Sijasoma Civics mimi sisi tulikuwa na soma linaitwa Siasa.......Huyo ni Mtanzania halisi udenimark wake ni kwenye taratibu za kwenye makaratasi
You are right and i was wrong mkuu, ni kweli kutokana na taratibu za nchi yetu the guy anasifa za kuwa mtanzania na ni mtanzania the rest ni siasa za kwenye makaratasi as you said mkuu.
Baada ya kupitia maandiko ya nchi yetu na haya ndio niliyoyapata.
URAIA WA TANZANIA
Masuala ya uraia nchini Tanzania yanasimamiwa na Sheria ya Uraia ya Tanzania ya mwaka 1995 Sura 357 kama ilivyorejewa mwaka 2002, pamoja na kanuni zake za mwaka 1997. Sheria hii imeanisha aina tatu za uraia wa Tanzania ambazo ni;
1. Uraia wa Tanzania kwa kuzaliwa
2. Uraia wa Tanzania kwa kurithi
3. Uraia wa Tanzania kwa Tajnisi au kujiandikisha.
URAIA WA TANZANIA KWA KURITHI.
Mtu aliyezaliwa nje ya Tanzania siku na baada ya Muungano atakuwa raia wa Tanzania kwa
kurithi endapo mzazi wake mmoja ni raia wa Tanzania kwa kuzaliwa au kuandikishwa/tajnisi. Ni vyema ieleweke kuwa mtu aliyezaliwa nje ya Tanzania hawezi kuwa raia wa Tanzania kwa kurithi iwapo baba/mama yake ni raia wa Tanzania kwa kurithi.