Tanzania tumejifunza nini na kifo George Floyd?

Tanzania tumejifunza nini na kifo George Floyd?

Mwanahalisi20

Senior Member
Joined
May 5, 2020
Posts
132
Reaction score
152
Dunia imezizima, Africa imezimama na Marekani imezizima. Kifo cha Mmarekani mweusi Mr. George Floyd(48) kimebadilisha kabisa mwelekeo wa siasa za Kibaguzi si Marekani tu baali dunia nzima ikiwemo Tanzania.

Siasa za Kibaguzi zipo tu kila sehemu duniani. Kuna watu wanafikiri ubaguzi ni wa rangi tu. Ubaguzi ni ubaguzi tu na uko wa Aina tafauti Upo Ubaguzi wa rangi, jinsia, siasa, kabila, Ukanda n.k.

Tanzania ni nchi iliyo jijengea heshima kubwa Africa na dunia nzima kwa kupambana na Ubaguzi wa rangi hasa wakti wa Uhai wa Baba wa Taifa Mwl. Nyerere(RIP).

Lakini kwa hivi Karibuni Tanzania chini ya Uongozi wa CCM Awamu ya 5, tatizo la Ubaguzi limerudi nchini kwa Kasi ya ajabu. Ubaguzi huu umejikita kwenye Siasa za Kibaguzi zinazotekelezwa na CCM.

Serikali ya CCM Tanzania chini ya Rais John Joseph Pombe Magufuli. Kuanzia 2016 baada tu ya kuingia Ikulu, Magufuli alipiga marufuku Vyama vingine vya siasa kufanya chochote; marufuku kufanya mikutano nje na ndani, marufuku maandamano, marufuku vikao vya kichama nje na ndani, marufuku kufanya kampeni wakti wa Chaguzi ndogo za Udiwani na Ubunge.

Serikali ya CCM ikaanza Sera za kuwabana Viongozi wa Kisiasa toka Upinzani kwa kuwakamata na kuwaweka Mahabusu,kuwafungulia kesi Mahakamani na KUWAFUNGA jela.

Kifo cha George Floyd kiwe fundisho kwa Viongozi wa CCM na waache hi tabia. Uchaguzi Mkuu wa 2020 bado miezi 3 tu, shime kwa CCM na Serikali yake kukomesha ubaguzi huu Vinginevo Tanzania itaenda kugeuka America ya Africa na kitakuwa na kina George Floyd wengi Sana watatengezwa na Serikali hii ya Rais Magufuli kama Serikali ya Rais Trump wa Marekani ilivyo sababisha kifo Cha George Floyd.
 
Ndugu co kila mtu huweza kujifunza,hili watajifunza wale wenye kutumia akili zao ktk siasa na wala co wale wanaotumia siasa ktk akili zao.
 
Nimejifunza kuwa Binadamu na unafiki ni sawa na binadamu na damu
 
Hakuna askari wa Tanzania anayeweza kumuua mtu kwa mateso vile hadhari, huko US ubaguzi wao hautaisha bado wanawachukulia watu weusi kama watumwa tu, so usifananishe Wale wazungu makatili na sisi.
Wewe utakuwa mgeni sana Tz hii,akina mwagosi walifanywa nn?
 
Floyd was innocent, hakuwa na shida na mtu na wala hakumfanyia kitendo kibaya yule askari ambacho kingehalalisha atoe reaction ya vile kwa Floyd.
Na nyie muwe calm kama Floyd mkae nafasi yenu hakuna atakayewaletea bugudha.Tatizo nyie ni too much sasa.And mind you it's always harmful!
 
Hakuna askari wa Tanzania anayeweza kumuua mtu kwa mateso vile hadhari, huko US ubaguzi wao hautaisha bado wanawachukulia watu weusi kama watumwa tu, so usifananishe Wale wazungu makatili na sisi.
Kabisa, hata unaposikia Mtu kafia kituoni a.k.a central basi ujue ni Mtu kapigwa ki kwenzi tu akazimika.
 
