Tanzania tunahitaji foreign experts katika swala la katiba,wataalamu wetu wamepoteza credibility!

Tanzania tunahitaji foreign experts katika swala la katiba,wataalamu wetu wamepoteza credibility!

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Wakuu,

Katika kupata ufafanuzi na tafsiri sahihi juu ya mipaka na mamlaka ya bunge maalumu dhidi ya iliyokuwa tume ya katiba katika uandaaji wa rasimu ya katiba,bila shaka tunahitaji msaada ya wataalamu kutoka nje ambao watakuwa "neutral" na sio hawa wa ndani wenye maslahi binafsi katika jambo hili.

Nasema hivi kwasababu hivi sasa watanzania tunapotoshwa na hawa wanaojiita wataalamu wa sheria na mambo ya katiba.Wengi wao wanatoa maoni na ushauri wao si kwa misingi ya kuzingatia taaluma zao,bali kwa maslahi binafsi,kutumika na pengine hata kununuliwa kwa faida ya makundi fulani au taasisi wanazotoka au zilizowatuma.

Katika hili hata waandishi wa habari nao wanatumika kwa njia moja au nyingine ili tu malengo ya watu fulani katika jamii au taasisi fulani yatimie kwa kupata katiba wanayoitaka.

Ningekuwa na mamlaka ningesitisha zoezi hili na kualika wataalamu kutoka nje waje watupe ufafanuzi na maelezo ya msingi kabla hata ya bunge maalumu kutunga sheria na kanuni zitakazotumika katika bunge hilo na baadae waanze kuijadili rasimu hiyo.

Katika hatua tuliofikia na jinsi mambo yanavyokwenda,wataalamu wa ndani si wa kuaminika tena kwani wengi wao wamebeba agenda zao na za watu wao!
 
Je, wakinunuliwa kwa namna yoyote ile ili wajadili rasimu
au watoe ufafanuzi kwa matakwa ya huyo aliyewaleta?

Tanzania haikuingia kwa makosa kwenye maajabu 7 ya dunia....
 
Mkuu matumbo yao yanawasumbua awakumbuki walienda kufanya nini Dodoma.wao wameng'ang'nia posho km wataongwa kweli tutapata katiba nzuri
 
Pumba.fuuu kabisa! Hata Kenya wamethubutu na waliweza kupata new constitution sisi bado bongolala
 
Je, wakinunuliwa kwa namna yoyote ile ili wajadili rasimu
au watoe ufafanuzi kwa matakwa ya huyo aliyewaleta?

Tanzania haikuingia kwa makosa kwenye maajabu 7 ya dunia....

Hata hawa wa ndani ------------!

Wanapotosha taifa!

Experts hatujaanza kuwatumia leo kwahiyo inawezekana.
 
Hata hawa wa ndani ------------!

Wanapotosha taifa!

Experts hatujaanza kuwatumia leo kwahiyo inawezekana.

yawezekana wamefanya vizuri ktk nyanja mbalimbali lkn
nadhani katiba ni roho ya taifa la leo na vizazi vijavyo.
sio rahisi wageni wakawa na uzalendo kiasi cha kutusaidia
tukaziba mianya mingi ya wao kuja kuvuna mali zetu kwa jina la uwekezaji.

nadhani bado tunao wazawa wenye uzalendo but
somewhere somehow something went wrong during the appointment of the members
 
Pumba.fuuu kabisa! Hata Kenya wamethubutu na waliweza kupata new constitution sisi bado bongolala

sisi watanzania ni wabinafsi mno, na hapo ndio tumekulia kwenye siasa ya ujamaa, hivi tungekulia kwenye siasa za kibepari ubinafsi ungepitiliza vibaya mno.
 
Katiba ni ya watanzania, lazima itengenezwe na wenyewe.
Kama wajumbe wa bunge la katiba ni wapuuzi, mchakato usitishwe, mambo yarekebishwe, wapuuzi waondoke, tuanze upya.
Mawazo ya kutafuta wageni kutufanyia kila kitu ni ya kitumwa zaidi.
 
