Tanzania One Theatre (T.O.T) wapo wapi?

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513
Watanzania poleni sana kwa msiba huu mkubwa uliotuelemea. Wengi tulimpenda sana rais wetu kutokana na mazuri mengi aliyotufanyia.

Mengi yamesemwa na sina lengo la kuyarudia. Lengo la hii thread ni kuhoji ukimya wa kwaya ya TOT ambapo nakumbuka wakati wa msiba wa mzee wetu Rais Mstaafu Mkapa walitoa wimbo maalumu tena muda mfupi baada ya tangazo la kifo chake.

Kwenye msiba wa Baba Magufuli naona Msechu ndiye amejikongoja na kutoa wimbo dakika chache baada ya Rais Samia Suluhu kutangazia Taifa kifo cha JPM.

Kulikoni?
Mlioko karibu na TOT tujuzeni kinachojiri au kwaya imesambaratika?

Mji mpana huu
 
TOT ni ya CCM!!!!! Mambo ni mengi na muda ni mchache sana. Watu wako busy na shamrashamra.
 
Jana nilisikia wimbo flani redion, sound yake ilikua ni ya TOT ila sina uhakika, nilisikia sauti ya yule jamaa wa Ile ngoma tumeipenda wenyewe!
 
Mara ya mwisho nawasikia wanaongelewa kabla ya wewe kuwaulizia Dr. Bashiru alisema watawatumia kwenye kampeni pamoja na nyimbo za mazumari na ngoma sema sijui nini kiliwakuta hatukuwaona
 
Dah! Ile TOT ya Captain John Komba (RIP) enzi zile ilikuwa ni nyoko! Jamaa alikuwa na kipaji cha uimbaji aisee! Hasa wa nyimbo zenye maudhui ya kwaya!!!

Yaani ule mwaka 1999 wakati wa kifo cha mwalimu Nyerere, unaweza ukadhani labda alijulishwa mapema kama kuna kifo! Maana nyimbo zake zote zilienda shule na zilikuwa zinasikilizika! Achilia mbali zile alizo zitunga kwa ajili ya kampeni za chama chake cha CCM!

Hakika pengo lake kamwe halitokuja kuzibwa.
 
Jana nilisikia wimbo flani redion, sound yake ilikua ni ya TOT ila sina uhakika, nilisikia sauti ya yule jamaa wa Ile ngoma tumeipenda wenyewe!
Wapo kimya hadi sasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…