Tanzania Yachomoa Kusaini Mkataba wa EPA

Tanzania Yachomoa Kusaini Mkataba wa EPA

wapi hata tunapochomoa tujulikne basi nini hasa twafanya sio kuzubaa zubaa tu kindaki ndaki
 
Shida hamjielewi intelligence yenu hovyoo tu, huwa anasema amezaliwa nzega,lakini birth certificate serial number yake na hospitali alipozaliwa birth record number hazifanani!, yaani ata mimi naweza kuja kugombea kiti cha ubunge hapo bongo maana nakifaham kiswahili! Tukipiga stori na wasomali huwa wanacheka sana, wanakwambia shamba la bibi afrika yetu linajulikana tu. Anyway nisiseme mengi tukamletea shida mbunge 'wenu' mpendwa bashe, alipozaliwa tutawaambieni siku nyingine tu.
Useless
 
Wakuu, naomba nitangulie kwa kujitambulisha kuwa mimi ni muafrika, mzaliwa na raia wa Tanzania. Pili mimi si mwanauchumi wala mwanasheria kwa hiyo uchambuzi wangu ni kwa uelewa wa mwananchi asiye na taaluma hizo mbili. Nimejaribu kusoma chambuzi kwenye vyombo vya habari, mkataba wenyewe na muhtasari mbalimbali wa mikataba hiyo ya EPA.

Nikijikita kwenye mada yenyewe:
- Moja, kwa uelewa wangu mikataba yoyote ile lazima kuna majadiliano ya pande husika. Kwa maana hii mikataba hii ilijadiliwa nchini kwetu, kisha Tanzania na wanachama wenza wa EAC, hadi hatua ya EAC na EU.
- Pili, majadiliano ya mikataba hii yalichukua zaidi ya miaka kumi, tangu enzi za Mh. Rais Mstaafu William Mkapa mpaka mwaka 2014.
- Tatu, kulikuwa na hatua mbalimbali ambazo kabla hujavuka kila hatua, lazima maridhiano ya pande zote mbili yafikiwe. Mpaka hatua iliyofikiwa sasa wanachama wote wa EAC na EU waliridhia mikataba hii kwa kuweka sahihi Oktoba 2014, ikimaanisha kuwa wanachama wa pande zote mbili (EAC na EU) wameridhia mikataba hiyo na hakuna nafasi tena ya kubadilisha yaliyomo zaidi ya kuhakiki lugha kabla ya sahihi za nchi wanachama (ratification).
- Nne, katika hatua zote Tanzania ilikuwa na jopo la wataalam wake na viongozi wa Serikali katika ngazi mbalimbali waliohusishwa na waliochangia katika kuandaa mikataba hii; kwanzia ngazi ya taifa, ukanda wa EAC na kati ya jumuiya hizi mbili. Wengine walisafirishwa na kwenda Brussels kwenye mafunzo ya mikataba, majadiliano, nk.

Kwa mantiki hiyo, kwa nini hoja ya kupinga mikataba hii tunaisikia katika hatua hizi za mwisho? Kwa nini katika hoja hizo hatuwasikii wale wataalam na viongozi waliohusishwa wakizungumza? Je, wao waliona makosa hayo tangu mwanzo au yamekuja kufahamika hatua ya kumalizia ng'ombe mkia?

Ninashangaa sana kuwalaumu wazungu kwenye jambo tuliloshirikishwa tangu mwanzo. Kama tunao uwezo wa kukataa katika hatua hii, je tulishindwaje kukataa katika hatua zilizopita? Tena tunawasema kuwa wanaturudisha kwenye ukoloni. Tukumbuke hawa wenzetu hawako kwenye kutoa misaada tu, bali kutengenezea nchi zao vyanzo vya mapato. Tunahitaji tuache mawazo ya kujinyongesha na kuona tunastahili tu misaada kwa sababu ya historia; tunajigeuza watumwa na tutaendelea kubaki watumwa wa mawazo yetu.