Mgogoro wa posho Bunge la Katiba unatudhihirishia kuwa kuna mafisadi wengi nchi hii. Wapo wanaopinga ufisadi kwasababu tu wapo nje ya system ila wakiingia kwenye system wanakuwa sehemu ya matatizo. Watu kama hawa waliojaa bungeni kupigania matumbo yao kamwe hawana uwezo wa kutusaidia kupata katiba mpya fikra zao wamezielekeza kwenye maslahi yoa binafsi, ni ajabu na kweli sijui tunakwenda wapi?

7744_10152206474802938_1857295675_n.jpg
 
Mkuu,

Nakubaliana na wewe kwenye suala la mchakato mzima wa katiba kutawaliwa na misingi ya kibinafsi na sio kitaifa. Kwamba wataalamu "waliohusika" moja kwa moja katika mchakato wametekwa kitaaluma na hawatumii utaalamu wao ni kweli kabisa. Ila tujikumbushe kuwa hata namna mchakato ulivyoandaliwa ulikuwa unalenga kutimiza matakwa hayo ya kibinafsi.

Sheria ya uundwaji wa tume ya katiba ilikuwa ina mapungufu mengi ya kimsingi
  • Tume ilikuwa sio ya wataalamu bali wateule wa wanasiasa;
  • Hakukuwa na vigezo vya sifa za wajumbe wa tume (CV zao hazijulikani)
  • Ikateuliwa kama kawaida - wanasiasa na wastaafu mashuhuri (sio lazima wataalamu) wakajazwa humo ili kuwapa ulaji wa mafao ya kustaafu au kupeana ulaji kindugu (kuna kijana mmoja ndugu yake Celina Kombani - aliyekuwa waziri wa sheria - yuko kwenye tume na ameshajijengea nyumba zake kadhaa na magari kiasi fulani)
  • Hadidu za rejea za kihuni
  • etc etc etc
Sheria ya bunge la katiba nayo ina mapungufu yake, yakilenga moja kwa moja uwezo wa bunge hilo kuwa la kisiasa hivyo kuuteka mchakato mzima kutoka kuwa wa kitaifa na kuwa wa kikundi fulani cha watu au taasisi:
  • Wabunge wote na wajumbe wa baraza la wawakilishi kuwa wajumbe wa Bunge maalumu la Katiba (Waheshimiwa hawa kwa ubinafsi wao walijua kuna ulaji kwenye bunge hilo hivyo wasingependa mwingine afaidi) - Ndiyo sababu hoja ya posho kuongezeka ikawa na kipaumbele;
  • Uteuzi wa wajumbe wa bunge hilo akaachiwa mtu mmoja anayewakilisha kundi fulani (Sishangai Kingunge kuwakilisha waganga wa kienyeji kwani hayo makundi maalumu hayakutajwa kwenye sharia ya Bunge la katiba; Shamim Khan anawakilisha dini gani jamani? Kwani hiyo dini anayowakilisha haina mwingine asiyekuwa mwanasiasa?
  • Bunge halina muwezeshaji mtaalamu (Sijui kama Spika wa bunge ni mtaalamu!) mada hazitaisha na hatujui kuwa hili bunge lina ukomo wa muda (Time barred). Baada ya hizo siku 70 zitaongezwa nyingine 70! usishangae. Na kazi isiishe ili tutengeneze posho nyingine miaka mitatu ijayo... ha ha ha.... Tutakuwa hapa Mungu akijaalia (Inshaallah) tutayaona.
Jamani, mimi nafikiri hata kama hiyo katiba itapitishwa, tutakuwa kama Ukraine. Itakuwa mbovu hadi miaka mitano ijayo tutaomba turudie ile ya mwaka 77! Ngoja tuone.

Hii ni hoja iliyodandiwa na chama tawala hawakuwa na clue waanzie wapi (Similar to BRN ambayo inaangamiza taifa kwa kupika data na kujifanya tumefanikiwa!)

Tungoje tuone yatakayojiri.

