Uchaguzi 2020 Tanzania ni yetu sote, hakuna mgeni kutoka nje tunayepambana naye

Uchaguzi 2020 Tanzania ni yetu sote, hakuna mgeni kutoka nje tunayepambana naye

DOMBWELA

JF-Expert Member
Joined
Jan 18, 2014
Posts
757
Reaction score
843
Nilivyo kuwa nasikia kuwa ukiona vyaelea ujue vimeundwa, nimeamini! au usilolijua ni kama usiku wa giza, nimeamini!

Wadau hali inayoendea ya kundi moja kujihakikishia kuendelea kuwepo madarakani na kundi lingine kujihakikishia linashika madaraka na kuongeza nchi sio lelemama aisee!

Makundi haya yako tayari umoja, mshikamano na amani yetu kuiweka kando ili ndoto zao zifikiwe!

Yanayoendelea awamu hii siambiwi na mtu ila naona kwa macho yangu kupitia nafasi yangu, maana chaguzi zilizopita nilikuwa nasimuliwa!

Wahusika kwa nafasi zenu naomba tukumbushane, Tanzania ni yetu sote hakuna mgeni kutoka nje tunayepambana naye. Mdogo mtu yupo upande mwingine na kaka mtu mtu pia yupo upande mwingine pia, vivyo hiyo kwa wajomba, baba na watoto wao!

Tukumbuke pia kuwa hatuna Tanzania nyingine zaidi ya Tanzania iliyoasisiwa na Hayati Baba wa Taifa Mwl J. K. Nyerere itasambaratishwa kwa tamaa ya madaraka, ubinafisi na makundi ya watu wenyewe malengo maovu wasio itakia mema nchi yetu na vizazi vilivyopo na vijavyo.

Kwakuwa wanaotaka kuendelea kushika dola na kwakuwa wanaotaka kushika dola wote ni watanzania wenzangu, kwa kuwa pia ndugu zangu mkae mkijua kuwa kura yangu kati yao au yenu nitaitoa tu kwa yule atakae nishawishi kwa sera zake za maendeleo, amani, mshikamano, n.k, na si kwa sababu nyingine yoyote.
 
Nilivyo kuwa nasikia kuwa ukiona vyaelea ujue vimeundwa, nimeamini! au usilolijua ni kama usiku wa giza, nimeamini!

Wadau hali inayoendea ya kundi moja kujihakikishia kuendelea kuwepo madarakani na kundi lingine kujihakikishia linashika madaraka na kuongeza nchi sio lelemama aisee!

Makundi haya yako tayari umoja, mshikamano na amani yetu kuiweka kando ili ndoto zao zifikiwe!

Yanayoendelea awamu hii siambiwi na mtu ila naona kwa macho yangu kupitia nafasi yangu, maana chaguzi zilizopita nilikuwa nasimuliwa!

Wahusika kwa nafasi zenu naomba tukumbushane, Tanzania ni yetu sote hakuna mgeni kutoka nje tunayepambana naye. Mdogo mtu yupo upande mwingine na kaka mtu mtu pia yupo upande mwingine pia, vivyo hiyo kwa wajomba, baba na watoto wao!

Tukumbuke pia kuwa hatuna Tanzania nyingine zaidi ya Tanzania iliyoasisiwa na Hayati Baba wa Taifa Mwl J. K. Nyerere itasambaratishwa kwa tamaa ya madaraka, ubinafisi na makundi ya watu wenyewe malengo maovu wasio itakia mema nchi yetu na vizazi vilivyopo na vijavyo.

Kwakuwa wanaotaka kuendelea kushika dola na kwakuwa wanaotaka kushika dola wote ni watanzania wenzangu, kwa kuwa pia ndugu zangu mkae mkijua kuwa kura yangu kati yao au yenu nitaitoa tu kwa yule atakae nishawishi kwa sera zake za maendeleo, amani, mshikamano, n.k, na si kwa sababu nyingine yoyote.
Umesema kweli kabisa ila mwaka huu kuna kura mbili uzalendo na beberu, kuna mgombea muda huu anapokea maelekezo kutoka kwa vibaka wa mabeberu na kutii kila kitu, na amekuwa akitishia watu kushitakiwa na ana shida si tu kushinda bali hata kuleta vurugu.
Kwa nini beberu wawe ndo wakosoaji kwa kila speech ya Raisi na mtu huyo sio mtz kisha kushauli uvunjifu wa sheria?