Halafu hatuwasikii wazungu wakilizungumzia hili wala kutupa upande wa pili. Hivyo nikajitahidi kupitia vyanzo nilivyokuta kwenye mtandao kufuatilia zaidi. Mkataba nimeukuta hapa:
http://trade.ec.europa.eu/doclib/docs/2015/october/tradoc_153845.compressed.pdf

Tafadhali kama kuna wataalam wa Uchumi na Sheria, nikotayari kukosolewa na kueleweshwa (bila matusi tafadhali). Ila nimepata yafuatayo:

Kulikuwa na hoja ya Mh Zitto Kabwe, kuwa nchi itakosa vyanzo vya mapato kwa kutotoza ushuru. Kwanza nchi za EAC zitafungua milango yake baada ya miaka saba kwa baadhi ya bidhaa za Ulaya hadi baada ya miaka 25 kwa bidhaa takribani asilimia 82, bila kutoza ushuru wa forodha. Bidhaa hizo pia zinatakiwa ziwe kitu tunachozalisha nchini. Kipengele cha tatu Ibara ya 100 ya mkataba huo kinasema kuwa EU itatoa rasilimali fedha kujazia hasara serikali itakayoingia kutokana na kukosa mapato yatokanayo na kuondoa au kupunguza ushuru wa forodha

upload_2016-11-10_18-2-32.png


Vile vile ibara hiyo hiyo ya 100 inazipa nafasi nchi wanachama wa EAC, kupitia mikataba hii, nafasi ya kuboresha au kuendeleza sekta za uzalishaji, kukuza taaluma na kuongezea uwezo nguvu kazi katika sekta za uzalishaji; na hata kutoa mwanya wa kushughulikia mapungufu au matatizo yatakayoathiri usalama wa chakula na lishe, maendeleo ya vijiji, usalama wa riziki na mapato ya nje
upload_2016-11-10_18-3-41.png


Nimekutana pia na ibara ya 142 inayowapa nafasi pande zote mbili kupitia upya mkataba huu kila baada ya miaka mitano na kutoa mapendekezo ili kurekebisha mahusiano ya kibiashara chini ya mkataba huu kulingana na uzoefu wa miaka mitano iliyoisha. Hivyo kuna nafasi ya mabadiliko kwa baadhi ya masuala

upload_2016-11-10_18-8-40.png


Kwa upande mwingine mkataba huu ni kweli unamapungufu hasa changamoto ya utayari wa nchi yetu kufikia viwango vya kuuza kwa wingi soko la Ulaya. Kwa sasa EBA (Everything But Arms) inatutosha kufurahia fursa za kuuza Ulaya bila kutozwa ushuru wowote. Tukumbuke tu kuwa hatutakuwa na uchumi wa chini siku zote, hivyo tusitukane mkunga na uzazi ungalipo.

Japo kuna changamoto za kuingia mikataba mingine na nchi nyingine ikiwa tutaingia kwenye mkataba huu, siyo kweli kuwa mkataba huu unatuzuia kuingia mikataba na nchi nyingine. Nilichoelewa ni kuwa, Nchi za Ulaya zimeweka sharti la kuwapa wao dili nzuri kwenye baadhi ya bidhaa. Na ikiwa nchi nyingine zitataka dili nzuri zaidi katika bidhaa hizo basi EU wanahaki ya kuomba dili kama hilo. Hii itakuja kutuchanganya kwenye biashara na nchi nyingine kama China na India tunazofanya nazo biashara zaidi.

Kikubwa ni kuwa, tujitahidi kujadili mambo kwa kuangalia uhalisia wa jambo lenyewe na siyo kutumia hisia na siasa kwenye kuamua kila kitu.

Ni hayo tu kwa leo.
 
@suelsmail mimi kama mchumi ngoja nikueleze kwa lugha nyepesi, priorities zinabadilika esp. baada ya mwekezaji mkuu Tanzania the UK kujitoa ndani ya EU. Tukiruhusu huu mkataba uendelee ina maana tunawaminya wale waliowekeza kwa kuwaanika kwa unfair competition toka kwa wale ambao hawajawekeza. Pili sera ya awamu ya tano ni tofauti na zote zilizopita. It is that simple. Kenya wamesaini kwavile wanataka kuvunja jumuiya na kumbuka kukosa pipeline deal kumewaumiza sana. Na pia project ya bandari ya Bagamoyo inawanyima usingizi ila amini hawatafanikiwa.

