Tanzania tunapaswa kuwa na sheria kali dhidi ya viongozi mafisadi na wala rushwa

Tanzania tunapaswa kuwa na sheria kali dhidi ya viongozi mafisadi na wala rushwa

Mdude_Nyagali

Member
Joined
Dec 11, 2022
Posts
79
Reaction score
1,444
Kwa huu ufisadi wa mawaziri na watendaji wengine unaoendelea nchini, ningekuwa Rais ningeukomesha ndani ya siku 100 za mwanzo katika uongozi wangu. Ningetunga sheria ya ufisadi na uhujumu uchumi ambayo ufisadi unaozidi mabilion adhabu yake ni kifo.

Kwamba kesi za namna hiyo sheria itaweka wazi kuwa zisikilizwe ndani ya siku 18 hii ni pamoja na rufaa. Baada ya hukumu ya mwisho mfungwa anapaswa kunyongwa ndani ya saa 48.

Kwamba vyombo vya habari vitaruhusiwa kurusha moja kwa moja mwenendo mzima wa kesi ili kuwapa nafasi wananchi kufuatili kesi ya mwizi wao na hukumu atakayopewa.

Kutakuwa na eneo maalumu pale Dodoma ambalo litatengwa kwa ajili ya kuzika mafisadi. Makaburi yao yataandikwa majina yao na kiasi cha ufisadi alioufanya. Hii ni kwa ajili ya kumbukumbu ya vizazi na wananchi watakaotembelea makaburi hayo kwa ajili ya kutalii.

Kwamba mkuu wa magereza Tanzania CGP atapewa mamlaka na sheria kunyonga wafungwa wa ufisadi na uhujumu uchumi ndani ya saa 48 tangu hukumu ya mwisho kutolewa kama mhusila alikata rufaa. Wala haitasubiri Rais kusaini.

Mdude Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.

====

Pia soma:

- Luhaga Mpina: Usambazaji wa sukari haukuwa ukifanywa na mfanyabiashara mmoja wa Mwanza pekee, Waziri Bashe alidanganya

- Luhaga Mpina: Waziri Bashe na Mwigulu walitengeneza uhaba wa sukari nchini, zilikuwa njama za kuiba mapato ya nchi
 
Uchaguzi wa kikanda wenyewe ulisheheni rushwa na ufisadi wa kutisha, chadema is uselessly! Tunahukumu haya mambo as if kuna ushahidi wa kina juu ya hili,wahusika wajitokeze watoe maelezo yao!..
 
Nani ataisimamia hio Sheria sasa maana bongo Sheria ni biashara.

Jela ni kwa ajili ya watu masikini
 
Nchi haiwezi kuongozwa hivi.

Inaamana mbowe nayeye anyongwe Kwa Kula pesa za lowasa na za mama Abdul??
Mbona umepanic mkuu. Shida ikowapi kama wewe siyo fisadi?

Au ndo wenyewe mko nyuma ya fake id?!
 
Kwa huu ufisadi wa mawaziri na watendaji wengine unaoendelea nchini, ningekuwa Rais ningeukomesha ndani ya siku 100 za mwanzo katika uongozi wangu. Ningetunga sheria ya ufisadi na uhujumu uchumi ambayo ufisadi unaozidi mabilion adhabu yake ni kifo.



View attachment 3018727
Na waliopewa dhamana wanao ahirisha kufikiri Kwa nafsi, (human herding)
 
Nchi haiwezi kuongozwa hivi.

Inaamana mbowe nayeye anyongwe Kwa Kula pesa za lowasa na za mama Abdul??
Tu-ashumu kuwa ujinga na upumbavu unaotembea kwenye kichwa chako kuwa Freeman Mbowe alipokea pesa za Lowassa na Mama Abdul ni kweli..

Sasa huyu anyongwe kwa sababu gani maana hajaiibia serikali, amepewa na watu binafsi kwa hiari yao (hata kama ni kweli, japo ni ujinga na uongo wako tu)??

Mdude_Nyagali anaongelea viongozi wanao divert pesa za umma kama hawa Bashe, Mwigulu na Bi Tozo ambao kupitia sukari wame - divert pesa za kodi ya serikali tokana import ya sukari zaidi ya Billion 600..!

Hawa ndiyo wanastahili adhabu kali ya namna hiyo..!!
 
Kwa huu ufisadi wa mawaziri na watendaji wengine unaoendelea nchini, ningekuwa Rais ningeukomesha ndani ya siku 100 za mwanzo katika uongozi wangu. Ningetunga sheria ya ufisadi na uhujumu uchumi ambayo ufisadi unaozidi mabilion adhabu yake ni kifo.



View attachment 3018727
Mozambiq wameendesha kesi za ufisadi live miezi 15 na bado wakafungana miaka ya kiushikaji hayo uyasemayo kwa kuwa tu una njaa lakini kwa uzalendo huna!
 
Uchaguzi wa kikanda wenyewe ulisheheni rushwa na ufisadi wa kutisha, chadema is uselessly!
Tunahukumu haya mambo as if kuna ushahidi wa kina juu ya hili,wahusika wajitokeze watoe maelezo yao!..
Inchi inafilisiwa wewe unaendekeza mizaha isiyokua na tija kwani uvccm mchawi wenu ni kiziwi?
 
Shida sio sheria kali bali ni viongozi wenye uthubutu wa kusimamia hizo sheria wakijitokeza mnawaita dictator na kuwatukana
 
Nani
Kwa huu ufisadi wa mawaziri na watendaji wengine unaoendelea nchini, ningekuwa Rais ningeukomesha ndani ya siku 100 za mwanzo katika uongozi wangu. Ningetunga sheria ya ufisadi na uhujumu uchumi ambayo ufisadi unaozidi mabilion adhabu yake ni kifo.

Kwamba kesi za namna hiyo sheria itaweka wazi kuwa zisikilizwe ndani ya siku 18 hii ni pamoja na rufaa. Baada ya hukumu ya mwisho mfungwa anapaswa kunyongwa ndani ya saa 48.

Kwamba vyombo vya habari vitaruhusiwa kurusha moja kwa moja mwenendo mzima wa kesi ili kuwapa nafasi wananchi kufuatili kesi ya mwizi wao na hukumu atakayopewa.

Kutakuwa na eneo maalumu pale Dodoma ambalo litatengwa kwa ajili ya kuzika mafisadi. Makaburi yao yataandikwa majina yao na kiasi cha ufisadi alioufanya. Hii ni kwa ajili ya kumbukumbu ya vizazi na wananchi watakaotembelea makaburi hayo kwa ajili ya kutalii.

Kwamba mkuu wa magereza Tanzania CGP atapewa mamlaka na sheria kunyonga wafungwa wa ufisadi na uhujumu uchumi ndani ya saa 48 tangu hukumu ya mwisho kutolewa kama mhusila alikata rufaa. Wala haitasubiri Rais kusaini.

Mdude Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.

====

Pia soma:

- Luhaga Mpina: Usambazaji wa sukari haukuwa ukifanywa na mfanyabiashara mmoja wa Mwanza pekee, Waziri Bashe alidanganya

- Luhaga Mpina: Waziri Bashe na Mwigulu walitengeneza uhaba wa sukari nchini, zilikuwa njama za kuiba mapato ya nchi
atakaye zitunga na kisha kuzipitisha hizo sheria kali atakuwa ametokea wapi ???🙄😳
 
Back
Top Bottom