Tanzania yafuzu hatua ya Robo fainali, Kombe la dunia la Wanawake Chini ya Miaka 17

Tanzania yafuzu hatua ya Robo fainali, Kombe la dunia la Wanawake Chini ya Miaka 17

Bila bila

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2016
Posts
22,168
Reaction score
39,118
Timu ya Taifa ya wanawake U17 Serengeti Girls imefanikiwa kufika hatua hiyo baada ya kutoka sare ya goli 1-1 dhidi ya Canada katika michuano inayoendelea Nchini India.

Matokeo hayo ya Kundi D yameiwezesha Tanzania kuwa na pointi 4 na kushika nafasi ya pili nyuma ya Japan iliyoongoza kundi kwa kuwa na pointi 9, huku Ufaransa na Canada zikiaga mashindano.

===========

Leo afe kipa afe beki ushindi au Sare inatupeleka Robo fainali.

C67684E1-E34C-4AAF-BBA8-62CE09AD3AFC.jpeg


=======
15’ Canada wanapata bao kupitia kwa Amanda Allen

36’ Tanzania wanasawazisha kupitia kwa Veronica Mapunda

70’ Tanzania 1 - Canada 1

85’ Tanzania 1 - Canada 1

88’ Tanzania 1 - Canada 1

Dakika 6 zimeongezwa

Mpira umekwisha, Tanzania (Serengeti Girls) imefuzu kucheza hatua ya Robo fainali dhidi ya Colombia.
 
Tunaupiga mwingi, tuko 1-1, hawa Canada walipata penati dakika ya 14 ila dakika ya 35 tukasawazisha.

Matokeo yakibaki hivi tunafuzu
 
Jinsi tunavyoshambuliwa wanaeza kupata bao Canada
 
Mabinti zetu U 17 wametoka draw 1-1 na Canada. Hivyo wametinga robo fainal. Kongole nyingi kwao[emoji120][emoji122][emoji122][emoji123][emoji91]
 
Back
Top Bottom