Ahsanteni
 
sio rahisi wageni wakawa na uzalendo kiasi cha kutusaidia
tukaziba mianya mingi ya wao kuja kuvuna mali zetu kwa jina la uwekezaji.

nadhani bado tunao wazawa wenye uzalendo s
Wenzetu wanafanyakazi ki-professional!
Si lazima akupende au aipende nchi, anachoangalia yeye ni kazi yake inamtaka afanye nini basi yeye hufanya.

Sasa hivi ninavyokuambia kuna nchi ya EU (jina ninalihifadhi) wanatafuta msaada wa wataalamu wa nje ya nchi ili wasaidiwe kufahamu imekuwaje wakaporomoka katika viwango vya elimu.

Hilo la kuvuna mali zenu hawana haja ya kutumia katiba wanajua kuwa wakitaka watawapata tu.

Sioni sababu ya kwa nini hili pendekezo lipuuzwe.
 
Umetoa rai nzur sana, wageni wakisimamia mchakato huu tutapata katiba iliyo bora.

Tukiwa tunamawazo ya kilakitu mkoloni,Muarabu kuna siku tusubiri kupigana mapanga.

Kiufupi hapa nusu na robo ya wajumbe wako kimaslahi.
 
Wenzetu wanafanyakazi ki-professional!
Si lazima akupende au aipende nchi, anachoangalia yeye ni kazi yake inamtaka afanye nini basi yeye hufanya.

Sasa hivi ninavyokuambia kuna nchi ya EU (jina ninalihifadhi) wanatafuta msaada wa wataalamu wa nje ya nchi ili wasaidiwe kufahamu imekuwaje wakaporomoka katika viwango vya elimu.

Hilo la kuvuna mali zenu hawana haja ya kutumia katiba wanajua kuwa wakitaka watawapata tu.

Sioni sababu ya kwa nini hili pendekezo lipuuzwe.

Umeongea vema mkuu.

Shivji,Werema,Warioba na wengineo wanatuchanganya na malumbano yao!
 
Yani UWEKEZAJI mpaka kwenye KATIBA?

Soon tutakuwa na KATIBA KWA HISANI YA WATU WA MAREKANI NA ULAYA.

Mkuu kwenye hili swala la katiba watu wanatumia profession zao kupotosha umma kwa maslahi yao.

Naposema foreign experts ninamanisha watu neutral,wakuaminika na wenye record nzuri lakini si hawa akina Werema na wenzake!
 
Watu wengine sijui vichwa vyao vimejaa vitu gani!!!
Mtu mzima anapost utumbo et watu wetu wamepoteza credibility! credibilities gani zilizopotea hadi tukahitaji experts?, Tz inawasomi wenye ueledi wa hali ya juu kiasi kwamba wao ndiyo ma-experts nje ya nchi kwa maswala mbalimbali. Kama hili halifahamu mleta hoja basi asome tafiti mbalimbali badala ya kuleta kichefu chefu humu janvini. Huyu huenda ni miongoni mwa -Wana Lumumba steet waliokolea kijani mioyono mwao.
 
Watu wengine sijui vichwa vyao vimejaa vitu gani!!!
Mtu mzima anapost utumbo et watu wetu wamepoteza credibility! credibilities gani zilizopotea hadi tukahitaji experts?, Tz inawasomi wenye ueledi wa hali ya juu kiasi kwamba wao ndiyo ma-experts nje ya nchi kwa maswala mbalimbali. Kama hili halifahamu mleta hoja basi asome tafiti mbalimbali badala ya kuleta kichefu chefu humu janvini. Huyu huenda ni miongoni mwa -Wana Lumumba steet waliokolea kijani mioyono mwao.

Hao unaowaona wanafaa si ndio mwanzoni walisema hakuna haja ya kuandika katiba mpya?!

Hivi wewe unaishi Tanzania ipi?!

Hivi kuna sheria ya hovyo kama hiyo sheria ya mabadilko ya katiba?!

Hivi msomi wa sheria anapokwambia eti Bunge la katiba linaweza kuja na rasimu mpya kabisa we unamuelewaje?!
 
Back
Top Bottom