Tanzania National Identities (Vitambulisho vya Taifa)

Tanzania National Identities (Vitambulisho vya Taifa)

Najaribu kupata nakala niisome vizuri, kwani kuna mambo yanahitaji kutafakari kidogo.

Hotuba hii imejaa data nyingi za kiuchumi ambazo ni economic indicaters muhimu, naimani approach hii ni nzuri na viongozi wengine wataiga, mfano aliposema dept/gdp ratio yetu sasa ni 25% ukilinganisha na 90% mwaka 2005 hii nidata muhimu kwa mwanauchumi makini.

Nimefurahishwa na approach ya kuanza kuukataa umaskini kwa kukataa kurudi HIPC, jambo hili jamani hebu tulipongeze.

Kuna hili la Imported inflation nadhani hapa anahitaki kwenda deep kidogo, mfano kitasa cha yale/union kimeuzwa shs 17,000/= tangu 2005 hadi leo bei ni hiyo hiyo. kigae cha spain 1' x 1' kimeuzwa shs 1200/= hadi leo. sealing board ya SA imepanda kutoka 9500/= hadi 12000/= ongezeko hili inawezekana nikutokana na kupanda kwa gharama za usafirishaji.

Hebu tuangalie locally produced goods katika soko la kamachumu, mchele umepanda kutoka shs 180/= mwaka 2005 hadi 1400/= todate, saruji imepanda kutoka 9800/= hadi 25,000/=, sukari kutoka 380/= hadi 1800/= vyote hivi has nothing to do with imported inflation.

Suala la diesel; iweje diesel kigali iuzwe franc 770 (= tshs 1400) na dar diesel iuzwe tshs2000! wakati rwanda wanapitishia diesel bandari ya dar!

Amesema alipofika Dodoma university alishangaa kweli, naimani alishangazwa na ujenzi uliomahili na sio uzuri wa students wanaosoma pale.

..ni kweli kwamba hizo data zinavutia. lakini, unafikiri zina maana yeyote kwa mwananchi wa kawaida, ambaye anapata tabu ya kula mlo wa kutosha kwa sababu bei za bidhaa zimepanda sana?

..hizo data kama unawahutubia wataalamu au wasomi zinakuwa zimefika kwa walengwa. lakini, kama unahutubia wananchi utakuwa kama unapigia mbuzi gitaa. wananchi wanataka majibu ya shija zao na si takwimu. ukisema uchumi umekuwa, basi na useme umesambaza maji vijijini, umejenga barabara,na zahanati vijijini zimepata dawa na hii iwe kweli na si iwe imepikwa kwenye data za wizara.

..pia, ajira za kweli ziwe zimetengenezwa vijijini na mijini. wakulima wawe wamepata mbolea na mbegu.

..hayo mambo ya hipc yana kazi kubwa. kwani tunakusanya kiasi gani cha mapato na tunatumia kiasi gani?. halafu, kama ndio tuko kwenye mkao wa kukopeka, je hiyo haiwezi kuturudisha kule kwenye madeni makubwa?. kumbuka, watu wa magharibi wanapenda tuwe tunadaiwa daima.
 
Kama ndiyo haya anayotaka kuzungumzia kweli
Je tukimwita ZeCommedy kuna tatizo
Hivi huyu President kwa akili yake nyepesi tu amabzo hakuna hata mtanzania mmoja ambaye hizo statistics hazimuingii hakilini yeye inakuwaje akubali jamani??

Lakini kwa Rais Kikwete sishangai mambo yake
Maana aliagiza kamati aliyounda kuchukua hatua za kisheria na pesa zirudishe, wao wakaja na riport vitu viwili tofauti na akapokea

Report yenyewe hata hajaisoma na kuona ndani yake kuna nini, anawapongeza kwa kazi ngumu na nzuri sana walioifanya

Hivyo kwa mtu kama huyu kwenda kuliutubia Bunge na watanzania wote kwa kupmba kama hizo si ajabu ndugu!!