Haswa kama Uganda watabaki na Tanzania hizi nchi mbili ndo zina strong say kwenye block kwa sasa. The EU can't afford to ignore them.
 
@suelsmail mimi kama mchumi ngoja nikueleze kwa lugha nyepesi, priorities zinabadilika esp. baada ya mwekezaji mkuu Tanzania the UK kujitoa ndani ya EU. Tukiruhusu huu mkataba uendelee ina maana tunawaminya wale waliowekeza kwa kuwaanika kwa unfair competition toka kwa wale ambao hawajawekeza. Pili sera ya awamu ya tano ni tofauti na zote zilizopita. It is that simple. Kenya wamesaini kwavile wanataka kuvunja jumuiya na kumbuka kukosa pipeline deal kumewaumiza sana. Na pia project ya bandari ya Bagamoyo inawanyima usingizi ila amini hawatafanikiwa.

Haswa kama Uganda watabaki na Tanzania hizi nchi mbili ndo zina strong say kwenye block kwa sasa. The EU can't afford to ignore them.
Wewe babu unazeeka vibaya, ikiwa wewe ni mchumi huko tanzania duu hata bibi yangu ni profesa sasa, mbona unatoa analysis ya uharo mtupu...ohh bomba, ooh uk, ooh eac ivunjike¿!!
 
Taarifa za bashe hizoo, kuna barua toka tiss, zingine toka ccm,na alichofanya hadi akapata "uraia"
1478795797022.png
1478795814685.png
1478795830705.png
1478795841045.png
1478795848005.png
 
Taarifa za bashe hizoo, kuna barua toka tiss, zingine toka ccm,na alichofanya hadi akapata "uraia"
1478796217165.png
1478796225675.png
1478796234185.png
1478796242085.png
1478796248296.png
 
Duu hicho chama chenu ni pori la ufusadi, eti bashe ni mnyamwezi wa nzega!! Hahaaa
1478796724013.png
1478796730639.png
1478796741986.png
1478796753250.png
1478796762976.png
 
@suelsmail mimi kama mchumi ngoja nikueleze kwa lugha nyepesi, priorities zinabadilika esp. baada ya mwekezaji mkuu Tanzania the UK kujitoa ndani ya EU. Tukiruhusu huu mkataba uendelee ina maana tunawaminya wale waliowekeza kwa kuwaanika kwa unfair competition toka kwa wale ambao hawajawekeza. Pili sera ya awamu ya tano ni tofauti na zote zilizopita. It is that simple. Kenya wamesaini kwavile wanataka kuvunja jumuiya na kumbuka kukosa pipeline deal kumewaumiza sana. Na pia project ya bandari ya Bagamoyo inawanyima usingizi ila amini hawatafanikiwa.

Haswa kama Uganda watabaki na Tanzania hizi nchi mbili ndo zina strong say kwenye block kwa sasa. The EU can't afford to ignore them.
Nashukuru kwa ufafanuzi.
Mosi, Brexit kweli itaathiri Mengi ikiwamo mahusiano ya kiuchumi. Je suala kujitoa mwanachama kwenye Jumuiya halikutizamwa kwenye mkataba huu?
Pili, kama vipaumbele vya uchumi vimebadilika katika miaka miwili tangu kutia sahihi ya kufunga mjadala, je tutaweza vipi kuhakikisha kuwa mikataba ijayo haitaishia katika hali hii pia? Maana kama hatuwezi kuwa na vipaumbele vyenye maisha marefu, inatia Sana shaka kwenye mikataba mingine tulioingia na tunayoingia.
Huu mkataba Ni picha tosha kuwa watanzania na hata tuliowapa dhamana ya kutuwakilisha kwenye maamuzi mbalimbali wanatuangusha Mara nyingi na wananchi tunaishia kupata maumivu sisi.