Hakuna askari wa Tanzania anayeweza kumuua mtu kwa mateso vile hadhari, huko US ubaguzi wao hautaisha bado wanawachukulia watu weusi kama watumwa tu, so usifananishe Wale wazungu makatili na sisi.
Ujui chochote ukikua utaelewa,vipi wanakufa kwa kuteswa mahabusu wakilazimishwa kukiri makosa.
 
Floyd was innocent, hakuwa na shida na mtu na wala hakumfanyia kitendo kibaya yule askari ambacho kingehalalisha atoe reaction ya vile kwa Floyd.
Na nyie muwe calm kama Floyd mkae nafasi yenu hakuna atakayewaletea bugudha.Tatizo nyie ni too much sasa.And mind you it's always harmful!
Ile inaitwa ukatili wa polisi,kuna good policeman and bad policeman.
 
Hakuna askari wa Tanzania anayeweza kumuua mtu kwa mateso vile hadhari, huko US ubaguzi wao hautaisha bado wanawachukulia watu weusi kama watumwa tu, so usifananishe Wale wazungu makatili na sisi.

Vipi Hawa ni wazungu? Heri yao Askari akiuwa uchukuliwa hatua Africa anapandishwa cheo,Kama alikuwa Kusini anapelekwa kaskazini hivo hivo.
 

Attachments

  • tanzania-police-brutality.jpg
    tanzania-police-brutality.jpg
    17.6 KB · Views: 3
  • bg4.png
    bg4.png
    321.5 KB · Views: 2
  • ETGD4eHWoAIgxpL.jpg
    ETGD4eHWoAIgxpL.jpg
    66.2 KB · Views: 2
  • police-brutality-kenya.jpg
    police-brutality-kenya.jpg
    42.5 KB · Views: 3
  • _111686113_saspol2afp.jpg
    _111686113_saspol2afp.jpg
    44.3 KB · Views: 2
  • Mwili+wa++Daudi+Mwangosi+ukiwa+umechanika++vibaya.JPG
    Mwili+wa++Daudi+Mwangosi+ukiwa+umechanika++vibaya.JPG
    21.9 KB · Views: 2
  • daudi-mwangosi-remains.jpg
    daudi-mwangosi-remains.jpg
    40.6 KB · Views: 2
  • kenyaviolence1_051816051717.jpg
    kenyaviolence1_051816051717.jpg
    37.2 KB · Views: 2
  • brtsap.jpg
    brtsap.jpg
    16.6 KB · Views: 2
  • zimbabwe-police(1).jpg
    zimbabwe-police(1).jpg
    41 KB · Views: 3
  • zimbabwe-police(2).jpg
    zimbabwe-police(2).jpg
    41 KB · Views: 3
  • Screen-Shot-2015-03-13-at-10.03.02-PM-1024x650-1024x650(1).png
    Screen-Shot-2015-03-13-at-10.03.02-PM-1024x650-1024x650(1).png
    207.1 KB · Views: 2
  • Police-1.jpg
    Police-1.jpg
    88.9 KB · Views: 3
  • 396D7A51-FC7A-430A-B9F9-ECEF0C8C1319.jpg
    396D7A51-FC7A-430A-B9F9-ECEF0C8C1319.jpg
    190.9 KB · Views: 2
  • cop.jpg
    cop.jpg
    219.4 KB · Views: 2
  • e552Rpx9j8573b81671a00002f00c28b8c.jpeg
    e552Rpx9j8573b81671a00002f00c28b8c.jpeg
    38.9 KB · Views: 2
  • cop(1).jpg
    cop(1).jpg
    219.4 KB · Views: 2
  • Police-kick-child.jpg
    Police-kick-child.jpg
    26.8 KB · Views: 3
  • Ug+police.jpg
    Ug+police.jpg
    41.7 KB · Views: 2
  • 31kenya.3.jpg
    31kenya.3.jpg
    37.4 KB · Views: 3
Back
Top Bottom