Tanzania tunaachwa nyuma?

Tanzania tunaachwa nyuma?

Sijali

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2010
Posts
2,672
Reaction score
1,814
Ukiwauliza Wabongo wengi watakuambia duh, Tanzania twakata mbuga aisei, wengine wataisoma tu! Tuna barabara za juu kwa juu, mwendo kasi, SGR ya kisasa yaja....wataka nini tena?
Lakini waulize wengi kama wanajua kuna (hata Kiswahili chake sijui kama kipo):
1- Artificial Intelligence (AI) au (Akili Bandia)
2- Nano technology (Teknolojia ya vichembe)
3- Imagine technologies (Teknolojia nadharia)
4- Cloud computing (kuficha mawinguni)
5- Start-up businesses (Biashara chimbukizi)
6- Crypto currencies (Sarafu za kidigitali) (Bitcoin, Ethereum ...), Virtual currency, electronic wallets.... na matumizi yake.
7- Autonomous vehicles, drones (Gari zijiendeshazo, Droni)....
Na elimu au trend nyingine nyingi ambazo zina/ zitabadilisha kabisa dunia yetu. Vijana wengi hata wa form 6 waweza wasiwe na mwamko wa vitu hivi. Ukweli ni kwamba watu wachache wamediriki hata kusikia.
Ukienda kwa jirani zetu, Uganda, Kenya, Zambia Rwanda, utastaajabu jinsi wanavyojumuika kati na dunia.
Binafsi naona sababu halisi ya sisi kukatwa na dunia ni lugha na elimu duni.
Aidha, kuna umuhimu wa serikali kuwa na 'sera ya Digitali' ambayo wanatoa mafunzo ya hiari kwa wananchi. Pia ijenge Kituo cha kitaifa: National Centre for Artificial Intelligence. Tusije tukaamka siku moja na kukuta 'digital divide' (kubaguliwa kidijitali) baina yetu na nchi nyingine duniani kunakwamisha kabisa shughuli za maisha yetu.
Unaonaje?
 
Kama ushawahi kufika nchi zilizo endelea Tanzania ni sawa na kijijini kwa bi Mtori Mashulo.
 
Ukiwauliza Wabongo wengi watakuambia duh, Tanzania twakata mbuga aisei, wengine wataisoma tu! Tuna barabara za juu kwa juu, mwendo kasi, SGR ya kisasa yaja....wataka nini tena?
Lakini waulize wengi kama wanajua kuna (hata Kiswahili chake sijui kama kipo):
1- Artificial Intelligence (AI) au (Akili Bandia)
2- Nano technology (Teknolojia ya vichembe)
3- Imagine technologies (Teknolojia nadharia)
4- Cloud computing (kuficha mawinguni)
5- Start-up businesses (Biashara chimbukizi)
6- Crypto currencies (Sarafu za kidigitali) (Bitcoin, Ethereum ...), Virtual currency, electronic wallets.... na matumizi yake.
7- Autonomous vehicles, drones (Gari zijiendeshazo, Droni)....
Na elimu au trend nyingine nyingi ambazo zina/ zitabadilisha kabisa dunia yetu.
Ukweli ni kwamba watu wachache wamediriki hata kusikia. Ukienda kwa jirani zetu, Uganda, Kenya, Zambia Rwanda......vijana wengi hata wa form 6 waweza wasiwe na mwamko wa vitu hivi.
Binafsi naona sababu halisi ya sisi kukatwa na dunia ni lugha na elimu duni.
Aidha, kuna umuhimu wa serikali kuwa na 'sera ya Digitali' ambayo wanatoa mafunzo ya hiari kwa wananchi. Pia ijenge Kituo cha kitaifa: National Centre for Artificial Intelligence. Tusije tukaamka siku moja na kukuta 'digital divide' (kubaguliwa kidijitali) baina yetu na nchi nyingine duniani kunakwamisha kabisa shughuli za maisha yetu.
Unaonaje?
TRAB na TRAT..[emoji23]
 
Uko sahihi mkuu, ukienda South Africa utakuta vijana wadogo under 25 years wana utajiri mkubwa ambao kibongo bongo watakuita freemason kwa umri huo, simply ni forex na crypto currency zinawapa utajiri wa kutosha... bongo vijana wengi busy kubet
 
Tupo mitandaoni tunataka kutiba mpya yani tukiipata hiyo bongo kama peponi tunakuwa tumemaliza yani simple tu kama hivyo.
 
Back
Top Bottom