Mbona watu tunakuwa wanafiki sana!
Si ni sisi sisi tunaoshangiliaga Simba yetu na Yanga yetu mpaka tunafia uwanjani?
Hizo timu zenu mbili ni mbovu balaa na ndiyo timu yenu ya Taifa.
CCM hawawezi kujinasua kwenye lawama hii. Viwanja vyote wameving'ang'ania wao, haviendelezwi havina taa.
Viwanja vya wazi vilivyokuwa vinatumika kuchezea mpira vingi vimejengwa majengo ya shule, si msingi si sekondari leo wakati wa mapumziko watoto hawana mahali pa kuchezea mpira. Mfano Mwanza hakuna kabisa viwanja vya wazi.
Udhamini uliopo katika ligi kuu na daraja la kwanza ni mdogo sana kiasi vilabu vingi vinashindwa kabisa kujiendesha.
Mimi huwa ninajiuliza, hivi serikali ikitenga walau hata billion 2 kila mwaka kudhamini vilabu vyetu vya ligi kuu itapungukiwa nini, hiyo si inakuwa ni namna nyingine ya kutoa ajira kwa vijana!
Leo Simba na Yanga zinazotoaga wachezaji wa Taifa eti ubora wao ni kuzifunga timu kama Mbao na Toto. Yaani uzifunge timu zenye wachezaji wa kuokoteleza na wenye njaa alafu ndiyo iwe qualification ya kupampana na Aly Misry? Masihara hayo.
Simba ile iliyokuwa inapata nafasi ya kutuwakilisha CAF na kufika hadi fainali ilikuwa kwanza inapitia kwenye tanuru la moto kwa kuzishinda Pamba, Sigara, Reli na Ushirika timu zilizokuwa hazina njaa chini ya udhamini wa serikali ya Mwinyi.
Uimara wa ligi yetu ndiyo uimara wa timu yetu ya taifa.