Tanzania(Taifa Stars) yanyolewa bila wembe na Algeria goli 4 kwa 1

Mkuu inawezekana wewe sio mtu wa mpira, Brazil wenyewe walishawahi kufungwa goli 7 pamoja na mastaa walionao. Taifa stars imecheza vizuri by the way
 
Si lazima tuwe succesful kwenye mpira na darasani lazima awe mburula wa mwisho na kipanga namba moja. Football is not our thing, tutangaze tu utalii wetu na urithi wa asili. Ufadhili unaokwenda kwenye soka toka mashirika mbalimbali upelekwe kuvumbua vipaji vingine kama riadha nk.
 
Mkuu inawezekana wewe sio mtu wa mpira, Brazil wenyewe walishawahi kufungwa goli 7 pamoja na mastaa walionao. Taifa stars imecheza vizuri by the way
Walifungwa zile 7 katikati ya UBORA wao, kuteleza kupo. Lini timu yetu iliwahi kuwa bora?
 
Yani ulivoitoa iyo hbr kama vile sio mtanzania, nadhan nyinyi wengine mnafurahia tunapopata matatizo kama taifa.
Kufungwa ktk mechi ya kirafik sio matatizo bali ni changamoto kwa kocha na wachezaji kuelekea kuwa na kikosi bora.
 
uwezo wetu kwenye haya mambo ya michezo ni mdogo sana. Tungeachana tu na mambo ya soka na riadha. Sisi tupo vizuri kwenye fitina za Siasa na Bongo fleva.
 
Yangekuwa mashindano tungepigwa 8-0 ...Kiufupi hatujui mpira
 
Kama tungeshinda tungesemaje? Tatizo Mpira tunaocheza ni bahati nasibu na sio uwezo wa wachezaji!
 
Tusikate tamaa jamani,Timu yetu inahitaji muda
 
Ushauri wa Zitto ufuate, pesa yote ya michezo ya kubahatisha ipelekwe kwenye michezo. Huwezi kufanikiwa bila kuwekeza. Jk alianzisha uwanja bora kabisa lakini umekua wakupigia selfie. Tatizo bajet hakuna.

Lakini pia watanzania tunapenda mawaziri wa chache wenye majukumu mengi bila kujua athari zake, utasikia mtu anaitwa waziri wa Habari, sanaa, utamaduni na michezo. Kwa bajeti gani na kichwa gani abebe hayo mambo yote? Ona sasa week hii TFF walikua bize kufungiana wizara nayo ilikua bize kupambana na wasanii matokeo yake tumepigwa tobo.
 
Tatizo ni TFF maana ndiyo wenye jukumu la kusimamia mpira nchini. mbaya zaidi FIFA hawataki serikali iingilie mpira vinginevyo jiwe angeshawatumbua na angekuwa kafanya kazi nzuri sana. TFF wanawaza matumbo ma si mpira wetu.
 
Kipigo cha goli 4 kwa Timu yetu ya Taifa dhidi ya Algeria Tatizo la msingi ni nin hasa...? Lakini nini kifanyike tutoke hapa tulipofikia
Hio ni improvement kuna mechi walitufunga 6 au 7 hivi! Tumejitahidi sana, mechi ijayo tutafungwa 1 tu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…