunge wa CCM wamejipanga kuimwagia sifa hotuba hii kuanzia aya ya kwanza hadi ya mwisho.

Na wameambiwa yeyote atakayejifanya kuikandia, 2010 ataula wachuya, na majamaa, kwa kuwa hayana ujasiri, yamenywea nywee!
 
Wabunge hawatajadili tena hii hotuba kwani kwa mujibu wa Spika alisema kuwa imepelekwa Ikulu kwa ajili ya kuhaririwa kabla ya kuchapwa na kusambazwa kwa wabunge, na hivyo wataweza kuijadili bunge la mwezi November.
 
Ule mpango wa kuijadili hotuba ya Kikwete Bungeni umezimwa. taarifa kutoka huko, zilizothibitishwa na Spika Sitta, zinaeleza kuwa mjadala wa hotuba hiyo hautakuwepo hivi sasa, labda katika bunge la Novemba.

Taarifa ni kuwa mjadala huo umefutwa kwa sababu hotuba ya rais hadi hivi sasa bado haijakamilika. Alisema maneno mengi wakati wa hotuba ambayo yapo nje ya hotuba yake iliyokuwa imeandikwa.

Imeshindikana kuingiza hayo maneno mengine kwenye hotuba na kuwahi kutengeneza vitabu vya hotuba ambavyo vingegawiwa kwa wabunge
 
Ni kweli hata mimi nilimsikia Spika akisema kuwa vitabu vimepelekwa Ikulu kwa ajili ya kufanyiwa uhariri sasa uhariri wanini kama Hansard walirekodi?si hata TV walitoa live na wengine kuirudia usiku?hapa maji yamezidi unga sasa ugali utaiva? na uji haunyweki kwani watu walilala njaa......
 
Ule mpango wa kuijadili hotuba ya Kikwete Bungeni umezimwa. taarifa kutoka huko, zilizothibitishwa na Spika Sitta, zinaeleza kuwa mjadala wa hotuba hiyo hautakuwepo hivi sasa, labda katika bunge la Novemba.
Taarifa ni kuwa mjadala huo umefutwa kwa sababu hotuba ya rais hadi hivi sasa bado haijakamilika. Alisema maneno mengi wakati wa hotuba ambayo yapo nje ya hotuba yake iliyokuwa imeandikwa. Imeshindikana kuingiza hayo maneno mengine kwenye hotuba na kuwahi kutengeneza vitabu vya hotuba ambavyo vingegawiwa kwa wabunge

Huo ni usanii. Hansard ni kazi ya siku moja tu.. Hotuba zote za jana pamoja na maswali na majibu viko tayari, kwanini hotuba ya Rais kama ingetakiwa watu wangekesha kufanya kazi na kuikamilisha. Taarifa ni kwamba inapelekwa Ikulu "kufanyiwa ukarabati" kwanza maana inawezekana kuna maeneo aliteleza kutokana na ile mashine ya kusomea kuleta matatizo na hivyo kumfanya aanze kuhangaika na makaratasi ndio maana hata mtiririko ukapotea akawa kama katika mkutano wa hadhara. Hata speech hazikugaiwa kwa waandishi kama kawaida tena hadi leo (japo ninayo).

Kimsingi ni kwamba sababu ya kuahirishwa mjadala ni kwamba kumeibuka sintofahamu kati ya Bunge na serikali na kauli ya spika imeongeza chumvi katika kidonda, na uamuzi wa kujadili hotuba nao umezidisha kabisa tatizo, lakini wakienda kuikarabati hotuba, haitakubalika maana hansard ni kama msahafu huwezi kuubadili kienyeji.
 
Ni kweli hata mimi nilimsikia Spika akisema kuwa vitabu vimepelekwa Ikulu kwa ajili ya kufanyiwa uhariri sasa uhariri wanini kama Hansard walirekodi?si hata TV walitoa live na wengine kuirudia usiku?hapa maji yamezidi unga sasa ugali utaiva? na uji haunyweki kwani watu walilala njaa......

Kazi za kulipua,kigugumizi au ni mpamgo mahsusi wa kuzima mjadala kuwa pesa za EPA wanaopaswa kuzigawa ni wabunge sio Kingunge
 
Viongozi wa CCM ni wapumbavu wa kwanza duniani!!! Ni mpaka lini wataendelea kufikiria kuwa njia ya kutatua tatizo ni kutolizungumzia/ku_assume halipo wakati lipo?

CCM isikwepe kutekeleza majukumu yake na badala yake ijaribu kuwaonyesha eti watu wanaozungumzia matatizo yaliyopo ni wakosaji wa adabu. Mtu kukiri kuwa una tatizo fulani ndio hatua ya kwanza ya kuelekea kwenye uvumbuzi.

Hii Kikwetemania au Rostamanian iliyoingia Tanzania ya sasa ya kufanya mambo kisanii itakuja tutokea puani Watanzania siku moja!!!!
 
Hata kama ni kujadili watajadili nini tena pale? Tuliyekuwa tunamtegemea ameongea kimzaha mzaha. Na kwa hao wa kujadili itakuwa zidumu fikra......
 
Kwani hujawahi kusikia madai kwamba watu weusi wana akili pungufu kuliko wengine? Sijui ukweli wa madai hayo, ila inaonekana kuna matatizo fulani katika fikra za binadamu-nyani.


Mkubwa hata wewe ni wa kusema haya?
 
JK na magumashi ataacha lini ? Usanii gani huu wa kumtia aibu jamani ?
 
Alisema pesa za EPA zipelekwe kwa wakulima kupitia TIB......tatizo litakuja kwenye accessibility ya wakulima hao kwenye hizo pesa (bond problems).....kitakachotokea.........ni mafisadi wale wale kwa kofia ya ukulima ndio watakao access kwa haraka zaidi......its good window of opportunity to the same mafisadi..............

Nadhani the best way ilikuwa ni kusaidia Vyama vya ushirika (kama bado vina-exist)direct
 
Kwani hamjui kuwa kampuni lililojichotea bilioni 40 kati ya hizo linaitwa Kagoda Agricultural LTD?

Huenda sasa Kagoda itaanza kujihusisha na kilimo rasmi tutajuaje?
 
Back
Top Bottom