Wakati huko kwao wanaheshimu sheria na maamuzi ya mwisho ni mahakama.
Kura ni haki yako unapotaka, ila ujue kuna mambo hayo mawili.
1 uzalendo
2 beberu
 
Ebu tuwekeeni ushahidi wa Hao Mabeberu.. Mh. Lissu hakuna asiyemjua kwa msimamo wake na uzalendo wake. Hao Mabeberu Mnaosema anafungamana nao sio Kweli. Lissu alikwenda Belgium kutibiwa baada ya jaribio ovu la Kumuua. Lissu hakuenda Nje ya Nchi Kutafuta Mabeberu, bali alienda Kutafuta uhai wake uliokuwa hatarini. Hakuna Mzalendo katika nchi hii wa Kumzidi Lissu... Ajitokeza na atuambie amefanya nini tofauti na kutetea tumbo lake. Watanzania wa sasa sio Wajinga...Lissu wanamjua vizuri..
 
Umeandika busara kubwa sana ambayo ni nadra sana kutolewa na mtu mzima wa karne hii anayeshabikia chama cha mapinduzi.
 
Hili kuwezekana hadi ccm itoke madarakani.Huu mfumo wakijima uliopo unawanufaisha wao kwahiyo kamwe usitegemee mabadiliko ya icho unachokisema endapo wataendelea kuwepo.
Kuna haja ya kuwa na mfumo imara unaolinda maslahi ya Taifa kwanza ambao hauwezi kuingiliwa na mtu, kikundi, chama au taasisi yoyote!.
 
Kauli hiyo imfikie balozi wa Marekani na viongozi wa siasa anapokutana nao huu ni uchaguzi wa watanzania kwa hiyo akae kando asituingilie
 
Kauli hiyo imfikie balozi wa Marekani na viongozi wa siasa anapokutana nao huu ni uchaguzi wa watanzania kwa hiyo akae kando asituingilie
Jeshi la polisi na silaha wanazopewa na sisi wananchi nao waambie wawaache waTanzania tufanye uamzi wetu bila kushurutishwa wala kutishwa.
Hapa unaweza usielewe nilichokiandika kwa sababu akili zilishagota siku nyingi.
 
Jeshi la polisi na silaha wanazopewa na sisi wananchi nao waambie wawaache waTanzania tufanye uamzi wetu bila kushurutishwa wala kutishwa.
Hapa unaweza usielewe nilichokiandika kwa sababu akili zilishagota siku nyingi.
Wewe mwenye akili za chabo huwezi kuelewa unasoma bila kutafakari
 
Kwakuwa wanaotaka kuendelea kushika dola na kwakuwa wanaotaka kushika dola wote ni watanzania wenzangu, kwa kuwa pia ndugu zangu mkae mkijua kuwa kura yangu kati yao au yenu nitaitoa tu kwa yule atakae nishawishi kwa sera zake za maendeleo, amani, mshikamano, n.k, na si kwa sababu nyingine yoyote.
Mkuu umeacha HAKI-usiwe na kigugumizi kuitaja wazi wazi.
 
Kuna haja ya kuwa na mfumo imara unaolinda maslahi ya Taifa kwanza ambao hauwezi kuingiliwa na mtu, kikundi, chama au taasisi yoyote!.
Hili lingefanyika Polisi na Usalama wa Taifa ningewaona wamelitendea makubwa Taifa letu. Lakini badala ya kulinda Taifa wanalinda Chama. Tuna vyombo vya dola visivyoweza kutofautisha kati ya Chama na nchi. Tanzania ukiisema CCM unaambiwa unaisema nchi.
 
Back
Top Bottom