#COVID19 Tanzania tuifuate dunia kwenye kupigana na Covid 19

#COVID19 Tanzania tuifuate dunia kwenye kupigana na Covid 19

Huku sio kuiga, bali ni makubaliano ya kitaalam yaliyofikiwa juu ya kupambana na corona, sawa na yale yaliyofikiwa juu ya namna ya kupambana na kaswendwe, gonoria, surua, malaria, mabusha na matende, kipindupindu, upungufu wa damu, magonjwa ya moyo, nk. Huwezi kusema kutumia panadol kupunguza maumivu ni kuigaiga, hiyo panodol haikugunduliwa Tanzania tumeiiga tu kama tulivyoiga na dawa na matibabu mengine yote kutoka nje ya nchi.
Tuna yakwetu ya kitaalam yaliyofanikiwa pia
 
Hao unaotaka kuwafata ili wasikutenge, walijipga lockdown na kujikinga kwa kila namna na sisi tukajiachilia kwa kila namna! kama wanayoyasema ni uhalisia zaidi kuliko porojo, siasa na vitisho vya huo ugonjwa basi hapa bongo tungekua tushadondoka wengi kama kuku mdondo!, kariakoo ingekua wanaokotwa watu kama 200 hvi kila siku, hosptali zingeja.

corona ipo ila wanaitumia kutupiga vita vya kisaikilolojia, its overated!
nani anatupiga vita vya kisaikolojia? maana dunia nzima wanahaha, wanaugua, wanakufa na wamevaa barakoa. Ni taifa gani linalotupiga vita vya kisaikolojia ambalo kwao hakuna corona? wacha ukasuku
 
Hayo ni kweli lakini dunia imetoa utaratibu wa namna ya kushughulikia corona, TB, mabusha, ngiri kavu, moyo mkubwa, nk. Hatuwezi kukubaliana na mengine halafu tukaacha mengine kwakuwa Tz sio kisiwa, tunaihitaji dunia kwa mambo mengi sana kuliko dunia inavyotuhitaji sisi. Mfano, naambiwa kuwa wachezaji wetu wa Namungo wamekwama huko Angola kwasababu ya protocol za kukabiliana na covid 19 zinavyotaka, sasa hapo utasema wameonewa?
ni kweli mkuu, lakini haimaanishi kua kisa miongozo ya mwanzo walituletea tukaitumia, haimaanishi ndo kila kitu sasa, we are okay as we are! they are not okay as they are!, we good they aint good, so why would we tryna actin we aint good just cuz they aint good, while actually we good pal?.

We are just trying to play on our own ways! If they care, they should respect that, dont u think!?
 
ni kweli mkuu, lakini haimaanishi kua kisa miongozo ya mwanzo walituletea tukaitumia, haimaanishi ndo kila kitu sasa, we are okay as we are! they are not okay as they are!, we good they aint good, so why would we tryna actin we aint good just cuz they aint good, while actually we good pal?.

We are just trying to play on our own ways! If they care, they should respect that, dont u think!?
I agree wit what y'r saying. But no single man can go against the world's direction and order, cos the world is a web like thing interlinked and interconnected. If the entire world believes the earth is sniping from east to west who are you arguing it without a robust research to negate the fact? Our arguments about covid that God has cured it are only good for allaying anxiety purposes among our own people, but not that of the world's people.

The world needs and works on a scientific argument, not just prayers worked. Prayers which did not work to th Israel and Saud Arabia where ALL the prophets came from are questionable to believe in.
 
Sio suala la kila ntu apambane na hali yake, bali lazima tufuate inavyotaka dunia (protocol) juu ya namna ya kushughulikia corona, vinginevyo dunia na majirani watatutenga kwenye mahusiano, kwenye michezo, kwenye uchumi, nk. Mfano, timu zetu zinahitaji kwenda kujumuika na timu nyingine kwenye mashindano ya ndani na nje ya nchi na ni lazima wapimwe corona, sasa itakuwaje kama sisi tunasema Tanzania hakuna corona, je, vijana wetu wakikutwa na corona huko tutawaambia nini wenzetu na dunia?.

