Tanzania "Shamba la bibi" hadi lini? Hii Ruby ni yetu. Iweje iko sokoni Dubai na serikali yetu haijui? Nasaidia, mchimbaji huyu, anzieni hapa!

Tanzania "Shamba la bibi" hadi lini? Hii Ruby ni yetu. Iweje iko sokoni Dubai na serikali yetu haijui? Nasaidia, mchimbaji huyu, anzieni hapa!

Duh...!. Mkuu fundimchundo!, That is the base kabisa!. Kumbe watu humu mnatufahamu hadi home!. Tuwe tunatambulishana utakuta mtu unamtukana kumbe ni mtu wako kabisa.
P
Kwangu mimi, wewe ni sehemu ya Familia kutokana na upendo wa MK. Na wewe Paskali umetuzidi ujasiri tulio wengi humu JF kwa kutumia jina lako halisi. Hongera sana. Ninayo namba yako. Nitakutafuta inbox
 
Mama amefungua nchi
Eban eh! Wewe unajua mambo kikamilifu. Ndiyo kufungua nchi kwenye huko ili vitu viingia ndani na vitoke nje. Tumefurahia nchi kufunguliwa, halafu tunaanza kulia vitu kutoka nje. Hatuwezi kupata yote: kufungua nchi, halafu vitu vibaki ndani tu. Utakuwa uhayawani huo.
 
Kwani ni sheria gani imevunjwa hapa? Kama ni mtu binafsi amechimba hilo Ruby halafu kaliuza, kavunja sheria? Ina maana mauzo binafsi (private sale) baina ya watu wawili waliokubaliana bei ni kinyume cha sheria? Kama ni kweli basi tuna mfumo mbovu wa kijamaa.
Kuna sheria ya uuzaji wa madini mzee; hayauzwi kama kama maandazi.
 
Kwangu mimi, wewe ni sehemu ya Familia kutokana na upendo wa MK. Na wewe Paskali umetuzidi ujasiri tulio wengi humu JF kwa kutumia jina lako halisi. Hongera sana. Ninayo namba yako. Nitakutafuta inbox
Thanks.
P
 
Ndiyo mfumo mbovu wa kijamaa huo.
Siyo mfumo wa Kijamaa ndugu yangu, ni sheria za nchi. Hata Marekani kwa baba wa ubepari kuna sheria za madini, kwa mfano huwezi kuuza madini ya uranium bila kupata kibali cha serikali, na huwezi kuuza baadhi ya products unazotengeza mwenyewe kwa mfano electronic components, infra red sensors, na optical gryoscpes bila kupata kibali cha serikali.

Urusi na China ndiyo basi kabisa, madini yote ya rare earth minerals yaliyoko China ni mali ya serikali tu. Halafu pia madini yote yaliyoko kwenye ardhi ya Urusi, pamoja na kuwa kuna makampuni binafsi yanayochimba, lakini lazima mauzo yake yarekodiwe serikalini. Sasa wewe sijui unataka system ipi hiyo isisyosimamiwa na serikali kuhusu raslimali za nchi.

Sikiliza hii kuhusu madini ya Uranium Marekani

 
Nigeria ni nchi ya 3 wao wanazalisha mafuta lkn rasilimali za mafuta haziko
Mkononi mwao!hawafaidiki kivile

Sababu ni viongozi wetu kutokua na msimamo na ubinafsi

Ova

shida ilianzia nchi za Africa zilipodai uhuru huku hazijui nini maana ya uhuru, zinahitaji nini, na uhuru unalindwaji......matokeo yake tukapewa uhuru wa bendera na kurudi utumwani kwa style nyingine...

WaAfrica tunahitaji ukombozi mwingine aka winbi la pili la kudai uhuru kamili..
 
mkuu kwani hii katiba ya sasa inaruhusu utoroshaji wa maliasili za nchi na uhujumu uchumi?
Tatizo ni mifumo mbovu huwezi kumwajibisha kiongozi yoyote kama wewe ni mwananchi mfano Jafo alisema mto Mara yale ni mavi ya ng'ombe jana wanasema ni sumu toka mgodini lakini bado yupo madarakani yaani yupo tayari wananchi wafe lakini yeye aendelee kula pipi mjini
 
Siyo mfumo wa Kijamaa ndugu yangu, ni sheria za nchi. Hata Marekani kwa baba wa ubepari kuna sheria za madini, kwa mfano huwezi kuuza madini ya uranium bila kupata kibali cha serikali, na huwezi kuuza baadhi ya products unazotengeza mwenyewe kwa mfano electronic components, infra red sensors, na optical gryoscpes bila kupata kibali cha serikali.

