Tatizo ni kwamba ndani ya katiba mpya kuna jina la Tanzania. Maana kuna Tanganyika, Zanzibar na Tanzania.Usihofu mkuu baada ya KATIBA MPYA kupita mwakani hilo jina la TANZANIA tutalizika rasmi, sasa wakianza kuziita bidhaa zao kwa jina letu halisi la TANGANYIKA tutatangaza kuwatimua wakenya wote nchini kama tulivyowafanya Wanyarwanda.
Hii nchi tunaishi bora liende tu, Nobody cares on anything just Selfishness and Greedy is all our leaders cares about.
Wanaofanya hadi nchi hii kusema ni ya mazezeta wanajulikana nafikili wao ndo ungesema mazezeta kuliko kusema nchi yote kiujumla, maana mimi mwananchi wa kawaida nitafanyaje kama wahusika wa kushugulikia hili wapo na hawatekelezeji wajibu wao.
View attachment 107734 View attachment 107735View attachment 107736
Hivi inawezekanaje hasa hadi majirani zetu watuchezee namna hii? A Kenyan tea, halafu inaitwa Tanzania, pamoja na ramani ya Tanzania na twiga ambaye ni alama ya Tanzania? Hivi kweli hawa wenzetu wanaweza kuuza bidhaa zao kwa kutumia vivutio vyetu kwa style hii? I once saw a Kenyan Coffee with a name Kilimanjaro, nikashangaa sana, sasa naona wamevuka mipaka hadi kuziita product zao kwa jina la Tanzania.
Mkuu kabla haujahitimisha kujiita na kuwaunganisha wengine basi ungefanya jitihada ya kutuonyesha hiyo Product imetengenezwa wapi (Made I /Product Of).
Maana nadhani kwa Kampuni toka Kenya inayofanya uzalishaji hapa Tanzania kutumia Nembo kama hiyo kibiashara ni Jambo la kupongzwa kuliko kuiponda na kuleta Siasa . Lakini kama uzalishaji na Raw material inayotumika kwenye mazao husika kama haitoki hapa kwetu basi hilo kupaza sauti ni muhimu na hata kuchukua hatua za Kisheria kupitia mamlaka inayohusika.
Usijali mkuu, nilifanya kosa mimi kwa kuwa sikuweka uwezi wa kwanini ninaikosoa hii hali. Hiyo chai inayotumia jina la Tanzania ni ya Kenya. Na ina label kabisa inayoonyesha kwamba hiyo ni quality tea ya Kenya. Sasa kama chai ni ya Kenya wanapata wapi mamlaka ya kutumia jina, Ramani, na alama za Tanzania? Hivi kama ingetokea kiwanda kimoja cha Tanzania kikafanya haya, wakenya wangetuacha?Mkuu Lukolo samahani kwa maoni yangu.Sikusoma kwa undani maelezo yanayosomeka kwenye hizo picha.Kusema kweli hii kitu imekaa ndivyo sivyo kwa kiwango chochote kile cha kibiashara hasa hiyo ya Safari Premium Tea .Hapa Wizara husika inatakiwa kuchukua hatua mara mmoja.
Hii nchi hivi sasa ni shamba la bibi, yeyote anayetaka kutengeneza faida kupitia nchi yetu anajitengenezea tu and there is any control mechanism. Najiuliza usiku na mchana hiyo idara inayoitwa usalama wa taifa ni akina nani na kazi yao ni nini? Mbona hii idara imekuwa hoi sana hivi sasa? Madawa ya kulevya, mabomu, mauaji, ujambazi wa kutisha, kupeperusha bendera (Iran), na sasa hadi kwenye biashara. Hii idara imelala tu. Haya ndiyo matatizo ya kupeana vyeo kutokana na ushemeji.Duh hiyo kweli balaa, kwa hiyo hata wakiuza sumu huko nje na ikagundulika kuwa ni sumu yenye madhara lawama na skendo yote ni juu ya Tanzania, maana inaonesha ndiyo origin ya product yenyewe, kweli hii ni zaidi ya majanga.
Where is our intelligence system. Ushenzi mkubwa kabisa, yale yale ya Meli za Iran na bendera za Tanzania.
well said, kuiondoa CCM madarakani ni hatua mojawapo! Lakini je watanzania wana mwamko huo?Toa elimu kwa ndugu yako ,kila mmoja ana wajibu huo.kwani hakuna njia nyingine ni lazima chama dhaifu na viongozi wao dhaifu waondoke kwanza.Tunatakikiwa kuondoa chanzo cha tatizo ili kumponya mama Tanzania.
si busara hata kidogo kutuita mazezeta, ungewaita waliokabidhiwa dhamana kuwa ni mazezeta, sio vinginevyo. ss sio mazezeta na hatutakuwa mazezeta ndio maana hata ww umeona kuwa ni kitu cha aibu sana
kibiashara wanaitangaza TZ siku tutakapoacha ufisadi na kuzlisha kahawa yetu tutakuwa maarufu kuliko kenya yenyewe