Vinginevyo Tanzania isimamishe kwanza mambo yote yanayohitaji watu wetu kusafiri nje
fuata
 
Usiopoifuata kwa hiari utaifuata kwa shuruti. Tanzania ni mali ya dunia sio yetu pekee. Bahari, madini, mlima, ardhi na masitu ni mali ya dunia, tunaitunza tu kwa kwa niaba ya dunia. Dunia Ina maslahi yake Tanzania.
 
Endeleeni kushupaza shingo nyie si kisiwa bwana..lakini soon mtajua hamjui..cha msingi kila moja ajilinde na kulinda familia yake..this shit is real!
 
nani anatupiga vita vya kisaikolojia? maana dunia nzima wanahaha, wanaugua, wanakufa na wamevaa barakoa. Ni taifa gani linalotupiga vita vya kisaikolojia ambalo kwao hakuna corona? wacha ukasuku
Vaccine kwa sasa haikwepeki, lazima ukweli huu usemwe.
 
Endeleeni kushupaza shingo nyie si kisiwa bwana..lakini soon mtajua hamjui..cha msingi kila moja ajilinde na kulinda familia yake..this shit is real!
Afya na uhai ni mali binafsi ya mtu, usisubiri mtu akuambie nini ufanye au usifanye ili uwe hai, changanya na akili zako kisha chukua hatua, kaa mbali na mikusanyiko isiyo ya lazima, usisafiri kama sio lazima sana kusafiri, takasa mikono, fanya mazoezi, kula vizuri, vaa barakoa na nenda hospitali mapema.

Kama una wasiwasi za zilipo nyeti za kuku subiri upepo uvume.
 
Vaccine kwa sasa haikwepeki, lazima ukweli huu usemwe.
Huu ni wimbo wa dunia kila mmoja lazima auimbe japo kibwagizo/chorus chake hata kama hajisikii kuimba. Wewe ni nani usiimbe? Watakuimbisha tu wenye wimbo wao kwa nguvu ni heri ujifunze mwenye taratibu kuuimba.
 
Tanzania sio kisiwa, tunahitaji nchi nyingine kwenye mambo mengi ya kisiasa, kiuchumi, kitamaduni na michezo, na kiusalama.

Kwakuwa Tanzania ni sehemu ya dunia, Afrika, SADC, na Afrika Mashariki basi kinachoikumba dunia, Afrika na East Afrika pia kinaikumba Tanzania na utatuzi wake lazima ufananefanane kote.

Dunia inasemekana kwa mujibu wa WHO shirika ambalo linaaminika duniani kote kuwa imekubwa na ugonjwa wa corona wanasayasi wamesema na wametoa njia ya kupambana na ugonjwa huo kama vile walivyoshauri kwa magonjwa mengine kama TB, HIV, Malaria, magonjwa ya moyo, kipindupindu, surua, kifaduro, pepopunda, ndui, nk ambayo hakuna MTU wala taifa linabishana juu ya namna ya kuyatibu na kuyakinga.

Ni kweli kuwa njia ambazo zimependekezwa safari hii na WHO ni njia ngumu sana kuzifuata kutokana na hali za kiuchumi za wananchi na mataifa yao, lakini kwakuwa Tanzania sio kisiwa tunategemea nchi nyingine kwa masoko, usalama, michezo, elimu, na fedha hatupaswi kuchukua njia tofauti kabisa na wenzetu wa dunia na wanaotuzunguuka katika kukabiliana na ugonjwa huu na pengine hata kukataa kuwa ugonjwa huu haupo Tanzania kutokana na maombi huku tukijua kuwa hata huko Israel na Maka ilikotoka mitume na dini hawasemi hakuna covid 19.

Inajulikana kuwa mataifa karibu yote hayatoi takwimu za kweli kuhusu covid 19 lakini angalau wanakubali kuwa covid 19 iko na watu wanaugua na wengine wanakufa.

