Tanzania tunahitaji foreign experts katika swala la katiba,wataalamu wetu wamepoteza credibility!

Tanzania tunahitaji foreign experts katika swala la katiba,wataalamu wetu wamepoteza credibility!

Umeongea vema mkuu.

Shivji,Werema,Warioba na wengineo wanatuchanganya na malumbano yao!
Kati ya hawa unadhani nani yuko sahihi?Warioba anasema kuwa kisheria, rasimu hii ni maoni ya wananchi yanayopaswa kuboreshwa tu na si kubadilishwa! Werema anasema kuwa Bunge lile lina mamlaka ya kunyofoa vifungu na kuweka vipya isipokuwa ibara ya 9 tu! Jaji mstaafu John Ramadhani anamuunga mkono Warioba na Shivji anampinga Warioba. Mwisho itakuwaje? Wanaweza kuleta rasimu nyingine au wanajadili hii? Nini maana na hatma ya kupeleka kwa wananchi? Ni ili wananchi wapige kura kati ya rasimu hii na mawazo mapya bunge litakayopendekeza au?! Kwa mkanganyiko huu huenda tunahitaji hao foreign expert ingawa nadhani ni too late!
 
Kati ya hawa unadhani nani yuko sahihi?Warioba anasema kuwa kisheria, rasimu hii ni maoni ya wananchi yanayopaswa kuboreshwa tu na si kubadilishwa! Werema anasema kuwa Bunge lile lina mamlaka ya kunyofoa vifungu na kuweka vipya isipokuwa ibara ya 9 tu! Jaji mstaafu John Ramadhani anamuunga mkono Warioba na Shivji anampinga Warioba. Mwisho itakuwaje? Wanaweza kuleta rasimu nyingine au wanajadili hii? Nini maana na hatma ya kupeleka kwa wananchi? Ni ili wananchi wapige kura kati ya rasimu hii na mawazo mapya bunge litakayopendekeza au?! Kwa mkanganyiko huu huenda tunahitaji hao foreign expert ingawa nadhani ni too late!

Hawa wataalamu wetu wana agenda zao na wengine ------------ ndio maana wanatuyumbisha!
 
Wasomi wa nje wako neutral!!!!

Hakika nchi tumeichoka....

Hakuna watu wanatumikia nchi zao na mabepari kama wasomi wa nchi zilizoendelea...karudie research yako...



Watu wengine sijui vichwa vyao vimejaa vitu gani!!!
Mtu mzima anapost utumbo et watu wetu wamepoteza credibility! credibilities gani zilizopotea hadi tukahitaji experts?, Tz inawasomi wenye ueledi wa hali ya juu kiasi kwamba wao ndiyo ma-experts nje ya nchi kwa maswala mbalimbali. Kama hili halifahamu mleta hoja basi asome tafiti mbalimbali badala ya kuleta kichefu chefu humu janvini. Huyu huenda ni miongoni mwa -Wana Lumumba steet waliokolea kijani mioyono mwao.
 
Mimi sijali nani kasema nini...ila kama wanataka kuwajua watanzania basi hilo Bunge liingize mada zao....hii katiba ni ya watanzania na si ya hao so called wabunge wa Katiba....

Kwanza tunapoteza pesa bureeee Warioba alishamaliza kazi; wanajadili wanajadili kitu gani?????



Kati ya hawa unadhani nani yuko sahihi?Warioba anasema kuwa kisheria, rasimu hii ni maoni ya wananchi yanayopaswa kuboreshwa tu na si kubadilishwa! Werema anasema kuwa Bunge lile lina mamlaka ya kunyofoa vifungu na kuweka vipya isipokuwa ibara ya 9 tu! Jaji mstaafu John Ramadhani anamuunga mkono Warioba na Shivji anampinga Warioba. Mwisho itakuwaje? Wanaweza kuleta rasimu nyingine au wanajadili hii? Nini maana na hatma ya kupeleka kwa wananchi? Ni ili wananchi wapige kura kati ya rasimu hii na mawazo mapya bunge litakayopendekeza au?! Kwa mkanganyiko huu huenda tunahitaji hao foreign expert ingawa nadhani ni too late!
 