Hata hivyo bora kuokoa jahazi kabla hatujatumbukia kuliko kutumbukia na kujuta. ILA tujifunze kuwa wakweli hata tunapokosea na siyo kudanganya umma kufunika makosa yetu au maslahi ya wachache
 
Duuuh watz bwana!, sasa mnanuabudu huyu msomali na baadhi familia ake ipo nairobi, kaka yake anamiliki petrol stations kadhaa in the city. Wengine ndugu zake kama zulekha bashe wapo hargeisa in somaliland!. Huwa mnachefua eti...
Haibu ya ndugu ako akitetea interest za nchi nyingine wakati nyie rushwa inawamaliza. Njoo umchukuee awasaidiee tuna kina bashe wengi wengine wapo mansese.
 
Nyie majamaa wa kwnya mnatakiwa kujua kuwa the ripe moment for tz is not yet. Naona nyie ndio mshakubali kujishogeshaaa...hehehe
 

Umesema kweli kwamba tumeongea nao kwa muda mrefu hadi kufika tulipo sasa, lakini sio kwamba wakati tunayaongea timu yetu haikuwa makini, walikuwa makini na walikuwa wanazuwa hoja za kupinga vipengele vya mkata ambavyo vilikuwa kandamizi. Kila tusema tuaambiwa usijali tutayatatua. Kuna wakati timu yetu ilikuwa nchi uholanzi, watu wetu kila wakiwafata timu ya Kenya kujadili vipengele kabla ya kukutana na wazungu, wakenya na wanajizungusha na kujifanya wako busy. Wenzetu wanaukabila lakini ikija swala la utaifa na kupiga dili, wanashikamana na ukabila unapotea. Mkapa alikuwa ana sema sana kuhusu huu mkataba, sehemu nyingi akipiga safari za ulaya anajaribu kuchomekea na kupinga. Ila kwasababu wenzetu wameweka maslai ya kupinga dili mbele, wanapata kigugumizi ikifika kupinga ukizingatia ni wazungu walio wekeza kwao ndio wanawasukuma kukubali mkataba huu.

Swala lingine ni vipengele vilivyo kwenye mkataba huu, vingi ni kandamizi, vitatuweka kifungoni kiuchumi mpaka hapo na sisi tutakapo fikia viwango kama vyao vya uzalishaji. Lakini wakati huo huo, mkataba huu aujaandikwa kutupa sisi wazawa uwezo wa kufikia vigenzo vyao, upo hapa kuwaruhusu wawekezaji (amabo ni wazungu wenzao) ili watumie ardhi yetu, rasilimali zetu, na masoko yetu kwa manufaa yakwao wenyewe. Kumbuka haya matatizo hapo hata kwenye utalii, watalii wanalipa holiday package huko huko ulaya, wakija hapa wanapokelewa na kampuni ya kigeni inayo tumia hela kiduchu kuwaweka hapa mpaka wanaondoka, walicho tumia hapa hao watalii ni kidogo sana ukilinganisha na walicho lipia kwao. Ndio maana JPM kaweka VAT ili tuwalime na huku pia, hiyo VAT imawauma kwasababu tunagema kile walicho kificha kwao ulaya.

