Tanzania Nchi 1 ya JMT, Zanzibar Kujiita Nchi, Sio Uhaini?. Zanzibar Iadabishwe Kuondoa Ubatili wa Katiba Yake ili Tuitambue au Tumchelee Mwana Kulia?

Mdugu yangu P najua upo ccm lakini huwa mtu wa kufundisha toa maoni na yenye tija japo sio yote kwa upande wangu , nikupongeze kwa yale huwa tija kwa upande wangu . Nami nakuuliza why Zanzibar wasikae kivyao na Tanganyika kaa kivyake , Zanzibar hawezi kuwa na chokochoko ,wakilianzisha tunamiliki kisiwa kama Watanganyika ,uwezo upo .
So kama ndivyo kwa nini wazanzibar wasipewe mamlaka kamili ya nchi yao
 
Wizara ya katiba na Sheria inasemaje kuhusu mkanganyiko huo kama upo? Haya sasa kama katiba ya Jamhuri ya muungano ikivunjwa basi katiba ya Zanzibar ni batili? Duh tuangalie Sheria mama ambayo ni Katiba ya Jamhuri ya muungano.
 
Kaka Paskali
Hoja nzito sana hii.
Natamani huu mjadala uwe live kwenye media au stream yeyote.

Swali gumu kwa hoja ngumu
 
Mkuu Pasco,

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndiyo sheria kuu ya nchi. Ibara ya 64(5) inasema wazi, "Iwapo sheria yoyote iliyotungwa na Bunge au chombo kingine chochote itakuwa kinyume cha Katiba hii, basi sheria hiyo itakuwa batili kwa kadiri ya ukinzani huo."

Kwa msingi huo, vipengele vyovyote vya Katiba ya Zanzibar vinavyopingana na Katiba ya JMT ni batili kisheria, bila kujali vimetungwa kwa nia njema kiasi gani.

Ibara ya 64(1) ya Katiba ya JMT inaeleza wazi kuwa, "Bunge la Jamhuri ya Muungano ndilo lenye mamlaka ya kutunga sheria kwa ajili ya Jamhuri ya Muungano." Hii ina maana kuwa, Bunge la JMT ndilo lenye mamlaka ya mwisho kuhusu sheria zinazohusu Muungano, na si Baraza la Wawakilishi la Zanzibar.

Ibara ya 1 na 2 za Katiba ya JMT zinaeleza wazi kuwa Tanzania ni nchi moja na Jamhuri ya Muungano. Eneo la Jamhuri ya Muungano ni pamoja na Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar. Kwa hiyo, kisheria, Zanzibar si nchi huru, bali ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hata yule mbunge kipindi anasema watanganyika waingie Zanzibar kwa passport aliongea pasipokujua sheria zinasemaje
 
Hakuna namna wanasheria wa Tanganyika wanaweza kutusaidia kuondoa huu mtanziko?
Mtanziko utaisha kama Rasimu ya Katiba ya Mzee Warioba ikirudi Mezani kwa ajili ya kutekelezwa !!

Mtu aseme eti Nchi ni moja lakini wakati huo huo anakubali kuwa wapo maRais wawili 😂😅. !
 
Wanasubiri wachume kwanza kwa kutumia mtu wao waliyemtuma kutawala Tanganyika, halafu ndipo waitumie katiba yao ipasavyo.

Haitachukuwa hata mwaka baada ya mtu wao kutoka madarakani watapaza sauti kuwa Zanzibar ni nchi kamili na hivyo inataka mamlaka kamili.
 
Zanzibar ni Nchi ndogo ndani ya nchi iitwayo TANZANIA
Zanzibar siyo nchi kwa mujibu wa katiba yetu. Lakini Zanzibar haijulikani kama ni mkoa wenye mikoa, ni shirikisho kwani shirikisho lazima lazima liwe na pande mbili au zaidi .
hitimisho langu zanzibar ni mkoa kama njombe na katavi.
 
Zanzibar siyo nchi kwa mujibu wa katiba yet. Lakini Zanzibar haijulikani kama ni mkoa wenye mikoa, ni shirikisho kwani shirikisho lazima lamina like na pande mbili na si moja
Ni sawa tu na mke ndani ya NDOA kuwaambia rafiki zake kuwa hii ni nyumba yangu.
 
Kwanza Muungano wenyewe muundo wake hauleweki toka unaasisiwa na isitoshe Zanzibar wameshachoka na huo Muungano japo nao hawana ujasiri wa kutamka bayana.
Lakini ni Tanganyika ndiyo tunalazimisha kwa hoja za kipuuzi eti maadui wanaweza kuitumia Zanzibar!
Sasa tujiulize leo hii wababe wa kivita wakiamua kutuvamia na kutupa kichapo tunao ubavu wa kupambana nao?
Angalia leo hii kwa upumbavu wetu tunatawaliwa na Zanzibar halafu wenyewe tunakenua meno tu na kujigeuza kuwa chawa wa Mkoloni! Hivi kina Nyerere wakati huo wangeamua kuwa chawa wa Malkia ili mradi tu wateuliwe kwenye nafasi za uongozi uhuru ungepatikana?
 
Kikwete ndiye aliyharibu mchakato
Kwa kuwa alikuwa ni mwenye kiti wa CCM hawezi akakwepa uharibifu uliotokea kwa kuwa ndiye alitwishwa zigo la mwisho kwenda kuharibu mchakato mzima wa katiba.

Lakini ni Kikwete huyohuyo ndiye aliyethubutu kukubali kuwapa watanzania katiba mpya,ni Kikwete huyohuyo ndiye aliyewambia wana CCM wenzake wajiandae kisaikolojia kupokea serekali 3 akimaanisha kuwa yeye alikuwa amekubaliana na maoni ya wananchi kuwa serekali 3 haziepukiki,tatizo likaja kwa wale tutaishije kama tutakubali katiba mpya,mmoja wapo alikuwa ni Magufuli ambaye alisema kavukavu kuwa mimi sikuahidi katiba mpya.
 
Sasa Kuna tatizo mtu kudai chake?
 
Hujui lolote
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…