Wazo zuri sana ila ni kweli tunahitaji foreign experts?

Tunashindwa kujiendesha na kuamua mambo yetu bila matatizo kweli?

waafrica tunatia aibu sana

Bora mkoloni arudi aisee.
 
Waafrika wenyewe tuna mchango mkubwa sana kwenye kudidimiza maendeleo yetu ya kiuchumi, stability za mataifa yetu na evolution za kimawazo katika jamii, vizazi vya leo haviwatendei haki vizazi vyao vya baadae. Aiwezekani baada ya miaka 60 ya most african independencies the social thinking is almost the same, the causes of the problems are the same and the solutions are the same (by expecting external interference from our colonial masters).

Kwenye dunia za wenzetu on the same time scale the thoughts have evolved with time, mawazo ya babu wa kizungu si sawa na vijana wa leo in terms of morals, tolerance, political rightness and life-chances/opportunities available to the current young adults. Sisi kila siku tunaona kwenye dunia matatizo ya mawazo tofauti ndani ya jamii zingine yanavyoweza kuwa chanzo cha chaos lakini bado politicians are always using those circumstances to further their personal ambitions.

Kizazi cha leo kinajukumu la kurithisha mawazo mapya kizazi cha kesho, kama JKN aliweza kupigana kupunguza fikra za kidini na kuwabana watu wa dini nje ya siasa na kutumia nguvu nyingi sana kwenye propaganda za utaifa. Maraisi waliofuata walitakiwa kuelekea kulenga kwenye kupunguza na kutoa kabisa mawazo ya ukabila ndaani ya fikra za watu (maana ili swala aliepukiki, eventually we will have to get there, that is very important hili jamii kushirikiana kikamilifu, na wazungu walichomana moto hili kuwekana sawa na kufikia malengo hayo).

Sisi leo tupo kwenye karne ambayo kuna elimu na mambo yamesonga mbele ni kujifunza tu jinsi waliopo mbele yetu waliwezaje, hatuhitaji trial and error approach iliyowafikisha hapo jamii zilizoendela. Maana wao kama walichomana zamani, leo wameshajua kumwekea mtu mawazo si lazima kumwogopesha kwa azabu kali, unaweza kutumia mass media kueneza propaganda na sheria ambazo ni raisi kuzi monitor and to reinforce.

Sasa leo kiongozi anapewa jukumu la kuandika katiba, mwongozo ambao unaenda kukaa miaka na kwa faida ya kizazi cha baadae. Badala ya kufikiria kuwasaidia vipi watanzania kupata viongozi bora na watu ambao wanaweza kuwaweka accountable huko mbele wakiboronga, yeye anaenda kuweka agenda zake wakati yeye mwenye ni mpita njia tu hapa. Kwakuwa anajua matatizo ya leo, badala kulenga kufuta hayo mawazo au kupendekeza misingi mizuri anakuja na mapendekezo yenye kuchochea hayo mawazo ya mgawanyiko. Matokeo yake wanasiasa waliogawanyika kimtazamo kutokana na mapendekezo ya rasimu wamekuwa wanapangiana njama za kutafuta uhalali wa fikra zao kuonekana sawa mbele ya jamii huku wakitumia upande mdogo sana kwenye hoja zao kuelimisha kwanini wako si leo bali na kesho.

Kwenye kujiuliza kwetu sisi wananchi cha muhimu si kuangalia nani yuko sawa leo, cha muhimu ni mawazo ya nani yanamfikiria "Rajabu" na "John" watakaozaliwa in 2040, hawa watu Tanzania tunataka waikute na mazingira gani: bado yenye ukabila, udini, upendeleo, umaskini mkubwa. Sisi kizazi cha leo tunalenga nini kwa sasa kwa ajili ya hawa watu wa kesho kwa matendo yetu.

