SautiYaMnyonge
JF-Expert Member
- May 13, 2018
- 439
- 742
Wazawa wameamua kurudi kuwekeza nyumbani!
Kiwanda cha Shafa Tanzania Investment ni kiwanda cha aina yake Afrika Mashariki na kipo Wilayani Mkuranga, Pwani. Katika ziara ya Waziri @AngellahKairuki imeelezwa kuwa kiwanda kinamilikiwa na wazawa.
Wazawa hawa ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakiwekeza nje ya nchi, lakini kwa kutambua umuhimu wa kuendeleza nyumbani, wawekezaji hawa wameamua kuja nyumbani ili kuunga mkono matamanio ya Mhe. Rais @MagufuliJP yanayohimiza ujenzi wa viwanda ili kufikia uchumi wa kati.
Mradi umeanza mwaka 2018 na tayari asilimia 90 ya ujenzi imekamilika ikijumuisha kiwanda na ghala.
Kiwanda kitawekeza takribani shilingi bilioni 18 mpaka kukamilika na utazalisha vifaa vya ujenzi ikiwamo tofali 'concrete blocks', 'perving blocks' na 'carb stones'.
Vifaa vya ujenzi viavyozalishwa katika kiwanda hiki vitakuwa na ubora wa hali ya juu kutokana na matumizi ya tekinolojia hii kutoka Ujerumani ijulikanayo kama 'Massa'. Kwa kuzingatia hilo kiwanda cha Shafa kimejipanga kuzalisha kiasi kikubwa cha vifaa, kwa bei nafuu,kwa muda mfupi.
Vifaa vitakavyozalishwa vitafaa kutumika kwenye ujenzi wa barabara, viwanja vya ndege, bandari, majengo makubwa na majengo madogo. Hivyo wateja wakubwa na wadogo watanufaika na uwekezaji huu.
#T2020JPM
Sent using Jamii Forums mobile app
Kiwanda cha Shafa Tanzania Investment ni kiwanda cha aina yake Afrika Mashariki na kipo Wilayani Mkuranga, Pwani. Katika ziara ya Waziri @AngellahKairuki imeelezwa kuwa kiwanda kinamilikiwa na wazawa.
Wazawa hawa ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakiwekeza nje ya nchi, lakini kwa kutambua umuhimu wa kuendeleza nyumbani, wawekezaji hawa wameamua kuja nyumbani ili kuunga mkono matamanio ya Mhe. Rais @MagufuliJP yanayohimiza ujenzi wa viwanda ili kufikia uchumi wa kati.
Mradi umeanza mwaka 2018 na tayari asilimia 90 ya ujenzi imekamilika ikijumuisha kiwanda na ghala.
Kiwanda kitawekeza takribani shilingi bilioni 18 mpaka kukamilika na utazalisha vifaa vya ujenzi ikiwamo tofali 'concrete blocks', 'perving blocks' na 'carb stones'.
Vifaa vya ujenzi viavyozalishwa katika kiwanda hiki vitakuwa na ubora wa hali ya juu kutokana na matumizi ya tekinolojia hii kutoka Ujerumani ijulikanayo kama 'Massa'. Kwa kuzingatia hilo kiwanda cha Shafa kimejipanga kuzalisha kiasi kikubwa cha vifaa, kwa bei nafuu,kwa muda mfupi.
Vifaa vitakavyozalishwa vitafaa kutumika kwenye ujenzi wa barabara, viwanja vya ndege, bandari, majengo makubwa na majengo madogo. Hivyo wateja wakubwa na wadogo watanufaika na uwekezaji huu.
#T2020JPM
Sent using Jamii Forums mobile app