Tanzania tumeambulia Medali 3 Jumuiya ya Madola Uingereza

Tanzania tumeambulia Medali 3 Jumuiya ya Madola Uingereza

Melubo Letema

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2020
Posts
416
Reaction score
414
Screenshot_20220807-003208.png

Baada ya Medali ya Kwanza ya Fedha kutoka Kwa Mwanariadha Alphonce Felix Simbu aliyoipata kwenye Mbio Ndefu Marathon Tarehe 30/07/2022, Leo Jioni Tanzania imehitimisha ngwe ya ndondi kwenye Michezo ya Jumuiya ya Madola kwa kupata medali mbili za shaba baada ya bondia wake wa pili Kassim Selemani Mbundwike kupoteza kwa pointi pambano lake la nusu fainali dhidi bondia wa Msumbiji jijini Birmingham, Uingereza.

Hivyo Tuna Medali ya Fedha Moja (Marathon) na Mbili za Shaba zote Ndondi (Boxing).

Wanariadha Wetu wa Mita 5000, Josephat Joshua Gisemo na Faraja Lazaro Damasi wamehitimisha Kwa kushika nafasi za 15 na 16 kati ya wanariadha 20, huku Mganda akichukua Medali ya Dhahabu na wakenya wakichukua medali za fedha na Shaba.

Nchi zinazoongoza Hadi Sasa
1. Australia -medali 155
2. Uingereza- Medali 148
3. Canada - Medali 84
 
Tuanzishe tuu mashindano ya kugegedana, labda hapo tutapata medali ya dhahabu🤣🤣🤣🤣

Yule waziri aliyefutaga michezo mashuleni ameturudisha nyuma kinoma.
Hata kugegedana sidhani kama tutatoboa. Maneno mengi, vitendo zero.

Labda umbeya, uchawa, mipasho, wizi, uzembe, rushwa, ubinafsi, ubabaishaji, hapo tunashinda asubuhi na mapema.
 
Tuanzishe tuu mashindano ya kugegedana, labda hapo tutapata medali ya dhahabu🤣🤣🤣🤣

Yule waziri aliyefutaga michezo mashuleni ameturudisha nyuma kinoma.
Kila waziri anakuja na Kanuni zake
 
Hata Sasa Hivi Hatuna waziri wa MICHEZO, tuna waziri wa utamadduni na Sanaa.
 
Hata kugegedana sidhani kama tutatoboa. Maneno mengi, vitendo zero.

Labda umbeya, uchawa, mipasho, wizi, uzembe, rushwa, hapo tunashinda asubuhi na mapema.
Aisee! So ata kugegeda hatujui🤣🤣🤣🤣🤣
 
Kwetu rushwa na connection vinatumaliza huwezi jua wangapi waliachwa na vipaji vyao kisa hawana connection,wapo walioachwa ili kundi la viongozi kwenye msafara wawe wengi huku wachezaji kidogo.

Nilishuhudia marathon moja aliyoshinda mganda akifatiwa na wakenya nikaona Tanzania hatupo serious kabisa,kale kajamaa kalikotuwakilisha kalienda kuuza sura tu
 
Kama nchi kuna wakati tulipotea na sasa ndio tunazidi kupotea, yaani hata Uganda wapo on top of us kwenye table ya medali, tatizo tunasifiana kwenye upumbavu na ujinga, why hatukujiandaa kuwatafuta warithi wa akina Ikangaa,Bali,Nyambui, Shahanga, Mwanjala?,halafu tulikua na wakimbiaji wazuri sana wa 200m na 100m ,what went wrong ndani ya nchi hii?,Kenya sasa wamewekeza kwenye mbio fupi na matunda wameanza kuyaona, sasa hivi watakua na the fastest man in the world!,tuendelee uzuzu
 
Kama nchi kuna wakati tulipotea na sasa ndio tunazidi kupotea, yaani hata Uganda wapo on top of us kwenye table ya medali, tatizo tunasifiana kwenye upumbavu na ujinga, why hatukujiandaa kuwatafuta warithi wa akina Ikangaa,Bali,Nyambui, Shahanga, Mwanjala?,halafu tulikua na wakimbiaji wazuri sana wa 200m na 100m ,what went wrong ndani ya nchi hii?,Kenya sasa wamewekeza kwenye mbio fupi na matunda wameanza kuyaona, sasa hivi watakua na the fastest man in the world!,tuendelee uzuzu
Tuanze na LAWAMA, Tuanze kupeleka lawama Wizara ya Michezo, Tuje Baraza la Michezo, tumalizie Kwa Mhuni TOC, chini ya Katibu Filbert Bayi, huyu Mzee hajawahi taka mtu wa kumpiku au kusifiwa Zaidi yake...AMEHARIBU RIADHA TANZANIA. inabidi Aondoke tu.
 
Tuanze na LAWAMA, Tuanze kupeleka lawama Wizara ya Michezo, Tuje Baraza la Michezo, tumalizie Kwa Mhuni TOC, chini ya Katibu Filbert Bayi, huyu Mzee hajawahi taka mtu wa kumpiku au kusifiwa Zaidi yake...AMEHARIBU RIADHA TANZANIA. inabidi Aondoke tu.
Exactly mkuu maisha ya sasa ni science na technology sio mazoea tuliyoyajenga ya kusifia sifia mediocrity
 
Kama nchi kuna wakati tulipotea na sasa ndio tunazidi kupotea, yaani hata Uganda wapo on top of us kwenye table ya medali, tatizo tunasifiana kwenye upumbavu na ujinga, why hatukujiandaa kuwatafuta warithi wa akina Ikangaa,Bali,Nyambui, Shahanga, Mwanjala?,halafu tulikua na wakimbiaji wazuri sana wa 200m na 100m ,what went wrong ndani ya nchi hii?,Kenya sasa wamewekeza kwenye mbio fupi na matunda wameanza kuyaona, sasa hivi watakua na the fastest man in the world!,tuendelee uzuzu
Kuna Vijana Wazuri waliachwa, ambao wangeongeza Medali...ila Nchi ya Connection, wamechaguliwa Kwa upendeleo kabisa....Riadha tuna Medali moja tu....
 
Exactly mkuu maisha ya sasa ni science na technology sio mazoea tuliyoyajenga ya kusifia sifia mediocrity
Tuanze kuifumua kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), iliyopo chini ya Wababe Wawili Henry Tandau na Filbert Bayi, wanawahonga BMT, Wizara wote Ili wasikilize wao.
 
Back
Top Bottom