Tanzania: Ni yapi yaliyojiri 1995?


Naweza nikasahihishwa kwenye hili ila kwangu mimi naona CY ya Dr. Salim Ahmed Salim imeng'arishwa zaidi na vyeo alivyo shika badala ya nini alifanya katika hivyo vyeo.

Mfano Sokoine anakubwa kwa yale aliyo yafanya akiwa waziri mkuu nk. ila kwa Salim sioni hili. Pia kutokana na uelewa wangu Salim amelaumiwa sana na Watanzania wengi pale OAU kwa kuto kusaidia Watanzania kupata nafasi za kazi mbali mbali.

Nikisema kusaidia simaanishi kuwafanyia upendeleo bali inasemekana alikwenda a step ahead na kama kuhakikisha ana wazibia oppportunity Watanzania. Naomba nisahihishwe ikibidi.
 

Labda alikua na ndoto ya A STAR SHINING ON THE DARK.
 
Labda alikua na ndoto ya A STAR SHINING ON THE DARK.

Ni kweli mkuu maana mimi sijaona kikubwa alicho fanya. Binafsi nadhani ana mafanikio zaidi katika siasa za nje (diplomasia) kuliko siasa za ndani.
 
Kuna mambo mawili ninayoyafahamu yaliyompelekea Mwalimu kumpenda Salim. Kitu cha kwanza ni uchapa kazi. Salim alikuwa akipewa assignment na Mwalimu, mathalan amekwenda ziara ya nje, akirudi alikuwa anahakikisha siku hiyo hiyo Mwalimu anapata ripoti kamili.

Niliwahi kuzungumza na afisa mmoja wa wizara ya mambo ya nje aliyekuwa akifutana na Salim akasema Salim alikuwa anawataka maafisa wake wakamilishe ripoti zao kwake kabla ya kufika Dar-es-Salaam. Mathalan, kama ndege imetua usiku wa leo, kesho asubuhi by saa nne Salim atakuwa ameshapeleka ripoti yake Ikulu. Hilo moja. Pili, ni jinsi alivyotendewa Zanzibar baada ya mapinduzi.

Salim hakuwahi kulalamika hadharani juu ya uovu waliotendewa ndugu zake wakati wa mapinduzi. Those 2 elements earned him Mwalimu's endearment. Kama angekuwa rais mzuri 1985 au 1995 sijui, lakini nina hakika katika utendaji he would have been much better than Kikwete in 2005.
 
Jasusi,Mwanafalsafa1,

..kwa upande mwingine ni vigumu kwa Mtanzania wa kawaida ku-appreciate mchango waziri wa Mambo ya Nje.

..inawezekana kabisa Salim Salim angetumikia ktk wizara kama ya Ujenzi au Kilimo basi tungeweza kuwa jambo la kusema kuhusu mchango wake kwa wa-Tanzania wa kawaida.

..binafsi I did not support his candidacy kwasababu nilikuwa naona ni mtu ambaye hakuwa seasoned enough ktk kushughulikia matatizo ya ndani, kama ya nchi hii.
 
Labda tuanzie pale Nyerere aliposema kuwa "serikali inanuka." Ilifika wakati wafadhili waligoma kuisaidia Tanzania kwa sababu serikali ya Mwinyi ilikuwa haikusanyi kodi.

Na mara kwa mara Nyerere alipokuwa anasafiri nje alikuwa anasikia malalamiko mengi kuhusu utendaji wa serikali yetu. Nakumbuka ilipotokea scandal ya Mbilinyi. Nyerere alikuwa New York wakati huo. Nikapata nafasi ya kuonana naye. Alisema kuwa hata kama si kweli kwamba Mbilinyi amechukua hela za kampuni ya samaki, ni lazima ajiuzulu kwa sababu ya kuonyesha kuwa serikali mpya haitavumilia tena mambo ya rushwa.

So he was very proud of Mkapa's performance, pale alipoanza kukusanya kodi na hela mitaani zikaisha, Waswahili wakakiita kipindi chake kipindi cha ukapa. Mwalimu aliamini kabisa kuwa sifa za Tanzania katika nchi za nje zitarejeshwa na utendaji wa Mkapa.
 
Jasusi, hivi umewahi kufanya mahojiano na Nyerere?
 

wewe jifunze historia vizuri
salim aliwahi kuwa waziri wa ulinzi
na aliheshimika mno na jeshi
sio kila waziri hasa kutoka zanzibar anae weza kukubalika na kuheshimi na jeshi

na alipokuwa waziri mkuu,akapendwa mno na watu
na uliza waziri ganimkuu alie pendwa na watu zaoidi ya salim na sokoine????/
 

The Boss,

..kama una taarifa zinazohusu rekodi na utendaji wa Salim Salim akiwa Waziri Mkuu, au alipokuwa Naibu Waziri Mkuu, Waziri wa Ulinzi na JKT, unaweza kuziweka hapa.

..habari za mitaani ni kwamba wanajeshi walimpenda sana Salim Salim kwasababu walikuwa na shida ya usafiri na yeye akaweza kwenda Uarabuni na kuleta magari ya msaada. wengine wanakwenda mbali na kumsifia kwa kudai kwamba magari hayo alipewa binafsi lakini kutokana na roho ya upendo aliyokuwa nayo akawagawia yote wanajeshi.

..pia kuna habari nyingine kwamba Salim Salim alikwenda mikoa ya kusini na kukuta wananchi wanashida kubwa ya chakula na mavazi. inasemekana alikuta wananchi wanakula mizizi na kuvaa kaniki. sasa ili kutatua tatizo hilo Salim Salim akaagiza wapewe nguo za mitumba.

..pamoja na kwamba maamuzi hayo yalikuwa ni mazuri na yenye msaada kwa wananchi, lakini sidhani kama yanatosha kumfanya mhusika afikiriwe kwa madaraka makubwa zaidi kama Raisi.

NB:

..binafsi ningemkubali Salim Salim kama angeweza kuja na program ya kilimo mikoa ya kusini ili wananchi wasikumbwe tena na tatizo la njaa. inaelekea baada ya kuwapa chakula cha msaada na nguo za mitumba na yeye kusifiwa magazetini basi wananchi wale wa kusini wamesahauliwa.
 
Salim angekubali kugombea mwaka 1995 ndiyo ingekua nafasi yake kubwa ya kushinda kwa vile baba wa taifa alikuwepo na ni wazi alikua akimtaka. Japo bado Wazanzibar wangemuekea ngumu nadhani sauti ya Nyerere ingesaidia sana. 1995 was his best chance at the presidency.

Ila pia hili swala zima la Salim na Nyerere inaonyesha asivyo mbaguzi. Yeye hakutaka mambo ya kupokezana ndiyo maana japo raisi aliekua ana maliza muda wake alikua Mzanzibar na Muislamu bado Nyerere hakuona tabu nafasi hiyo kuchukuliwa tena na Mzanzibar Muslamu. Sasa sijui wale wanaosemaga Nyerere alikua anapinga Uislamu au kuitawala kimabavu Zanzibar wanatoa wapi mawazo hayo.
 


kitendo cha kum face nyerere tu na kumwambia sera hazileti matunda tubadilishe sera
ili watu wale na kuvaaa ilikuwa ujasiri ambao si kila mtu aliweza enzi hizo
 
Joka Kuu,
Kwenye bold; I aggree kwamba wenye njaa dont give them fish,instead teach them how to fish.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…