Utakuja kugundua swala kubwa na tatizo kubwa kwa sasa ni nguvu za raisi (kwenye katiba ya sasa, hili leo aliitajiki tena na muda wake umepita), kama tunataka kuweka misingi imara na kujenga utamaduni wa kukosoana na kushitakiana, umuhimu wa kuweka watu kutokana na sifa zao hili taifa lisonge mbele na kuwapa nafasi watu wenye mawazo na huwezo wa kutupeleka mbele. Inabidi tuanze leo, lakini sisi ndio kwanza tunaangaika na katiba yenye maswala ambayo si matatizo halisi zaidi ya mitazamo tofauti ya watu wachache. Wakati huo huo hakuna mtu anaefikiria raisi ajae hawe na sifa gani mfano kwa hali tuliyonayo hili tusogee mbele kwenye sifa za kiongozi tujali uzoefu wa mtu, au kazi zake alizofanya, mtu mwenye mawazo ya kesho na jinsi ya atakavyotusogeza etc.

Tunarudi palepale kwenye mawazo ya mleta mada, maana tumefikia hatua hatumianiani kwenye kulijenga taifa letu tunataka watu watoke nje kujakutusaidia, watu hao hao wenye malengo ya kuja kuchukua mariasili kwa kutmia mikataba isiyo na haki leo kwenye dunia ya biashara.

Kwa mtaji huu waafrika tuna safari ndefu sana, kama watu wa leo hatuwezi kuwaachia chochote watu wa kesho kukiendeleza zaidi ya mawazo ya chukichuki tu, tamaa na kupenda anasa bila ya kuwa na huwezo. Ubaya hapo ni kwamba tunataka kubomoa hata hatua chache tulizopiga na kuwarudisha nyuma zaidi kifikra vizazi vya baadae.
 
Waafrika wenyewe tuna mchango mkubwa sana kwenye kudidimiza maendeleo yetu ya kiuchumi, stability za mataifa yetu na evolution za kimawazo katika jamii, vizazi vya leo haviwatendei haki vizazi vyao vya baadae. Aiwezekani baada ya miaka 60 ya most african independencies the social thinking is almost the same, the causes of the problems are the same and the solutions are the same (external interference from our colonial masters).

Kwenye dunia za wenzetu on the same time scale the thoughts have evolved with time, mawazo ya babu wa kizungu si sawa na vijana wa leo in terms of morals, tolerance and political rightness. Sisi kila siku tunaona kwenye dunia matatizo ya mawazo tofauti ndani ya jamii yanavyoweza kuwa chanzo cha chaos lakini bado politicians are always using those circumstances to further their personal ambitions.

Kizazi cha leo kinajukumu la kurithisha mawazo mapya kizazi cha kesho, kama JKN aliweza kupigana kupunguza fikra za kidini na kuwabana watu wa dini nje ya siasa na kutumia nguvu nyingi sana kwenye propaganda za utaifa, maraisi waliofuata walitakiwa kuelekea kutoa kabisa mawazo ya ukabila ndaani ya fikra za watu (eventually we will have to get there, that is very important hili jamii kushirikiana kikamilifu, na wazungu walichomana moto hili kuwekana sawa).

Sisi leo tupo kwenye karne ambayo kuna elimu na mambo yamesonga mbele ni kujifunza tu jinsi waliopo mbele yetu waliwezaje, hatuhitaji trial and error approach iliyowafikisha hapo, maana wao kama walichomana zamani, leo wameshajua kumwekea mtu mawazo tumia mass media kueneza propaganda na sheria maana ni raisi kuzi monitor.

