Tanzania nzima inaweza msahau Hayati Magufuli ila sio Tabora

Tanzania nzima inaweza msahau Hayati Magufuli ila sio Tabora

Nebuchadinezzer

JF-Expert Member
Joined
Oct 1, 2018
Posts
1,403
Reaction score
2,546
Nimefika Tabora ndugu zangu, nimelia sana baada ya kukumbuka kuwa JPM hayupo tena duniani.

Magufuli, Magufuli, Magufuli, nimekuita mara tatu, najua hunisikii, ila Mungu atakulipa siku ya ufufuo. Ni miaka 60 tangu tupate uhuru, mkoa wa Tabora ulisahaulika sana...hasahasa kwenye huduma muhimu za kijamii.

Awamu zote kabla ya JPM zilipita,bila kuwaletea wana Tabora maji safi na salama. JPM aliwahi kusema, ukiomba mkopo ili upeleke huduma ya maji Tabora, wahisani wanakataa.... JPM aliamua kutumia hela anayokusanya (Kodi) kupeleka maji katika mkoa mkubwa wenye historia iliyotukuka.

Kilichoniliza sio JPM kufa, wala kuleta maji Tabora. Kilichoniliza, kuna bibi mmoja, aliniomba hela 2,000...nikasita kumpatia maana anaonekana ni mlevi. Mimi msabato, ni makosa kumpatia mtu hela akanunue kitu kitakachomuangamiza.

Nikamuuliza ya nini 2000, akanambia "Mjukuu wangu, hii naenda kulipia mkopo wa bomba la maji" Nilishituka, ikabidi nimuite dogo mmoja, alikuwa anapita, nikamuuliza kama kuna mikopo ya hivyo.

Dogo akanambia baada ya maji kufika wilaya ya nzega kipindi cha JPM, changamoto ilikuwa wananchi wengi hawakuwa na uwezo wa kuvuta mabomba ya maji kutoka ziwa Viktoria. Serikali ya wanyonge, kupitia rais Magufuli akatoa order, kila asiyenauwezo wa kuvuta bomba la maji, atakopeshwa, atakuwa analipa 2000 kila wiki mpaka itakapo timia 40,000.

Bibi yule nilimpa 2000. Sasa leo Napita zangu mitaa ile yule bibi ananiletea risti inayodhibitisha kalipia maji. Nilishangaa sana. Nilimpa 20,000 ili akalipe deni lote. Baada ya kufika, napolalaga, nilianza kulia baada ya kukumbuka kuwa JPM hayupo tena duniani.

Tabora nayoifahamu mimi, leo ndoo mbili shilingi 50? Miaka 60 bila maji, Magufuli akaleta maji.

AsanteMagufuli- Kweli vizuri havidumu
 
Hivi Rais ndio analeta sehemu maji?

Haya mambo ndio yanatufanya tushinikize katiba mpya

"UGATUZI" watu wapate maendeleo wanayoyataka kwa kupanga wenyewe sio kupangiwa na yeyote

Maana watu ndio walipa kodi sio mtu anaamka kisa yeye ni Rais anajenga uwanja wa ndege kwao na Hifadhi ya wanyama

Hivi wananchi wa Chato kipaumbele chao ni Uwanja wa ndege na Mbuga ya wanyama?
 
Ivi Rais ndio analeta sehemu maji?

Haya mambo ndio yanatufanya tushinikize katiba mpya

"UGATUZI" watu wapate maendeleo wanayoyataka kwa kupanga wenyewe sio kupangiwa na yeyote

Maana watu ndio walipa kodi
Upo sahihi mkuu,
Rais haleti maji ila kodi za wananchi zinaleta maji.

JPM alikubali kutukanwa na kuambiwa anachukua kodi kwa nguvu ili apate hela ya kupeleka maji Tabora.

Kukusanya kodi kwa wafanyabiashara waliozoea kusamehewa na kukwepa kodi sio mchezo mkuu.

Si unajua kuna baadhi ya wafanyabiashara walihamishia biashara zao nje ya nchi ili kukwepa kodi? Akiwepo tajiri Freeman Mbowe wa Moshi?

Miaka yote ya uhuru, kodi imekusanywa, Tabora ni miongoni mwa mikoa inayotoa mapato makubwa sana, mbona maji hayakuwepo?

JPM will forever live in peoples's hearts.
 
Dah nchi hi bana KODI yako lakn unaona Kama mtu katoa mfukoni mwake
Upo sahihi mkuu,
Rais haleti maji ila kodi za wananchi zinaleta maji.

JPM alikubali kutukanwa na kuambiwa anachukua kodi kwa nguvu ili apate hela ya kupeleka maji Tabora.

Kukusanya kodi kwa wafanyabiashara waliozoea kusamehewa na kukwepa kodi sio mchezo mkuu.

Si unajua kuna baadhi ya wafanyabiashara walihamishia biashara zao nje ya nchi ili kukwepa kodi? Akiwepo tajiri Freeman Mbowe wa Moshi?

Miaka yote ya uhuru, kodi imekusanywa, Tabora ni miongoni mwa mikoa inayotoa mapato makubwa sana, mbona maji hayakuwepo?
 
Juzi nimesikia Rais katoa hela kula Jimbo,
Mh akasema tumpigie makofi.
 
Acha kuropoka, mpango wa kupeleka maji Tabora, Singida hadi Dodoma kutoka Ziwa Victoria uliandaliwa tangu enzi za Rais Mkapa wakati Lowassa akiwa waziri wa maji. Na mpango huo bado unatekelezwa!
Wewe ndio unaropoka mkuu,

Tanzania iliweka mpango, ifikapo 2025, ifikie Uchumi wa kati wa Chini, mwaka 2020 Tanzania ikafikia uchumi wa kati wa chini.

Mipango ni kitu kimoja, kutekeleza mipango ni kitu kingine.

Kupanga ni rahisi sana ila kutekeleza ni kazi inayohitaji kujitoa sadaka.

Nadhani utaacha uropokaji baada ya hapa.
 
..Tabora maji yamefika.

..lakini kuna maeneo ya karibu zaidi na Ziwa Nyanza / Victoria hayajapatiwa maji.

..wakati huohuo serikali inatumia matrilion kununua ndege zinazotuingizia hasara, na kujenga mji mkuu wakati tayari tulikuwa nao.
 
Back
Top Bottom