Kuna kipengele kwenye mkataba kinacho tunyima sisi fursa kuuza bidha iliyowekwa thamani kwenye soko lao kwa kisingizio cha viwango vyetu ni duni. Lakini wao wanaruhusiwa kuleta bidha zilizo ongezewa thamani na kuuza kwetu. Tunalima zabibu hapa, tunachuma tunapeleka kwao wao wanturudishia ikiwa kwenye chupa kama wine. Kuna vipengele vya bei, wanataka tukiuza bidha zetu kwa nchi kama india, kwa dola moja, basi na wao tuwauzie kwa dola moja hata kama tunajuwa wanauwezo wa kunua kwa dola tano. Kwa wakenya hawana shida sana, maua hayana haja ya kuongezewa thamani, wanakata shambani, pakia kwenye mfuko, safirisha hadi ulaya, kahawa hivyo hivyo, chai hivyo hivyo. Lakini jiulize, mchina atakubali dili kama hiyo, au mmarekani? Umasikini wetu usiwe kigezo cha kujingiza kwenye mikataba iso na tija, rasilimali tunazo nyingi na hatujaanza kuzitumia, ukanda wote wa bahari ni rasilimali yenye mapana na marefu, kuanzia uvuvi, utalii, mafuta na gesi, usafirishaji, ujenzi wa meli za aina zote, ufugaji wa samaki uzalishaji wa magugu ya baharini mpaka usalishaji wa umeme unawezekana. Kilimo ndio kwanza tuajenga kiwanda cha matreka, huko nako fursa hazina mwisho. Maziwa makuu ni fursa, utali ni fursa kubwa na pana. Usafiri wa aina zote. Viwanda ndio usiseme, kwa kifupi mkataba huu kwa sasa utatunyima uwezo wa kujihinili kiuchumi na utatufanya tuendele kuwa tegemezi, Kenya hawana rasilimali nyingi na tukikubali huu mkataba wawekezaji wazungu na wazawa wa kenya watakimbikia huku kwetu kwa mwamvuli wa EAC na kusafirisha kila kitu ulaya. Unaweza kuuliza kwani kuna ubaya gani hapo kama tuna pata pesa. Ujuwe hali hiyo haita tusaidia katika kuinua vipaji na kumiliki uchumi wetu, kila siku tutakuwa tunanyeyekea watu wa nje wakati wa kwetu wanadumaa. Numba ya watanzania kinaongezeka kwa haraka sana tusipo watengenezea mazingira ya kumiliki uchumi wao na wao watazaliwa wakiwa watumwa kama sisi.
 
Serikali bhana.ule muswada wa vyombo vya habari.wameupitisha fasta fasta.wakati yote ni majanga
 
Umesema kweli kwamba tumeongea nao kwa muda mrefu hadi kufika tulipo sasa, lakini sio kwamba wakati tunayaongea timu yetu haikuwa makini, walikuwa makini na walikuwa wanazuwa hoja za kupinga vipengele vya mkata ambavyo vilikuwa kandamizi. Kila tusema tuaambiwa usijali tutayatatua. Kuna wakati timu yetu ilikuwa nchi uholanzi, watu wetu kila wakiwafata timu ya Kenya kujadili vipengele kabla ya kukutana na wazungu, wakenya na wanajizungusha na kujifanya wako busy. Wenzetu wanaukabila lakini ikija swala la utaifa na kupiga dili, wanashikamana na ukabila unapotea. Mkapa alikuwa ana sema sana kuhusu huu mkataba, sehemu nyingi akipiga safari za ulaya anajaribu kuchomekea na kupinga. Ila kwasababu wenzetu wameweka maslai ya kupinga dili mbele, wanapata kigugumizi ikifika kupinga ukizingatia ni wazungu walio wekeza kwao ndio wanawasukuma kukubali mkataba huu.

Swala lingine ni vipengele vilivyo kwenye mkataba huu, vingi ni kandamizi, vitatuweka kifungoni kiuchumi mpaka hapo na sisi tutakapo fikia viwango kama vyao vya uzalishaji. Lakini wakati huo huo, mkataba huu aujaandikwa kutupa sisi wazawa uwezo wa kufikia vigenzo vyao, upo hapa kuwaruhusu wawekezaji (amabo ni wazungu wenzao) ili watumie ardhi yetu, rasilimali zetu, na masoko yetu kwa manufaa yakwao wenyewe. Kumbuka haya matatizo hapo hata kwenye utalii, watalii wanalipa holiday package huko huko ulaya, wakija hapa wanapokelewa na kampuni ya kigeni inayo tumia hela kiduchu kuwaweka hapa mpaka wanaondoka, walicho tumia hapa hao watalii ni kidogo sana ukilinganisha na walicho lipia kwao. Ndio maana JPM kaweka VAT ili tuwalime na huku pia, hiyo VAT imawauma kwasababu tunagema kile walicho kificha kwao ulaya.

