Kwajinsi na mifano yako utakuwa unapenda sana umalaya na una pepo la ngono. Wanawake humu wametoka wapi.
Anayeona mwanamke ni mfano wa umalaya na ngono ndiye mwenye pepo la umalaya na ngono.
Kwangu mimi wanawake ni mama zangu, dada zangu ndugu zangu etc.
Kama hujaelewa mfano, uliza.
Siwezi kutoa mfano wa quantum physics na Kaluza-Klein manifold hapa kwa kuwa sina uhakika wengi wataelewa.
Nimetoa mfano wa mwanamke kwa sababu watu wote watauelewa.
Nchi ikiwa inavutia sana kwa kuwekeza vitegauchumi inaweza kupitwa na nchi ambayo haivutii sana katika kuvutia vitegauchumi, kwa sababu za jinsi wenye nchi wanavyojua kutumia fursa zao walizopewa kuvutia vitega uchumi.
Mfano, Kenya haina vivutio sana vya vitegauchumi, lakini inaishinda Tanzania yenye vivutio zaidi kwa sababu wenzetu wanajua kutumia vivutio vyao vichache.
Vivyo hivyo, hata mwanamke ambaye si mzuri sana lakini anayepewa matunzo mazuri na vipodozi anaweza kuvutia kuliko mwanamke mzuri sana ambaye hapewi matunzo wala vipodozi.
Sielewi hapo mtu mwenye akili zake timamuanaonaje umalaya.
Wewe ni Taliban, ISIS au Al-Qaeda?