Sasa leo kiongozi anapewa jukumu la kuandika katiba, kitu ambacho kinaenda kukaa miaka na kwa faida ya kizazi cha baadae, anaenda kuweka agenda zake wakati yeye mwenye ni mpita njia tu hapa na anajua matatizo ya leo, badala kulenga kufuta hayo mawazo anakuja na mapendekezo yenye kuchochea hayo mawazo ya mgawanyiko. Wanasiasa tena imekuwa wanatafutiana njama za kutafuta uhalali wa namna zao ndio sawa.

Kwenye kujiuliza kwetu cha muhimu si kuangalia nani yuko sawa leo, cha muhimu ni mawazo ya nani yanamfikiria "Rajabu" na "John" watakaozaliwa in 2040, hawa watu Tanzania bado waikute yenye ukabila, udini, upendeleo, umaskini mkubwa. Sisi kizazi cha leo tunalenga nini kwa sasa kwa ajili ya hawa watu wa kesho kwa matendo yetu.

Utakuja kugundua swala kubwa na tatizo kubwa kwa sasa ni nguvu za raisi (kwenye katiba ya sasa, hili leo aliitajiki tena na muda wake umepita), hili tuanze kujenga misingi imara ya kukosoana na kushitakiana, kuanza kuweka watu kutokana na sifa zao hili taifa lisonge mbele na mawazo yenye kutupeleka mbele. Leo tunaangaika na katiba na maswala ambayo si matatizo halisi zaidi ya mitazamo tofauti ya watu wachache. Lakini hakuna mtu anaefikiria raisi ajae hawe na sifa gani mfano kwa hali tuliyonayo hili tusogee mbele kwenye sifa za kiongozi tujali uzoefu wa mtu, au kazi zake alizofanya, mtu mwenye mawazo ya kesho na jinsi ya atakavyotusogeza etc.

Tunarudi palepale kwenye mawazo ya mleta mada, maana tumefikia hatua hatumianiani kwenye kulijenga taifa letu tunataka watu watoke nje kujakutusaidia, watu hao hao wenye malengo ya kuja kuchukua mikataba isiyo na haki leo kwenye dunia ya biashara.

Kwa mtaji waafrika tuna safari ndefu sana, kama watu wa leo hatuwezi kuwaachia chochote watu wa kesho kukiendeleza zaidi ya mawazo ya chukichuki tu, kibaya zaidi tunataka bomoa hata hatua chache tulizopiga na kuwarudisha nyuma zaidi.

Huu ujumbe unastahili uwafikie wajumbe wote wa Bunge la katiba.Umeandika maneno ya busara sana na hasa kwa wanasiasa wetu wasiojua wajibu wao kwa taifa lao.
 
Happy Feet ulichofanikiwa ni kuandika maneno meeengi na kupoteza muda mwiingi bila kuandika chochote cha maana. jaribu kuyafanyia utafiti hayo uliyobwabwaja.
 
Nahisi kama tunakurupuka ktk suala la katiba. Sioni umakini na nia njema 100%. Hususan suala la rushwa, uongozi wa hovyo, mikataba ya rasilimali zetu na nation vision on earth n.k. Sijui ngoja tuone.
 
Mimi sijali nani kasema nini...ila kama wanataka kuwajua watanzania basi hilo Bunge liingize mada zao....hii katiba ni ya watanzania na si ya hao so called wabunge wa Katiba....

Kwanza tunapoteza pesa bureeee Warioba alishamaliza kazi; wanajadili wanajadili kitu gani?????

I hate to say this, hata bunge likiingiza mada zake watanzania hawatafanya chochote.
 
Wakuu,

Katika kupata ufafanuzi na tafsiri sahihi juu ya mipaka na mamlaka ya bunge maalumu dhidi ya iliyokuwa tume ya katiba katika uandaaji wa rasimu ya katiba,bila shaka tunahitaji msaada ya wataalamu kutoka nje ambao watakuwa "neutral" na sio hawa wa ndani wenye maslahi binafsi katika jambo hili.