Kusema kwetu kuna surua nadhani sio dhambi wala aibu bali ni njia njema ya kukinga watoto wenzako wasipate maambukizi kwa kuepuka kuja kucheza na we we nyumbani. Lakini kuficha watoto wenzako kuwa kwenu kuna surua ni kutaka waje kwenu au wewe uende kwao ili nao waambukizwe surua. Watoto wenzako hawatakukubali na watakuchukia sana kama wakijua kwenu kuna surua lakini unaficha. Na ndio maana dunia inalia na China ikidhani labda ilificha uwepo wa corona.

Ni kweli nia ni njema ya kuwatoa watu hofu dhidi ya korona, lakini njia hiyo inakubalika kwa majirani, Africa na dunia? Je, ni kweli maombi yameiondoa covid-19 Tanzania, je ni kweli Tanzania sasa hakuna corona?

Madhara yake makubwa ya kufanya hivi ni kwamba tutaonekana kuwa ni waongo hata kwa mambo mengine yasiyo ya covid 19 huko mbeleni. Ni vema kuwa na mkakati wa pamoja wa kikanda kama vile East Africa, SADC au afrika kuliko kila nchi ikaogelea kivyake.
Wewe si ni CCM mnaopinga kucha kuchwa??
 
Tanzania sio kisiwa, tunahitaji nchi nyingine kwenye mambo mengi ya kisiasa, kiuchumi, kitamaduni na michezo, na kiusalama.

Kwakuwa Tanzania ni sehemu ya dunia, Afrika, SADC, na Afrika Mashariki basi kinachoikumba dunia, Afrika na East Afrika pia kinaikumba Tanzania na utatuzi wake lazima ufananefanane kote.

Dunia inasemekana kwa mujibu wa WHO shirika ambalo linaaminika duniani kote kuwa imekubwa na ugonjwa wa corona wanasayasi wamesema na wametoa njia ya kupambana na ugonjwa huo kama vile walivyoshauri kwa magonjwa mengine kama TB, HIV, Malaria, magonjwa ya moyo, kipindupindu, surua, kifaduro, pepopunda, ndui, nk ambayo hakuna MTU wala taifa linabishana juu ya namna ya kuyatibu na kuyakinga.

Ni kweli kuwa njia ambazo zimependekezwa safari hii na WHO ni njia ngumu sana kuzifuata kutokana na hali za kiuchumi za wananchi na mataifa yao, lakini kwakuwa Tanzania sio kisiwa tunategemea nchi nyingine kwa masoko, usalama, michezo, elimu, na fedha hatupaswi kuchukua njia tofauti kabisa na wenzetu wa dunia na wanaotuzunguuka katika kukabiliana na ugonjwa huu na pengine hata kukataa kuwa ugonjwa huu haupo Tanzania kutokana na maombi huku tukijua kuwa hata huko Israel na Maka ilikotoka mitume na dini hawasemi hakuna covid 19.

Inajulikana kuwa mataifa karibu yote hayatoi takwimu za kweli kuhusu covid 19 lakini angalau wanakubali kuwa covid 19 iko na watu wanaugua na wengine wanakufa.

Kusema kwetu kuna surua nadhani sio dhambi wala aibu bali ni njia njema ya kukinga watoto wenzako wasipate maambukizi kwa kuepuka kuja kucheza na we we nyumbani. Lakini kuficha watoto wenzako kuwa kwenu kuna surua ni kutaka waje kwenu au wewe uende kwao ili nao waambukizwe surua. Watoto wenzako hawatakukubali na watakuchukia sana kama wakijua kwenu kuna surua lakini unaficha. Na ndio maana dunia inalia na China ikidhani labda ilificha uwepo wa corona.

Ni kweli nia ni njema ya kuwatoa watu hofu dhidi ya korona, lakini njia hiyo inakubalika kwa majirani, Africa na dunia? Je, ni kweli maombi yameiondoa covid-19 Tanzania, je ni kweli Tanzania sasa hakuna corona?