Kuna kipengele kwenye mkataba kinacho tunyima sisi fursa kuuza bidha iliyowekwa thamani kwenye soko lao kwa kisingizio cha viwango vyetu ni duni. Lakini wao wanaruhusiwa kuleta bidha zilizo ongezewa thamani na kuuza kwetu. Tunalima zabibu hapa, tunachuma tunapeleka kwao wao wanturudishia ikiwa kwenye chupa kama wine. Kuna vipengele vya bei, wanataka tukiuza bidha zetu kwa nchi kama india, kwa dola moja, basi na wao tuwauzie kwa dola moja hata kama tunajuwa wanauwezo wa kunua kwa dola tano. Kwa wakenya hawana shida sana, maua hayana haja ya kuongezewa thamani, wanakata shambani, pakia kwenye mfuko, safirisha hadi ulaya, kahawa hivyo hivyo, chai hivyo hivyo. Lakini jiulize, mchina atakubali dili kama hiyo, au mmarekani? Umasikini wetu usiwe kigezo cha kujingiza kwenye mikataba iso na tija, rasilimali tunazo nyingi na hatujaanza kuzitumia, ukanda wote wa bahari ni rasilimali yenye mapana na marefu, kuanzia uvuvi, utalii, mafuta na gesi, usafirishaji, ujenzi wa meli za aina zote, ufugaji wa samaki uzalishaji wa magugu ya baharini mpaka usalishaji wa umeme unawezekana. Kilimo ndio kwanza tuajenga kiwanda cha matreka, huko nako fursa hazina mwisho. Maziwa makuu ni fursa, utali ni fursa kubwa na pana. Usafiri wa aina zote. Viwanda ndio usiseme, kwa kifupi mkataba huu kwa sasa utatunyima uwezo wa kujihinili kiuchumi na utatufanya tuendele kuwa tegemezi, Kenya hawana rasilimali nyingi na tukikubali huu mkataba wawekezaji wazungu na wazawa wa kenya watakimbikia huku kwetu kwa mwamvuli wa EAC na kusafirisha kila kitu ulaya. Unaweza kuuliza kwani kuna ubaya gani hapo kama tuna pata pesa. Ujuwe hali hiyo haita tusaidia katika kuinua vipaji na kumiliki uchumi wetu, kila siku tutakuwa tunanyeyekea watu wa nje wakati wa kwetu wanadumaa. Numba ya watanzania kinaongezeka kwa haraka sana tusipo watengenezea mazingira ya kumiliki uchumi wao na wao watazaliwa wakiwa watumwa kama sisi.

Mwanzi1 ufafanuzi wako nimeuelewa. Ilihitajika pia kuwe na uelewa wa mazungumzo/majadiliano yalikuwaje. Ndio maana kuna umuhimu wa kuweka wazi mikataba ya kimataifa kuondoa utata kwa wananchi pia.

Je unaweza kutufahamisha malengo ya sisi kukubali kujadiliana mkataba huu tangu mwanzo? Tulikuwa tunataka kufaidika na nini hasa? Tulileta nini mezani (What was our leverage)? Maana miaka kumi ni mingi kwa majadiliano, halafu kuja kuyapinga makubaliano mwishoni. Naona kuna haja ya kujifunza michakato ya mikataba ya kimataifa 🙂

Pia nakubaliana na wewe kuwa tusikubali kuburuzwa au kunyonywa kwasababu yoyote ile. Hata hivyo tuwe na dira ya nini tunataka na siyo kuwa na vipaumbele vinavyobadilika badilika kila mara. Tukiwa na dira ya muda mrefu, tutaweza pia kuwa na mikakati thabiti na kuisimamia katika majadiliano kama haya. Vile vile, tuache kujifungia kwa kuwa hatuko tayari, tujitayarishe! Kama mpaka leo elimu yetu, sera na mipango yetu, sheria, miundo mbinu, maamuzi ya viongozi na wadau, nk. havijalenga kututayarisha kujitegemea, kukuza ujuzi na kuhamasisha ugunduzi na uzalishaji wa ndani; tutaimba wimbo huu huu miaka hamsini ijayo. Na kipindi hicho hakuna kitakacho zuia Wakenya au nchi nyingine kuendelea kufaidika na rasilimali zetu, hata kama tukijenga ukuta kuzunguka nchi nzima!
 