anyway simkubali hata kidogo na nina mengi sana ya kumuelezea huyu mtu
tusubili hiyo kesho
mimi nawaomba wana JF wore tuwe na subira tusikate tamaa kwasababu MH: ameshalitupia bunge: tusikilize kuwa bunge litatoa maaqmuzi gani:SIMNAJUA KUWA WENGI WANAOTUHUMIWA NI BESTI ZAKE SASA SI RAHISI AWAHUKUMU YEYE NADHANI NDO MAA NA ANAJARIBU KUKWEPA NA KULISUKUMIA BUNGE: WATAKAVO AMUA YEYE ASAIN TU. ITAKUWA SI YEYE ALIE WAHUKUMU ILA NI BUNGE. HUYU BWANA TEKNIKI ANAYOTAKA KUCHEZA HAPA NI KIALI ILA NAWASIHI TUSICHOKE KUSUBIRI.
 
Ila huyu Kikwete na Bunge lake hajavunja rekodi mpya ya dunia ambayo iliwekwa Na Mhafidhina Karume aliewaita waandishi kisha yeye akaingia mitini na kuwaachia tape iwasomee aliyowaitia na waandishi haijulikani kama waliridhika au hawakuridhika ,ila waliandika wamekwenda Ikulu ya Zanzibar kukutana na Rais.

Sasa hawa waandishi waliokwenda Bungeni kusikiliza hotuba ya Kikwete haijulikani kama walisikiliza hotuba au mazungumzo?

Hadi leo hakuna hotuba kuna alichozungumza ila magazeti wanaandika Hotuba ya Kikwete imejaa changamoto ukiwauliza iko wapi ,mnayo copy ,jibu hawana.
 
Kuna mtu ametamba kuwa Hotuba ilisema bei ya kitasa cha kuagizwa cha Yale haijabadilika tangu 2005, lakini bei ya mchele ambao ni chakula imepanda marudufu.

Hivi kwa yeyote mwenye akili timamu, kipi ni cha muhimu na maana kwanza, mchele au kitasa kutoka ulaya? kipi kina manufaa ya lazima na muhimu kwa mwananchi, Mchele au kitasa cha kuagizwa cha Yale?

Mambo mengine tunafanya na kuzungumza bila kufikiri! Mchele umepanda bei kiasi cha kutisha na kutishia uhai wa nchi kwa watu kushindwa kununua chakula, lakini tunajitapa eti kutumia vigezo vya uchumi kuwa uchumi wetu ni imara kwa kuwa bei ya kitasa cha kutoka ulaya haijabadilika kwa miaka 3?

Kama kauli hiyo ni ya mchumi, sijali iwe ni suala la inflation au nini, mchumi huyu na kiongozi huyu ajiulize, kwa hali ya umasikini ilivyo na jinsi wananchi wanataabika kujilisha ili wazalishe mali, leo tunadiriki kujigamba kuwa eti pamoja na hali ngumu ya uchumi, bei ya kitasa kutoka ulaya madukani haijabadilika?

I tell you we have wrong people in our leadership and so is the so called technocrats!
 
Tabu watu wanaosema hotuba mbaya wanataka kuchafua nchi tu sasa mnataka angeenda anza kutoa namba za gerezani wapewe wezi wa EPA. Hizo hela mmeshaambiwa sio za serikali, Serikali zimeziweka chini yake sasa hivi. Hizo hela hata watu wa JF mngeweza kuzipata mkengiztaka

Kikwete kawanyamazisha sana kwani Ushindi 2010 pale pale. Na kina slaa wakiongea zaidi kashawapa warning in a joking way so pole wana JF tafuteni lingine.

Sizzla,

Ulichoongea hapa si Ujinga tu, bali ni Upumbavu wa hali ya juu!

Kmaa unachoongelea hapa na ndio nguzo na mhimili wa Serikali katika kesi hii ya Uhujumu ni kusema kwa kuwa pesa si za Serikali basi ni ruksa kuiba, ina maanisha kuwa hakuna maana ya kuwa na sheria, kila mtu ana haki kuiba, kudhulumu na kunyanganya mali isiyo ya Serikali.

Sasa jiulize, maana ya Serikali ni nini? Serikali ni watu, kama tutaesma mali ya Watu ni huru kuibiwa, basi naja nyumbani kwako kukuibia hata kukutoa roho maana weye ni Serikali na sitafunguliwa mashitaka!
 
