Pule
JF-Expert Member
- Apr 18, 2024
- 378
- 719
- Mmoja ya suala ambalo limekuwa tatizo kubwa ni UMASIKINI ambao umekithiri Kwa kiasi kikubwa Kwa WATANZANIA walio wengi na limekuwa ni tatizo sugu lisiloisha toka enzi hizo. Ili kuweza kupunguza au kuondoa umasikini kabisa ni lazima serikali kupanga na kuweka mikakati iliyothabiti ilikuweza kuondoa tatizo Hilo, mfano kuboresha nyanja zote za uchumi kama kilimo, biashara,miundombinu,kutafuta masoko ya uhakika ya ndani na nje ya nchi ilikuweza kuwahakikishia watu wanafanya kazi kwa kuboreshewa mazingira ya kazi husika.
- Ili kujenga Tanzania tuitakayo viongozi wanapaswa kutekeleza Yale wanayosema hasa katika masuala ya kiuchumi ilikuweza kumuezesha Kila mtanzania kuwa na uchumi mzuri na kuweza kufuta umasikini uliokithiri dhidi yetu. Viongozi wanatakiwa kuwa mstari wa mbele kutoa muongozo wa namna gani tunafnya kuukabli umasikini lakini imekuwa n tofauti na imebaki Kama stori tu hakuna utekelezaji na kama upo ni ule ule alioukuta kabla ya yeye kushika madaraka
- Ni vyema kuanza na viongozi ilikuweza kuleta Mwanga Kwa wananchi walio wengi Kwa namna ya kuwatoa kwenye umasikini uliokithiri na kuondokana na hali hii ya muda mrefu.
Upvote
1