Tanzania vs Guinea: Tanzania yaaga mashindani baada ya kutoka sare ya mabao 2 kwa 2 dhidi ya Guinea

Sio tu mpira binafsi naamini hatuna watu wenye vipaji vya soka wewe angalia marefa,makocha,wachezaji wetu nk nk wangapi wako nchi za nje kulinganisha na nchi ndogo kama Burundi na Rwanda kwa mfano?...
Only way ya kubadilisha mpira wetu ni kuwekeza kwa vijana na makocha....mie ndio maana nawakubali sana wataliano...sawa watu wanasema ligi lao sio zuri but the majority of the coaches kule ni wataliano na wanawapromote makocha wao ndio mpaka wanaweza kwenda nje ya italia na kutamba.

Hapa tunatakiwa tuweke mkakati kuwa national team itafundishwa na wazawa tuu. Foreigner atakuja nchini kuwafundisha makocha lakini aio kufundisha national teams au the majority of the clubs.
 
Sasa mkuu hao vijana wanatoka wapi?kila kitu kwetu ni kuomba kudra tu!!yaani hata mambo ya kisayansi tunataka kubahatisha batisha tu!!hii nchi mpira hakuna hayo mambo ya usimba na uyanga ndio yanatutia ujinga na kuaminishwa kuwa hata timu gani ikija haitoki!!tunaendeshwa na kauli mbiu!!"ETI ZAMU HII AFE BEKI AFE KIPA, FULANI HATOKI"(slogan za kilimo kwanza)uzitumie kwenye soka!!!Tena sasa tangazo hilo apewe nugaz, daaa!!utadhania timu yenyewe ni ile brazil ya 1994!!!halafu ukitokea ukasema ukweli, utaambiwa wewe sio mzalendo!!halafu usishangae wakapokelewa kishujaa eti kutoka sale na guinea , sio mchezo!!!juzi wanajisifu eti ubora wa ligi africa ni wa 8!!sasa CHAN, timu nyingi wachezaji wao wa kutegemewa wako ligi za nje, Tz, karibu asilimia 99, ni wa hapa hapa mmeshindwa!!timu ya taifa nayo eti unatafuta balance ya wachezaji, ili isionekane ni ya upande mmoja!!utadhania labda ni nyadhifa za kisiasa, mbona congo dr, karibia asilimia 100, wametokea AS VITAR?
KWANI LAZIMA MPIRA TU, TWENDENI KWENYE NGUMI.
 
Exactly, unge change tech bench la hizi timu Tz ingeshinda! Hata Matola ananipa wasiwasi sana sasa
Sio matola tu hata juma mgunda hakuna kitu , matola alienda na Simba Mapinduzi cup lakini simba ilikuwa inashinda kwa uwezo binafsi wabwachezaji timu haikuwa na muunganiko wowote.
Tusikimbilie kusema tunataka makocha wazeee bali makocha inabidi wasome na watafute timu za kufundisha nje ya nchi tunashindwa hata kutoa marefa halafu tunakimbilia hoja ya uzawa
 
Roho yaniuma kocha m*seng* sana yule pamoja namatola wake Yani Tolla boy katulia tuli kudadeki zao
 
hata hii unateseka?
 
Hii nchi haina vipaombele ndio maana kuanzia kwenye siasa Hadi michezo hakuna tunakofanya vizuri

Kama tunataka kubadili mpira wa timu ya Taifa na kuuza wachezaji tufanye ulivyoshauri ila kama tunataka kuuza ligi yetu kibiashara tuende na mtindo wa sasa wa kutegemea wachezaji wa kigeni so ni lazima tuchague njia tunayotaka Ili tusiwe looser kwa kila kitu
 
Kuna kitu kikubwa wachezaji wetu wanakosa, Kuna kitu kinaitwa "Football intelligence" sijui neno fasaha kiswahili ni ile hali yakujuwa au kusoma mchezo kabla ya tukio. wachezaji wetu hawana hii kitu. Unajuwa kabisa unaongoza goal 2 na utakuwa umepita na unawaona wapinzani wako wanakuja speed sababu wanataka goal wanajuwa draw nzuri kwao sisi draw mbaya ndio maana tukaona baada ya kuwafunga goal la 2 tukawaona Guinea tofauti speed sasa badala ya kuwasoma hawa wana moto ngoja to slow game kwa vipasi vya maudhi na kujiangusha kufanya mambo ili wapanick ndio kwanza tukaanza kucheza ngoma yao wanapiga sebene na sisi tunacheza sebene baada ya kucheza blues, tukaanza kubutua tu wanakuja tukipata tunapiga tu kwao wanakuja tena unaona kabisa goal linakuja. Hapo ndio intelligence inaonekana slow game piga square pass huku na huku kama mnaenda mbele wakirudi nyuma tu nyinyi mnaanza kwa kipa wenu bahati tukawa kama tunacheza league zetu ukija piga tu wanakuja piga wanakuja. wakapata goal wakaanza kutuudhi kujitupa hizo ndio akili. akili hizo hazikuwa na wachezaji wetu wala kocha kuwaelekeza wabadilike. Mimi nadhani hiyo ndio tofauti kubwa sana baina ya sisi na wao. Lazima tujuwe sisi ni kama team kamili maana hatuchezi sana nje wao wale ikija team yenyewe kama kina Nabby Keita hawa wote wanakaa bench ndio ujuwe bado sana sisi.
 
kwa mara ya kwanza Jana nimetoa machozi kwa uchungu wa kufungwa bao la 2 , nilihisi nimechomwa ktk moyo wangu. nilishindwa kuelewa haswa nini kiliwatokea wachezaji wa taifa stars wakati wakiwa wanaonhoza kwa bao 2 na dakika zilikuwa zime yoyoma wakashindwa kutumia mbinu za kuchelewesha na kupelekea presha kubwa kwenye goli lao na hatimaye kufungwa?!!!
nimeumizwa sana
 
Forward kuwa Nchimbi heri kocha angeweka debe la viazi kwenye namba ya Nchimbi tungejua ni viazi
Giroud kombe la dunia alifunga magoli mangapi? Kwaajili taarifa yako bila Nchimbi na ule usumbifu wake pale mbele inawezekana tungekufa mapema tu,yes hey ndiye forward inatakiwa afunge,Ila huwezi kubeza kazi yake pale mbele
 
Uko sahihi mkuu,sisi wachezaji wetu hawana basics na principle's za football
 
Hakuna kufurahia mnataka mafanikio kwa kutia tia maji.

Icho kitu hakipo mpira wa bongo umeandamwa sana na siasa na mihemko.

Wekeni long term plan za kukuza nyamja ya mpira ila si kukurupuka na kuzima moto kila mashindano.

Tusipobadilika maisha yetu yatakuwa hivi hivi kwa kipindi kirefu.
Kwa hivyo umefurahui sio
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…