Nasema hivi kwasababu hivi sasa watanzania tunapotoshwa na hawa wanaojiita wataalamu wa sheria na mambo ya katiba.Wengi wao wanatoa maoni na ushauri wao si kwa misingi ya kuzingatia taaluma zao,bali kwa maslahi binafsi,kutumika na pengine hata kununuliwa kwa faida ya makundi fulani au taasisi wanazotoka au zilizowatuma.

Katika hili hata waandishi wa habari nao wanatumika kwa njia moja au nyingine ili tu malengo ya watu fulani katika jamii au taasisi fulani yatimie kwa kupata katiba wanayoitaka.

Ningekuwa na mamlaka ningesitisha zoezi hili na kualika wataalamu kutoka nje waje watupe ufafanuzi na maelezo ya msingi kabla hata ya bunge maalumu kutunga sheria na kanuni zitakazotumika katika bunge hilo na baadae waanze kuijadili rasimu hiyo.

Katika hatua tuliofikia na jinsi mambo yanavyokwenda,wataalamu wa ndani si wa kuaminika tena kwani wengi wao wamebeba agenda zao na za watu wao!
Tanzania ina wataalamu wa aina mbalimbali tena wenye ubora wa kimataifa ingawa baadhi yao ni wababishaji. Kuwepo kwa wababaishaji ni jambo la kawaida, ila siyo kweli kuwa Watranzania wote ni wababaishaji.

Tratizo la Watanzania wa leo ni njaa, tamaa ya mali na ubinafsi. Kila mmoja anafaikiria zaidi atafaidika na jukumu hilo kimsahai binafsi. Wengine wao kwa kujua kuwa pesa iko serikalini ambako kunatawaliwa na CCM wako tayari kufanya lolote kuifurahisha CCM ili wapate maslahi yao binafsi.


Uundwaji wa Katiba ya Kenya, pamoja na mapungufu yake haukutuwawaliwa na tamaa binafsi za pesa au madaraka kwa vile ilihusisha watu wa nje ya nchi. Lakini hapa Tanzania naona pesa na madaraka ndivyo vinavyotawala mchakato wote. Kwa hiyo nina wasiwasi kuwa Katiba hii itakuwa ni viraka tu.
 
Wakuu,

Katika kupata ufafanuzi na tafsiri sahihi juu ya mipaka na mamlaka ya bunge maalumu dhidi ya iliyokuwa tume ya katiba katika uandaaji wa rasimu ya katiba,bila shaka tunahitaji msaada ya wataalamu kutoka nje ambao watakuwa "neutral" na sio hawa wa ndani wenye maslahi binafsi katika jambo hili.

Nasema hivi kwasababu hivi sasa watanzania tunapotoshwa na hawa wanaojiita wataalamu wa sheria na mambo ya katiba.Wengi wao wanatoa maoni na ushauri wao si kwa misingi ya kuzingatia taaluma zao,bali kwa maslahi binafsi,kutumika na pengine hata kununuliwa kwa faida ya makundi fulani au taasisi wanazotoka au zilizowatuma.

Katika hili hata waandishi wa habari nao wanatumika kwa njia moja au nyingine ili tu malengo ya watu fulani katika jamii au taasisi fulani yatimie kwa kupata katiba wanayoitaka.

Ningekuwa na mamlaka ningesitisha zoezi hili na kualika wataalamu kutoka nje waje watupe ufafanuzi na maelezo ya msingi kabla hata ya bunge maalumu kutunga sheria na kanuni zitakazotumika katika bunge hilo na baadae waanze kuijadili rasimu hiyo.

Katika hatua tuliofikia na jinsi mambo yanavyokwenda,wataalamu wa ndani si wa kuaminika tena kwani wengi wao wamebeba agenda zao na za watu wao!

Mbona unawaponda mawakili wasomi wetu?
 
Back
Top Bottom