kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 13,778
- 14,214
Tanzania sio kisiwa, tunahitaji nchi nyingine kwenye mambo mengi ya kisiasa, kiuchumi, kitamaduni na michezo, na kiusalama.
Kwakuwa Tanzania ni sehemu ya dunia, Afrika, SADC, na Afrika Mashariki basi kinachoikumba dunia, Afrika na East Afrika pia kinaikumba Tanzania na utatuzi wake lazima ufananefanane kote.
Dunia inasemekana kwa mujibu wa WHO shirika ambalo linaaminika duniani kote kuwa imekubwa na ugonjwa wa corona wanasayasi wamesema na wametoa njia ya kupambana na ugonjwa huo kama vile walivyoshauri kwa magonjwa mengine kama TB, HIV, Malaria, magonjwa ya moyo, kipindupindu, surua, kifaduro, pepopunda, ndui, nk ambayo hakuna MTU wala taifa linabishana juu ya namna ya kuyatibu na kuyakinga.
Ni kweli kuwa njia ambazo zimependekezwa safari hii na WHO ni njia ngumu sana kuzifuata kutokana na hali za kiuchumi za wananchi na mataifa yao, lakini kwakuwa Tanzania sio kisiwa tunategemea nchi nyingine kwa masoko, usalama, michezo, elimu, na fedha hatupaswi kuchukua njia tofauti kabisa na wenzetu wa dunia na wanaotuzunguuka katika kukabiliana na ugonjwa huu na pengine hata kukataa kuwa ugonjwa huu haupo Tanzania kutokana na maombi huku tukijua kuwa hata huko Israel na Maka ilikotoka mitume na dini hawasemi hakuna covid 19.
Inajulikana kuwa mataifa karibu yote hayatoi takwimu za kweli kuhusu covid 19 lakini angalau wanakubali kuwa covid 19 iko na watu wanaugua na wengine wanakufa.
Kusema kwetu kuna surua nadhani sio dhambi wala aibu bali ni njia njema ya kukinga watoto wenzako wasipate maambukizi kwa kuepuka kuja kucheza na we we nyumbani. Lakini kuficha watoto wenzako kuwa kwenu kuna surua ni kutaka waje kwenu au wewe uende kwao ili nao waambukizwe surua. Watoto wenzako hawatakukubali na watakuchukia sana kama wakijua kwenu kuna surua lakini unaficha. Na ndio maana dunia inalia na China ikidhani labda ilificha uwepo wa corona.
Ni kweli nia ni njema ya kuwatoa watu hofu dhidi ya korona, lakini njia hiyo inakubalika kwa majirani, Africa na dunia? Je, ni kweli maombi yameiondoa covid-19 Tanzania, je ni kweli Tanzania sasa hakuna corona?
Madhara yake makubwa ya kufanya hivi ni kwamba tutaonekana kuwa ni waongo hata kwa mambo mengine yasiyo ya covid 19 huko mbeleni. Ni vema kuwa na mkakati wa pamoja wa kikanda kama vile East Africa, SADC au afrika kuliko kila nchi ikaogelea kivyake.
Kwakuwa Tanzania ni sehemu ya dunia, Afrika, SADC, na Afrika Mashariki basi kinachoikumba dunia, Afrika na East Afrika pia kinaikumba Tanzania na utatuzi wake lazima ufananefanane kote.
Dunia inasemekana kwa mujibu wa WHO shirika ambalo linaaminika duniani kote kuwa imekubwa na ugonjwa wa corona wanasayasi wamesema na wametoa njia ya kupambana na ugonjwa huo kama vile walivyoshauri kwa magonjwa mengine kama TB, HIV, Malaria, magonjwa ya moyo, kipindupindu, surua, kifaduro, pepopunda, ndui, nk ambayo hakuna MTU wala taifa linabishana juu ya namna ya kuyatibu na kuyakinga.
Ni kweli kuwa njia ambazo zimependekezwa safari hii na WHO ni njia ngumu sana kuzifuata kutokana na hali za kiuchumi za wananchi na mataifa yao, lakini kwakuwa Tanzania sio kisiwa tunategemea nchi nyingine kwa masoko, usalama, michezo, elimu, na fedha hatupaswi kuchukua njia tofauti kabisa na wenzetu wa dunia na wanaotuzunguuka katika kukabiliana na ugonjwa huu na pengine hata kukataa kuwa ugonjwa huu haupo Tanzania kutokana na maombi huku tukijua kuwa hata huko Israel na Maka ilikotoka mitume na dini hawasemi hakuna covid 19.
Inajulikana kuwa mataifa karibu yote hayatoi takwimu za kweli kuhusu covid 19 lakini angalau wanakubali kuwa covid 19 iko na watu wanaugua na wengine wanakufa.
Kusema kwetu kuna surua nadhani sio dhambi wala aibu bali ni njia njema ya kukinga watoto wenzako wasipate maambukizi kwa kuepuka kuja kucheza na we we nyumbani. Lakini kuficha watoto wenzako kuwa kwenu kuna surua ni kutaka waje kwenu au wewe uende kwao ili nao waambukizwe surua. Watoto wenzako hawatakukubali na watakuchukia sana kama wakijua kwenu kuna surua lakini unaficha. Na ndio maana dunia inalia na China ikidhani labda ilificha uwepo wa corona.
Ni kweli nia ni njema ya kuwatoa watu hofu dhidi ya korona, lakini njia hiyo inakubalika kwa majirani, Africa na dunia? Je, ni kweli maombi yameiondoa covid-19 Tanzania, je ni kweli Tanzania sasa hakuna corona?
Madhara yake makubwa ya kufanya hivi ni kwamba tutaonekana kuwa ni waongo hata kwa mambo mengine yasiyo ya covid 19 huko mbeleni. Ni vema kuwa na mkakati wa pamoja wa kikanda kama vile East Africa, SADC au afrika kuliko kila nchi ikaogelea kivyake.