SueIsmael ....Ndio tumejadiliana kwa muda mrefu, lakini watu lazima waelewe kwamba katika hiyo miaka kumi, sio kama majadiliano yalikuwa yanakwenda smooth halafu dakika ya mwisho ndio tukarupuka na kusema hatu sahini. We've been raising flag every time we came across an issues which is not in fervour. Na ikumbukwe kwamba kuna vipengele tulivyo kuwa tunavukubali na vina tija kwetu kama biashara huru au soko huru, lakini tatizo linakuja kwenye vitu ambavyo vinatukwaza na ambavyo ni muhimu zaidi kwetu. Nia kubwa yetu ilikuwa ni kuwa na Uhuru wa kutumia rasilimali zetu kadiri tunavyo taka. Na wenzetu walitaka zaidi wachukuwe wao rasilimali zetu na kuhamisha kazi zote ambazo sisi tungezifanya kutoka huku kwetu na kuzipeleka kwao. Mfano, tunalima mawese, wenzetu wanakuja kununuwa mawese "ghafi" kutoka mkulima na kusafirisha hadi ulaya. Mawese yana ingizwa kiwamdani na kuchakachuliwa kama mafuta, mafuta yale yana pelekwa kwenye viwanda vingine kama chakula, sabuni, mafuta ya kujipaka, dawa nk. Hapo kuna kazi nyingi sana zimezalishwa Ulaya, wakati sisi watu wetu wamekaa tuu hawana chakufanya zaidi ya kulima mawese. Sasa kama tukiwa na Uhuru wa kutumia rasilimali zetu tunavyo taka, huoni kama hivyo viwanda vingekuwa huku kwetu vina tengeneza ajia nyingi kwa watu wetu?. That is only one example, Mh. Zitto alisema the devil is in the details, mkataba huu hautupi hata Uhuru wa kupanga bei ya bidhaa zetu, tuna nyimwa uhuru wa kuongea na maeneo mengine ya kibisha mpaka wao wao watupe kibali, bidhaa za kutoka kwao hazita lipiwa ushuru kwa asililia tisini, na mengine mengi tuu ambayo ni kandamizi. This was design to make us slaves to a white man again, kwamba tunakila kitu, lakini hatutakiwi kujuwa kama tulicho nacho ni thamani.

Tusione aibu kwamba wenzetu wamesahini sisi tunajivuta vuta, tume lalamika sana, lakini inafika wakati unajiuliza hawa wenzetu tukonao upande mmoja au ni double agent. Maana tumewaomba sana watuelewe na wajadili haya tunayo yapinga lakini wanaruka ruka tuu, mpaka mgogoro wa magari ya utalii, shinikizo lilikuwa ni hilo hilo, kwamba ukitukatalia sisi tutakuminya kiuchumi, wakati wanasahau kwamba hata sisi timeshika mpini.

Dira ya taifa ipo, na tunajiweka sawa kwenye miundo mbinu. Wakati taifa letu linatawaliwa na wakoloni, wakoloni hawakulichukulia taifa hili kama koloni, sisi tulikuwa kama eneo lakushikilia tuu kama ngome, hali hiyo inajidhirisha kwenye miundo mbinu tuliyo achiwa na wakoloni. Wenzetu walio tawaliwa na wakoloni wameachiwa vitu vingi sana tofauti na sisi. Tulipo fika leo, ni jitiada zetu wenyewe, tumepata changamoto nyingi huko nyuma, lakini huu ni Wakati wa kijipanga upya na kujenga uchumi huru na haki.
 
Back
Top Bottom