Madhara yake makubwa ya kufanya hivi ni kwamba tutaonekana kuwa ni waongo hata kwa mambo mengine yasiyo ya covid 19 huko mbeleni. Ni vema kuwa na mkakati wa pamoja wa kikanda kama vile East Africa, SADC au afrika kuliko kila nchi ikaogelea kivyake.
Sasa ndio naanza kuona picha jinsi Mussa alivyopata shida ktk kuwaongoza wana wa Israel kwenda Kanani kwa miaka 40! Binadamu ni pasua kichwa! We omba visa wafuate na ukafanye kama wanavyofanya! Na usitumie Tanzania wala watanzania! Fanya kivyakovyako tu!
 
Nia ni njema kivipi?
Ni njema kwakuwa anataka watu wake wasiwe na hofu kubwa mno iliyopitiliza, taifa halina uwezo wa kuwagawia chakula watu waliojifungia ndani, miradi inayoendelea isisimame, na watu waendelee kulipa kodi ili serikali iendelee kutoa huduma. Hii inachagizwa na hamu ya kufanya vizuri kwnye uchumi na upatikanaji wa chakula usiyumbe.

Lakini ubaya wake tunasahau kuwa ugonjwa huu unaua wote, haubagui rangi, jinsia, kabila, cheo, wapanga sera na mipango wala wapangiwa mipango. Ugonjwa huu unaweza kubakisha mahame tu watu wa familia nzima wakiwa wamekufa kwa muda mchache kabisa.

Kama sio lazima sana kwenda kijijini kwenu tafadhali usiende huko jamani ili kuepuka kusafirisha ugonjwa hadi kwaa mama na baba yako, shangazi, mjomba, ndugu na jamaa zako huko kijijini ambako hakuna miundombinu na huduma za afya za kutosha. Baki mjini bhana, wewe watumie hela tu kwenye simu, usiende jamani huko waache wacheze harusi wenyewe, wacha wazike wenyewe na wacha wauguze wengine.
 
Ni njema kwakuwa anataka watu wake wasiwe na hofu kubwa mno iliyopitiliza, taifa halina uwezo wa kuwagawia chakula watu waliojifungia ndani, miradi inayoendelea isisimame, na watu waendelee kulipa kodi ili serikali iendelee kutoa huduma. Hii inachagizwa na hamu ya kufanya vizuri kwnye uchumi na upatikanaji wa chakula usiyumbe.

Lakini ubaya wake tunasahau kuwa ugonjwa huu unaua wote, haubagui rangi, jinsia, kabila, cheo, wapanga sera na mipango wala wapangiwa mipango. Ugonjwa huu unaweza kubakisha mahame tu watu wa familia nzima wakiwa wamekufa kwa muda mchache kabisa.

Kama sio lazima sana kwenda kijijini kwenu tafadhali usiende huko jamani ili kuepuka kusafirisha ugonjwa hadi kwaa mama na baba yako, shangazi, mjomba, ndugu na jamaa zako huko kijijini ambako hakuna miundombinu na huduma za afya za kutosha. Baki mjini bhana, wewe watumie hela tu kwenye simu, usiende jamani huko waache wacheze harusi wenyewe, wacha wazike wenyewe na wacha wauguze wengine.
Safi sana, kama shida ni kuogopa kufanya lock down, kuna shida gani kuwaambia wananchi jamani huu ugonjwa upo, hatuwezi kulock down, lakini mnatakiwa kufuata masharti haya, kama ilivyokuwa mwaka jana, baada ya hapo yeye, waziri , katibu mkuu na serikali nzima iongee lugha moja. Shida iko wapi?
 
Safi sana, kama shida ni kuogopa kufanya lock down, kuna shida gani kuwaambia wananchi jamani huu ugonjwa upo, hatuwezi kulock down, lakini mnatakiwa kufuata masharti haya, kama ilivyokuwa mwaka jana, baada ya hapo yeye, waziri , katibu mkuu na serikali nzima iongee lugha moja. Shida iko wapi?
hata mm kero yangu imejikita hapohapo pa kusema Tz hakuna korona kabisa, maombi yamefanya muujiza wa kuangamiza corona sasa inakoromea kwingine huko
 
Back
Top Bottom