HUKO MTAANI KUNA TOLEO MAALUM LA RAI. MKUMBUKE KUWA RAI INATOKA ALHAMISI. LAKINI LEO WAMEJIMWAGA MTAANI KAMA TOLEO MAALUM. LIMESHEHEINI UPPUZI MARA OH KIKWETE MWISHO;

sasaa ndo watu tumemjua rostam azizi

tukumbuke maneneo ya dr mwakyembe bungeni- WATANZANIA SASA SIYO MABWEGE

BILA SHAKA SASA MABWEGE NI ROSTAM. NA WAANDISHI WAKE WOTE WA RAI; MTANZANIA; NK KAYIKA LIST YA MABWEGE ATAKUWEMO MHARIRI MKUU BALILE KWA KUWA AMESAHAU KUWA PROPAGANDA ZAKE NA ROSTAM ZINZWEZAKANA TU KWA WAPIGA DEBE KAMA WALE WANAOSHINDA KWENYE JUA KALI PALE MOROGORO WAKISIFIA MAGARI YA HOOD; NA ABOOD

KWA WATANZANIA WA LEO ROSTAM NA AKINA BALILE WANAOTA NDOTO ZA ALINACHA
 
War against grand corruption: Govt should get much tougher - Speaker Sitta

-Delivers blunt rejoinder to presidential address

THISDAY REPORTER
Dodoma

THE Speaker of the National Assembly, Samwel Sitta, yesterday urged President Jakaya Kikwete to adopt a tougher approach in dealing with serious allegations of grand corruption in the country, saying there should be no let-up in the fight against graft.

Giving a vote of thanks on behalf of members of parliament as a whole after the president's marathon address to the House, Speaker Sitta delivered a blunt message; ''The government must become extra-brutal in tackling high-level corruption in the corridors of power''.

''It appears that more importance is being placed on individual rights than national interests. There is no such thing as the human rights of an individual involved in economic sabotage being violated,'' he said.

The Speaker noted that some countries in South-East Asia had succeeded in making more progress in economic development by tackling corruption upfront and with an iron fist.

He stressed that the individual rights of people responsible for the massive looting of public funds are of little importance in the fight against grand corruption.

Citing various grand corruption scandals such as the external payment arrears (EPA) account embezzlement at the Bank of Tanzania, the Commodity Import Support (CIS) scam, and the purchase of an overpriced military radar system, the Speaker said lawmakers in the current Parliament are likely to become even more insistent in demanding government action.

''These allegations may appear quite difficult to tackle because of the various loopholes in government procedures, regulations and legislation. But they are all within our (parliamentary) jurisdiction to deal with,'' he said in his frank rejoinder to President Kikwete's speech.

''If you (Mr President) were to become a little more strict in these issues, we (MPs) are ready to support you in this,'' he added, asserting that the House is anxious to see President Kikwete's government tackling corruption with unyielding resolve.

According to Speaker Sitta, the ordinary man or woman in the street would find it hard to comprehend if individuals known to be behind the massive looting of billions of shillings in public funds are ultimately allowed to walk away scot-free.

He said Parliament is at the full disposal of the government to enact tough, new legislation that gives relevant authorities more teeth to tackle corruption allegations in the higher echelons of public leadership.

He said despite good progress made by the Kikwete administration in enhancing good governance and the rule of law, serious flaws still exist in the implementation of many government promises.

''Promises made by the government inside and outside Parliament are not always kept as a result of the weaknesses of some government officials,'' the Speaker stated, warning that some government officials may be deliberately delaying implementation of important decisions.

On the fate of the ongoing debate on the Union and the shaky Zanzibar political reconciliation (Muafaka) talks, he said more seriousness is needed to tackle this problem.

''It is our hope that this problem will be fully resolved by the government before the year 2010,'' he said, apparently referring to the next general elections.

Meanwhile, reacting to yesterday's presidential address, the Leader of the Official Opposition in the National Assembly, Hamad Rashid Mohamed (Wawi-CUF), said the speech had touched on the main concerns of Tanzanians today.

He said the wananchi are now waiting to see how the various pledges made by President Kikwete in his speech will be implemented.

Hamad Rashid especially called on President Kikwete to address the problem of the stalled Muafaka talks sooner rather than later, in order to prevent a further deterioration of the political situation in Zanzibar.