Urusi na China ndiyo basi kabisa, madini yote ya rare earth minerals yaliyoko China ni mali ya serikali tu. Halafu pia madini yote yaliyoko kwenye ardhi ya Urusi, pamoja na kuwa kuna makampuni binafsi yanayochimba, lakini lazima mauzo yake yarekodiwe serikalini. Sasa wewe sijui unataka system ipi hiyo isisyosimamiwa na serikali kuhusu raslimali za nchi.

Sikiliza hii kuhusu madini ya Uranium Marekani


Uranium ni tofauti kwa sababu inatumika kutengeneza silaha. Kwa hiyo haiuzwi kiholela. Ila hao wamarekani wakati wanajenga nchi yao, watu wa kawaida tuu walitajirika kwa kuchimba na kuuza dhahabu. Kwa mfano mji wa San Fransisco California ulijengwa na hao wachimba dhahabu


Tena siyo Marekani tuu, hata Australia na New Zeland walikuwepo

 
Uranium ni tofauti kwa sababu inatumika kutengeneza silaha. Kwa hiyo haiuzwi kiholela. Ila hao wamarekani wakati wanajenga nchi yao, watu wa kawaida tuu walitajirika kwa kuchimba na kuuza dhahabu. Kwa mfano mji wa San Fransisco California ulijengwa na hao wachimba dhahabu


Tena siyo Marekani tuu, hata Australia na New Zeland walikuwepo

Marekani ardhi ni mali ya mtu binafsi, kuna sehemu chache ambazo ardhi ni mali ya serikali, na madini yakichimbwa kwenye ardhi hiyo ya serikali, ni lazima serikali ipate mrahaba. Kwa sasa hivi ardhi ya serikali inatumika kuchimba mafuta tu.

Kwa Tanzania ardhi ni mali ya serikali kwa hiyo huwezi kuchimba madini ukayauza kinyemelea bila serikali kujua. Kinachotakiwa hapa siyo kwamba marekani wanafanya nini, bali ni kufuata sheria zilizopo. Nimekupa mfano wa Uranium tu, lakini kuna madini na vitu vingine ambavyo haviuzwi kiholela nje na wala havitumiki kwenye silaha. Tafuta sheria ya export control kwenye department of commerce uone list ya vitu ambavyo viko controlled. Tunaofanya research kuna wakati ukinunua vifaa ya research unaambiwa usaini makaratasi ya viapo kuwa hutavitoa nje ya nchi.
 
Pasco, sijasoma makala yote kwa sababu Ni ndefu sana! Swali langu Ni dogo tu, hilo jiwe la ruby ni letu, au Ni lake huyo ‘aliyelivua’?! Mtu amepambana huko, labda atapata TB kwa kula vumbi, wewe upo Dar unakula raha ufukweni unasema ruby yetu?!!!
 
Pasco, sijasoma makala yote kwa sababu Ni ndefu sana! Swali langu Ni dogo tu, hilo jiwe la ruby ni letu, au Ni lake huyo ‘aliyelivua’?! Mtu amepambana huko, labda atapata TB kwa kula vumbi, wewe upo Dar unakula raha ufukweni unasema ruby yetu?!!!
Kuna utaratibu wa kuexport madini na tozo au kodi za serikali.

Kuna hela kibao hapo serikali itapata.
 
Marekani ardhi ni mali ya mtu binafsi, kuna sehemu chache ambazo ardhi ni mali ya serikali, na madini ikichimbwa kwenye ardhi hiyo ya serikali, ni lazima serikali ipate mrahaba. Kwa sasa hivi ardhi ya serikali inatumika kuchima mafuta tu.

Kwa Tanzania ardhi ni mali ya serikali kwa hiyo huwezi kucimba madini ukayauza kinyemelea bila serikali kujua. Kinachotakiwa hapa siyo kwamba marekani wanafanya nini, bali ni kufuata sheria zilizopo. Nimekupa mfano wa Uranium tu, lakini kuna madini na vitu vingine ambavyo haviuzwi kiholela nje na wala havitumiki kwenye silaha. Tafuta sheria ya export control kwenye department fo commerce uone list ya vitu ambavyo viko controlled. Tunaofanya research kuna wakati ukinunua vifaa ya research unaambiwa usaini makaratais ya viapo kuwa hutvitoa nje.
Ndiyo tunarudi pale pale kwamba tuna mfumo mbovu wa kijamaa. Marekani hiyo watu wa kawaida wamechimba dhahabu wameuza kiholela wakatajirika na wakajenga nchi, sisi hata ardhi haturuhusiwi kumiliki.
 
Back
Top Bottom