However, Kigoma North MP Zitto Kabwe (CHADEMA) expressed reservations about the president's comments regarding the EPA embezzlement scandal.

''For example, he did not exactly say what action will be taken against the EPA suspects after they return the (stolen) money,'' noted Zitto.

He added: ''If there is to be a presidential pardon or amnesty to the EPA suspects, proper procedures should be followed and Parliament must be officially notified about this decision.''
 
Maskini papasi, huuzwa na mbwa wake!Tulidhani wamebadilika kumbe bado ni vibaraka wa muungwana,kweli sikio la kufa halisikii dwa.
 
Maskini papasi, huuzwa na mbwa wake!Tulidhani wamebadilika kumbe bado ni vibaraka wa muungwana,kweli sikio la kufa halisikii dwa.

Rai ni RA na RA ni EPA = JK na CCM yao .Kuna la kushangaa hapa jamani ?
 
.......Mimi kama Rais nina mamlaka makubwa ninao uwezo wa kusema kamata Slaa........ Mwema atakwenda kumkamata bila kuniuliza kwanini nimetoa amri ya kumkamata. Baadaye ndipo atakuja ...Sasa Mzee yule mtu yuko ndani tumfungulie mashitaka gani. Nami nikasema mwache akae kwanza..."

Huu ni ushahidi wa wazi kuwa kwa mujibu wa katiba, rais wetu ni dikteta. hatuitaki katiba ya aina hiyo hasa wakati huu tunapojidai kuwa nchi yetu ni ya kidemokrasia. Kwa kauli hii, Rais mwenyewe amethibitisha kuwa tunahitaji katiba mpya yenye kujali haki za watu
 
mimi nilikuwa najiuliza hivi leo ni alhamisi rai linapendwa hivyo likae mpaka leo kumbe ni toleo maalumu ? siku ya leo nimesoma mwananchi na the guardian tu
 
RAI ni Rostam Aziz na hiyo i baada ya z, hana jioya huyu fisadi Watanzania wengi tumekwishamshtukia.
 
rostam usijali wewe ni muwekezaji mzalendo hupeleki mali nje kama chenge tutakuunga mkono mpaka anguko lako na mwishi
 
Sizzla,Rev.Kishoka,BMK,Mpita Njia,

..hivi baada ya Raisi kutamka fedha za EPA siyo za serikali, je ameeleza fedha hizo ni za nani?

..halafu inakuwaje sasa anaamua kuzitumbukiza ktk mfuko wa pembejeo kusaidia wakulima?
 
Kishoka, naona haukunielewa. Mie nimezungumzia kipengele cha Imported Inflation pekee.

Nimesema bidhaa zilizokuwa-imported kama finished goods hazikupanda bei sana, nakama zilipanda ilisababishwa na kuongezeka kwa haulage cost. Ila zile locally produced/manufactured kama mchele sukari na saruji zilipanda bei mno, maana yangu nikuwa ile single digit inflationary rate indicator sio sahihi sana.

Kuna suala la strategical trading na strategical business hapo nimempa bigup. kwenye kubuni agricultural financing na micro agroeconomic support amekuja na wazo zuri ila tunahitaji critical thinkers ili wazo hili liweze kutekelezeka, sidhani kama Dr.David Mathayo anauwezo wa kuimpliment hizi ideas.

Kuhusu EPA nadhani hatukumwelewa nikuwa Gavana ambaye alikuwa next subordinate kwake kishamtimua, nawengine nao watekeleze wajibu wao. Hapa nisuala tu la collective responsibility.
 
Jamani EPA hizi ni outstanding LC! ambao hamjaelewa semeni tufungue darasa.
 
Sizzla,Rev.Kishoka,BMK,Mpita Njia,

..hivi baada ya Raisi kutamka fedha za EPA siyo za serikali, je ameeleza fedha hizo ni za nani?

..halafu inakuwaje sasa anaamua kuzitumbukiza ktk mfuko wa pembejeo kusaidia wakulima?

This is the real Question! Sina hakika kama anajua maana ya Serikali. Au anadanganya moja kwa moja. Pengine uanzishe Thread mpya kabisa, kuuliza hili swali la msingi kabisa.
 
Back
Top Bottom